......gagnija ..inawezekana wewe sio mkatoliki ..lakini kwa kifupi kanisa katoliki huwa halitegemei wala kukubali kumtegemea muumini mmoja kwa mapato....hata kama unayo pesa ya kujenga na kulisha kanisa lote peke yako hawatakubali zaka yako peke yako...kwani kanisa ni la watu wote,mkapa anajuwa utaratibu huo...hata kama anatoa sadaka atakuwa kama waumini wengine wenye uwezo tu....
nikirudi kwenye mada ...nemebahatika kupata huduma za makadinali RUGAMBWA na PENGO....wote walikuwa na mshango mkubwa kila mmoja kwa wakati wake.
Wakati wa utawa wa cardinal pengo ...ndio wakati serikali iliruhusu kanisa kuendelea na huduma za shule na hospitali,amefanikiwa kiasi kikubwa kujenga mashule mengi .....sasa hivi hapa dar karibu kila parokia inayo shule.....na kila kitongoji kuna kanisa...amefanya juhudi kubwa sana kuunganisha nguvu za waamini,...
amefanikiwa kwa upande wa upashanaji habari kwa kuanzisha magazeti na kuimarisha redio [au uanzisha]....na kuanzisha televisheni .
mahospitali yamefunguliwa kwenye parokia nyingi.....
kwa kushirikiana na maaskofu wengine ...baada ya kuruhusiwa na serikali ndani ya miaka 15 ....wameweza kuimarisha hospitali ya rufaa ya BUGANDO,....pia wameweza kuimarisha hospitali zao zilizoenea kila wilaya nchini[ambazo nyingi ndio zinatumiwa na serikali kutoa huduma ya hospitali za wilaya kwenye maeneo ambayo bado serikali haina hospitali zenye hadhi hiyo.....
katika kipindi hicho wameweza kujenga vyuo vikuu ,iringa,mwanza,moshi,etc...vyote vikijulikana kama st.augustine... pia wameweza kujenga chuo kikuu cha teknelojia dar es salaam [st.joseph college of engineering and technology]...tunawashukuru maaskofu,mapadre,watawa,waumini na wote wenye mapenzi mema kwa mafanikio hayo makubwa...ambayo mengi yametokana na juhudi za ndani na michango ya waumini...hasa katika enzi hizi ambazo misaada kutoka ulaya kuendesha makanisa imeshakoma.....na misaada mingi kutoka rome inaelekea sehemu zenye maafa ya vita,...etc[ie congo,east europe,darfur etc]