Kwanini Polisi walishindwa kuifichia aibu familia ya Mzee David Makerege? Yesu aliwaambia "asiye na dhambi miongoni mwenu awe wa kwanza kumtupia jiwe"

Samahani kidogo, hiv huyu mzee alikuwa ni kigogo fulani mkubwa wa serikali/mtu fulan maarufu mpaka habari yake imetrend hivi au ni mtu qa kawaida upepo mbaya tu umemwelekea habari yake ikavuma hiv?
Sina jibu sahihi mkuu
 
Alikufa binti wa ndugu yangu na Polisi hawakusema kwenye media
 
Hakuna mahali amevunjiwa heshima,kilichoripotiwa ni kifo chake na mazingira ya kutokea kwake kwisha.Au ulisikia Polisi anasema marehemu alikosea kulala na mjukuu wake?
Huyu mzee angekuwa na mtoto Police OCD mngeweza kumtaja kwenye media?
 
Sio kila tukio linapaswa kutolewa report kwa umma kwa njia zinazofanana.

Polisi heshimuni wazee. Wazee ndio walioijenga Tanzania mpaka hapa ilipofikia.
 
Police hawakutoa taarifa ila iliyoleak ni ile Document halali ya Police, ambapo ni kosa kubwa maana taarifa inayosambaa ni ile ripoti iliyoandikwa na Askari wetu aloyeshuhudia tukio!
Inasikitisha sana mkuu...
 
Kwani wanaokamatwa kwa ujambazi au utapeli au rushwa familia zao hazidhaliliki?ulishawahi kuona sio sawa?
Polisi ikiua majambazi huwa hawawataji majina. Watoto walioathirika katika kesi ya babu Seya mbona Polisi hawakuwataja majina?...
 
Ni Vema ukafahamu kwamba polisi Wanatoa taarifa kwa makusudio makuu mawili,kwanza kuuhabarisha umma ambao ni Wajibu wa kila taasisi, pili kutoa funzo au onyo ya tabia au mienendo fulani.
Sawa wametoa taarifa, sasa kulikuwa na ulazima gani wa kutaja majina ya yule mzee? Kwani bila majina jamii haiwezi kujifunza?...
 
Linaporipotiwa tukio la ujambazi au wizi fulani ni kuuambia umma ukae macho juu ya wizi wa namna hiyo,unaposikia polisi wameua majambazi kadhaa ni kuwapa onyo Wezi wengine na wale wenye nia ya kuingia kwamba watauawa
Mbona hao majambazi baada ya kuuwawa huwa hawatajwi majina yao? Kesi ya babu Seya wale watoto hawakutajwa majina, kwanini?...
 
Polisi wanaongozwa na PGO Ndio inamuongoza RPC kutoa taarifa ya Matukio yote katika eneo lake.huo mfano wako wa maneno ya Yesu ni irrelevant Kwasababu hawaongozwi na Bibblia au Quran.
Kazi za Polisi ni kufuata PGO pamoja na hekina na kuheshimu wazee waliowazidi umri mkuu...
 
Nakumbuka Chenge na Ditopile kukumbwa na mikasa ya kusababisha vifo huku wakiwa na vidosho vyao pembeni. Na iliripotiwa hivyo japo yawezekana taarifa zilichujwa.
Kwa bahati mbaya sana hii sikuwahi kuisikia mkuu
 
mhhh...
 
Una hoja hapa,.

Ila mimi nilipoona kinachosambazwa kinafanana na "radio call" ya kipolisi nilichoka kabisa
 
Huyu mzee angekuwa na mtoto Police OCD mngeweza kumtaja kwenye media?
Malima ambae Sasa hivi ni Mkuu wa Mkoa wa Mara,aliibiwa silahaa na pesa na Malaya Guest ,na taarifa ziliiandikwa kwa vyombo vya habari, Ditopile pia alifia Nyumba ya Wageni na taarifa zake pia ziliandikwa kwa vyombo vya habari!! Tena kipindi hicho Smart phone zilikua bado hazijaanza!!
 
Alichopata huyo mzee ni stahiki yake. Sisi tunasema hivi ukimstiri Mola wako na yeye anakustiri.

Ukifatilia utakuta alifanya matukio mara kibao, ila wakati ulipofika yakamkuta yakumkuta. Amepata mwisho mbaya sana huyo mzee.

Mola wetu tujaalie mwisho mwema.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…