Kwanini Nyerere hakuweka vituo vya kijeshi kwenye nchi alizozisaidia kupata uhuru?

Kwanini Nyerere hakuweka vituo vya kijeshi kwenye nchi alizozisaidia kupata uhuru?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Marekani ina jumla ya vituo vya Kijeshi (overseas military bases) 38 katika mataifa mbalimbali! Ukiacha Marekani, kuna mataifa mengine zaidi ya kumi na tano yenye vituo vya kijeshi sehemu tofauti tofauti.

Ni gharama sana kulihudumia Jeshi. Ukiona nchi inaamua kuanzisha vituo vya kijeshi nje ya mipaka yake, ujue inapata faida inayoendana na gharama inayoingia.

Ndiyo maana nchi ndogo kama Singapore nayo ina vituo vya kijeshi katika nchi mbili, Brunei na Taiwan.

Kwa jinsi Tanzania ilivyozisaidia nchi nyingi Afrika kupata uhuru, ilikuwa rahisi sana kwa Tanzania kuweka vituo vyake vya kijeshi huko. Kwa sasa tungekuwa na military bases Msumbiji, Zimbabwe, Comoro, Uganda, Afrika Kusini, Angola, Namibia, n.k.

Ingawa si nchi zote Tanzania ilishiriki moja kwa moja kuzisaidia kupata uhuru, lakini mchango wa Tanzania bado ni mkubwa, hata kwa amani zinazofurahiwa na hizo nchi kwa sasa. Nani asiyefahamu, kwa mfano, kuwa Tanzania ndiyo iliyomuondoa Dikteta Amin Uganda?

Fedha, muda, ardhi, na rasilimali nyingine za Watanzania zilisaidia nchi nyingi za Afrika kupata uhuru. Si vitu tu, lakini pia na wanajeshi wa Tanzania. Tena, kuna waliopoteza maisha kwenye hizo "operation".

Japo sijajua kwa undani faida ya hivyo vituo vya kijeshi, lakini naamini kuna maslahi nchi inayoweka huko vituo vya kijeshi inayapata. Inasemekana Paul Kagame ameshaweka vituo vyake vya kijeshi katika mataifa mawili hapa Afrika, Msumbiji na Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Kitendo cha Kagame kufanya hivyo ni ishara tosha kuwa kufanya hivyo kunawanufaisha. Si unajua Kagame ni "Mjasiriamali?" Anaweza kuziona fursa ambazo wengine hawazioni.

Kama Nyerere angeamua kuweka vituo vya kijeshi, inawezekana ingetunufaisha kama nchi. Labda,

1. Tungeweza kurudisha gharama zilizotumika kugharamia vita vya ukombozi kwenye hizo nchi!

2. Nchi ingeweza kutumia ushawishi wa Jeshi letu katika nchi husika kutengeneza fursa zitakazowasaidia Watanzania kunufaika huko!

3. Jina la Tanzania lingekuwa kubwa zaidi ya ilivyo sasa

Naweza nisiwe sahihi sana, lakini ninafikiria hizo zinaweza zikawa miongoni mwa faida ambazo tungezipata!

Kwa nini mzee wetu, J. K. Nyerere hakuliona hilo?
 
1. Tungeweza kurudisha gharama zilizotumika kugharamia vita vya ukombozi kwenye hizo nchi!

2. Nchi ingeweza kutumia ushawishi wa Jeshi letu katika nchi husika kutengeneza fursa zitakazowasaidia Watanzania kunufaika huko!

3. Jina la Tanzania lingekuwa kubwa zaidi ya ilivyo sasa

Naweza nisiwe sahihi sana, lakini ninafikiria hizo zinaweza zikawa miongoni mwa faida ambazo tungezipata!

Kwa nini mzee wetu, J. K. Nyerere hakuliona hilo?
I say, haya ndio malengo ya kuwa na vituo vya kijeshi mahali? Kweli akili ni nywele. Hebu tufafanulie. Kwa mfano, kuwa na kituo cha kijeshi Msumbiji kungetusaidiaje kurudisha gharama zilizotumika kugharamia vita vya ukombozi kwenye hiyo nchi?
 
nchi ilikuwa hata haijiwezi sembuse kambi za kivita sehemu zingine .....kimsingi nyerere aliyoyafanya ni yaa maana kwa kipindi kile
 
I say, haya ndio malengo ya kuwa na vituo vya kijeshi mahali? Kweli akili ni nywele. Hebu tufafanulie. Kwa mfano, kuwa na kituo cha kijeshi Msumbiji kungetusaidiaje kurudisha gharama zilizotumika kugharamia vita vya ukombozi kwenye hiyo nchi?
Kujijenga kisiasa, kiuchumi na hata kiushawishi kwenye eneo husika lazima kudhibiti kijeshi kichinichini au moja kwa moja.
Hata hivyo, hoja ya uwezo wa kiuchumi inajibiwa kwa kutumia hivyo vituo kuwawezesha wananchi wako (private sector) kutumia hivyo vituo kujiimarisha katika eneo hilo.
Siyo mambo yote huandikwa kwa watu wenye akili.
 
Kujijenga kisiasa, kiuchumi na hata kiushawishi kwenye eneo husika lazima kudhibiti kijeshi kichinichini au moja kwa moja.
Hata hivyo, hoja ya uwezo wa kiuchumi inajibiwa kwa kutumia hivyo vituo kuwawezesha wananchi wako (private sector) kutumia hivyo vituo kujiimarisha katika eneo hilo.
Siyo mambo yote huandikwa kwa watu wenye akili.

