Kwanini nyumba za NHC bei iko juu?

Kwanini nyumba za NHC bei iko juu?

suwaulize nani kakwambia Kuwa humu kuna office zao

yotr haya ni madhara ya kuto jua matumizi ya mitandandao ya kijamii, nadhani wewe ni limbukeni na utoto unakusumbua, kama ndio hivyo basi habari zote zingekuwa zinapelekwa sehemu husika na sio kujadiliwa huku. Shwain
 
naona topic inakimbiza kwenye kutolewa hatuwezi hata kuhoji sikuhizi
 
Kwani kwa watu binafsi hali ipoje? Maana kuna jamaa hapa Songea kauza nyumba yake yenye bedroom 3, sebule, jiko, store na public toillet kwa shilingi milioni 65. Naona hawa wa NHC wanauza kwa bei nafuu sana ukizingatia kuwa nyumba wanajenga kwa kiwango cha hali ya juu. Yaani ukinunua nyumba ya NHC hutegemei kufanya ukarabati kwa siku za karibuni kwani wanatumia vifaa bora sana. Mie nimenunua moja hapa Songea na kwa hakika ubora wake ni wa hali ya juu
Za kule mkuzo vyumba viwili au?
 
Nhc iko chini ya wizara ya ardhi lakini wizara ya ardhi haimiliki ardhi,ardhi inamilikiwa na halmashauri na wananchi wizara kazi yao ni kusimamia sheria ya ardhi na kutunga sera ikiwa ni pamoja na kusimamia matumizi sahihi ya ardhi

sasa unasemaje kuwa anauziwa bei kubwa wakati valuer ndio muuzaji na mnunuaji?kwani halmashauri na wizara au serikali wanatofauti gani?

ukweli ulio wazi kuwa ile ni biashara ya wakubwa wala sio kukomboa wananchi.labda kwa watumishi wa umma wenye mikataba ya maisha kazini.
 
Hakuna mwananchi mwaminifu muadilifu mwenye uwezo wa kununua nyumba za NHC zenye bei ya mamilioni. Tahadhari yangu ni kwamba nchi inauzwa vipande vipande kwa wahindi, waarabu, wachina n.k. kupitia shirika hili la kifisadi la NHC.
 
Njoo mbagala nikupe kiwanja, Huko ni nji ingine, , mimi nitahamia mbande!
 
Nakuunga mkono kwa asilimia zote. Najiuliza hivi hakuna hata kiongozi mmoja pamoja na Rais na wabunge ambaye haoni kwamba NHC haisaidii hao watu wanaotajwa? Mfanyakazi anayepata mshahara 4m ndiye anaweza kukopa pesa hiyo akanunua nyumba hizo,nje ya hapo anakuwa ameiba.
 
ni ndoto kwa mtanzania wa kipato cha chini kumiliki hizi nyumba mi naonaga mazingaombwe tu na hadaa tu
 
Hawa jamaa materials wanazyotumia kujengea hizi nyumba hata ukijumlisha ufisadi bado hazikutakiwa kuvuka milioni ishilini, hizi bei zinazouzwa utafikiri wanauziwa wauza sembe.
 
Kwani kwa watu binafsi hali ipoje? Maana kuna jamaa hapa Songea kauza nyumba yake yenye bedroom 3, sebule, jiko, store na public toillet kwa shilingi milioni 65. Naona hawa wa NHC wanauza kwa bei nafuu sana ukizingatia kuwa nyumba wanajenga kwa kiwango cha hali ya juu. Yaani ukinunua nyumba ya NHC hutegemei kufanya ukarabati kwa siku za karibuni kwani wanatumia vifaa bora sana. Mie nimenunua moja hapa Songea na kwa hakika ubora wake ni wa hali ya juu
Peleka Mipasho ya Hadija Kopa kule!
 
Ramani ya kizamani

Kinyumba cha vyumba 2 na sebule, bei milioni 55.

Hawa watu wana dunia yao kabisa
 
Mkuu mimi ninavyojua ni kuwa nhc wanalipa kodi kama kawaida ndiyo maana wana charge hela nyingi katika uuzaji wa nyumba zao na pia shirika linajiendesha kibiashara kwa kuwa hawapati ruzuku tofauti na tbc ccm,hata viwanja vipya wanavyopita wanauziwa at market price au wanaingia ubia na wauzaji huwezi amini mpaka katika halmashauri wanwauzia au wanaingia ubia now a days there is no free lunch.
NHC hawalipi property tax badala yake wanalipishwa wapangaji ingawa wao sio owner
 
Mkuu mimi ninavyojua ni kuwa nhc wanalipa kodi kama kawaida ndiyo maana wana charge hela nyingi katika uuzaji wa nyumba zao na pia shirika linajiendesha kibiashara kwa kuwa hawapati ruzuku tofauti na tbc ccm,hata viwanja vipya wanavyopita wanauziwa at market price au wanaingia ubia na wauzaji huwezi amini mpaka katika halmashauri wanwauzia au wanaingia ubia now a days there is no free lunch.
Pambana ujenge ya kwako !! Acha kulia lia nyumba za serikali nao huduma huku zinatakiwa zijiendeshe.....pambana jenga hata vyumba 2 hamia.....waavhie wenye meno.....
 
Ni kweli hawa jamaa wana act very funny.....shirika ni la uma lakini walengwa wao ni tabaka fulani tu la uma huo...ni ukichaa kusema unauza nyumba kwa bei nafuu ya sh 40ml, nina mashaka kama kweli serikali na shirika lake wanajua hali ya wanainchi wake.

Hata za kupanga nazo ni vichekesho tu....hivi tabaka la wenye uwezo wa kulipa laki mbili na nusu kwa mwezi ni asilimia ngapi ya Watanzania mil 45 ?

Matokeo yake nyingi ya nyumba za kupanga na zile zina/zilizouzwa (haswa mijini) zimehodhiwa na wenye nafasi na uwezo waoduka au fletish milioni nne kwa ...na wao ndio wanakuwa mtu wa kati.....kwa kupanga au kununua.
Ngoja majengo ya Msimbazi yakimalizika uone kodi juuu. Hapo wataishi matajiri tu wanaoweza kulipa mamilioni
 
Pambana ujenge ya kwako !! Acha kulia lia nyumba za serikali nao huduma huku zinatakiwa zijiendeshe.....pambana jenga hata vyumba 2 hamia.....waavhie wenye meno.....
Hata serikali siyo ya baba yako.

Serikali ni kwaajili ya kila mtu.

Hao unaowaita wasio na meno ndio kila kitu ikiwemo serikali inawategemea
 
Wadau labda ni mimi tu lakini sijaelewa ni kwanini nyumba za NHC ni ghali sana ukizingatia kwamba hawanunui viwanja na hawalipi tax.

NHC wanabomoa nyumba ambazo Watanzania wanapanga kwa bei nafuu na kutengeneza nyumba kwenye viwanja hivyohivyo nyumba za bei ya juu sana bila kujua sababu ya gharama ya juu.

Kama kweli NHC ni shirika la serikali na linapata viwanja bure na wakati mwingine kuchukuwa viwanja vya Watanzania kwa manufaa ya uma basi wawekewe kiwango cha faida mfano gharama za ujenzi +15% badala ya utaratibu wa sasa ambao ni wa kuleta faida zaidi badala ya kusaidia wananchi.
Nyumba ambayo inagharimu milioni let say 30. NHC wanauza nyumba hiyohiyo kwa milioni 90-100. Na kwao wanadai hizo ni nyumba za bei nafuu

Miradi ya watu hiyo
 
Back
Top Bottom