Sawa, kama mambo huyaelewi ni bora kuyaacha, maana unacopendekeza hapa hakina hata sense yeyote. Ni kufikiri kwa mtoto wa darasa la tatu
 
Sawa, kama mambo huyaelewi ni bora kuyaacha, maana unacopendekeza hapa hakina hata sense yeyote. Ni kufikiri kwa mtoto wa darasa la tatu
Labda tunaishi sayari tofauti, kwa hili hata wale mababu zetu ambao hawakupata elimu ya darasani walilielewa.
Kwa nini usitumie akili (kama unayo) kunijibu?
 
Labda tunaishi sayari tofauti, kwa hili hata wale mababu zetu ambao hawakupata elimu ya darasani walilielewa.
Kwa nini usitumie akili (kama unayo) kunijibu?
Ni ngumu sana kujibu kwa kutumia akili kitu ambacho kimeandikwa bila kutumia akili. Kwa mfano, wewe unasema Kagame ameweka kituo cha kijeshi Msumbiji. Sasa inabidi nianze kwa kukueleza kile sio kituo cha kijeshi bali kikosi cha jeshi kufuatia ombi la Msumbiji kwa Kagame kupambana na waasi wa Msumbiji. Wakimaliza operation wanaondoka. Kuna wakati tulikuwa na majeshi Uganda, sio kituo cha kijeshi.

Na pia unapoweka kituo cha kijeshi lengo ni kujihami sio kuchuma faida za kiuchumi katika nchi, na hupati faida bali unaingia gharama kuilipa nchi uliyoweka majeshi na kuhudumia jeshi lako huko nje. Na hulazimisi, bali unakubaliana na nchi kuweka kituo cha kijeshi, na mara nyingine wakijua utawasaidia katika ulinzi wa nchi yao. Sasa sisi tuwe na kituo cha kijeshi South kusaidia ulinzi wa South Africa, unalijua jeshi la South lilivyo?

Na pia lazima uwe na "perceived enemy" na unaweka kituo cha kijeshi katika nchi fulani kama defensive au offensive strategy. Sasa sisi tuweke kituo cha kijeshi South Africa, nani ni perceived enemy wetu katika eneo lile?
 
Kipindi hicho uchumi wetu ulikuwa hauruhusu..
Nilisoma hzo pumba zake nikaraka kumjibu ila ushaliandika jibu na zaid hata hv sasa hatuna hao wanaoitwa wanajeshi wenye ushawishi kama unajua recruitment ya hao wanaoitwa waushawishi asinge andika uji wake hapa je wajua taifa la US na hao wengne wana umri gani compere to SS mengn angeshirikisha akili
 
Wewe ndio ungetoa fedha za kuhudumia hayo majeshi huko?
 
Bajeti ya jeshi la marekani mwaka jana lilikuwa $916b
Sisi tukaweke kambi kwenye nchi za watu kwa kujilinda na nani? Au tunamlinda nani?
Maumivu ya Ug mpaka leo akili hazijakaa sawa
 
Hahaha Nyerere alikuwa ma jeshi au Sungu sungu.

Marekani ina jeshi, na vifaa pia.
 
Mkuu gharama za kuendedha hizo kambi za kijeshi Tanzania isingeweza!
Huwezi ukalinganisha na nguvu ya US.
 
Ni ngumu sana kujibu kwa kutumia akili kitu ambacho kimeandikwa bila kutumia akili. Kwa mfano, wewe unasema Kagame ameweka kituo cha kijeshi Msumbiji. Sasa inabidi nianze kwa kukueleza kile sio kituo cha kijeshi bali kikosi cha jeshi kufuatia ombi la Msumbiji kwa Kagame kupambana na waasi wa Msumbiji. Wakimaliza operation wanaondoka. Kuna wakati tulikuwa na majeshi Uganda, sio kituo cha kijeshi.

Na pia unapoweka kituo cha kijeshi lengo ni kujihami sio kuchuma faida za kiuchumi katika nchi, na hupati faida bali unaingia gharama kuilipa nchi uliyoweka majeshi na kuhudumia jeshi lako huko nje. Na hulazimisi, bali unakubaliana na nchi kuweka kituo cha kijeshi, na mara nyingine wakijua utawasaidia katika ulinzi wa nchi yao. Sasa sisi tuwe na kituo cha kijeshi South kusaidia ulinzi wa South Africa, unalijua jeshi la South lilivyo?

Na pia lazima uwe na "perceived enemy" na unaweka kituo cha kijeshi katika nchi fulani kama defensive au offensive strategy. Sasa sisi tuweke kituo cha kijeshi South Africa, nani ni perceived enemy wetu katika eneo lile?
Sasa na tuanze kusaidiana kutumia akili;
1. Sijaandika habari za majeshi ya Rwanda nchini Msumbiji. Hoja yangu ilikuwa general kwenye faida za nchi kuweka vituo vya kijeshi kwingine. Uwepo wa enemies (perceived or offensive) ni theories za kujiimarisha kiulinzi wa kimapigano zaidi kuliko wa kijamii na kiuchumi (old fashioned against new).
2. Hivi unafikiri uwepo wa majeshi ya ufaransa na nchi nyingine za magharibi huku Africa kuna maadui zao perceived na offensive?
 
Back
Top Bottom