Kwanini Rais Samia kakwepa Hoja za Wafanyakazi na kamtuma Makamu wa Rais wakati Rais wa Zanzibar yeye amevunja ziara kwa ajili ya Mei Mosi?

Truth Bot AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 16, 2021
Posts
307
Reaction score
731
Ni swali linaloniumiza Kichwa Hapa Arusha. Kila nikiangalia Naona kabisa hakutakuwa na majibu ya Wafanyakazi Nchini zaidi ya Porojo..

Nilidhani Rais atakuja na Kujibu Hoja za wafanyakazi kama Kikokotoo, Maslahi yao na hata Kuongezwa Mishahara..

Mbona amekimbia?

Mbona mwenzake wa Zanzibar alikuwa Na ziara ila akaisimamisha..?
 
Mkuu, Hivi huyo aliyekuja hatoshei kutoa majibu? Kwani Uwakilishi unamaanisha kitu gani?........ Inafikirisha sana.
Halafu kama ni kweli ulidhania Rais atakuja.............lakini sasa imetokea hakuja yy in person hakuna sababu ya kuendelea na kudhania amekimbia.......n.k. nk. Nashauri ungefuatilia zaidi kama hoja, dukuduku na kero za wafanyakazi zimepata majibu stahiki au la.
Mkuu tusiwalinganishe watu au Marais.Yule wa Z'bar kafanya kwa maamuzi yake ukizingatia kwamba Kila mmoja anatenda kadri ya Utaratibu wake. (Ni kama kudai eti huyu mbona anakula Ugali mwenzake anakula wali.... )
Labda nikuulize (samahani lakini); mbona Mh. Magu hakupenda sana kutoka nje ya nchi lakini wadau Tulihoji, huyu wa sasa anatoka nje ya nchi lakini wadau bado Tunahoji - Tutahoji mpaka lini?
 
Mpaka pale kutakapokuwa na Balance..

Na Ruto Na Rais wa Uganda mbona hawajatuma mwakilishi wameenda na wanahutubia Mataifa yao??
 
Kilaza yule kwanza muoga sana.Yaani kipindi kile Magufuli akiwa Rais ,Magufuli akichachamaa Samia anatoa machozi hadi alitaka kujiuzulu.Bora angejiuzulugu tu.
 
Mpaka pale kutakapokuwa na Balance..

Na Ruto Na Rais wa Uganda mbona hawajatuma mwakilishi wameenda na wanahutubia Mataifa yao??
Dah! Wadau bhana; kwani ni kwa mujibu wa sheria(Katiba) au ni Utaratibu tuu?
Halafu hili swala ni kama linachukua mrengo wa kisiasa zaidi.
Sasa Tusemeje kuhusu yale mataifa ambayo hawajafanya lolote yan imekuwa ni siku kama siku nyingine za Jumatano ila kuna mapumziko?
 
Kilaza yule kwanza muoga sana.Yaani kipindi kile Magufuli akiwa Rais ,Magufuli akichachamaa Samia anatoa machozi hadi alitaka kujiuzulu.Bora angejiuzulugu tu.
Lakini si mlimtea wenyewe kwenye zile kamati zenu za chama?
 
HUyu ambae hajui kujielezašŸ¤”
 
Kwani wafanyakazi ni suala la muungano?
Hapana sio swala la Muungani
Kama taifa Lipi???
Tusizungumzie Mataifa yaliyoendelea Tuzungumzie mataifa yanayoendelea
 
Hapana sio swala la Muungani

Kama taifa Lipi???
Tusizungumzie Mataifa yaliyoendelea Tuzungumzie mataifa yanayoendelea
Umeyapitia mataifa yote yanayoendeleA na kujiridhisha kwamba maraisi wao leo Mei mosi 2024 wapo Uwanjani wanahutubia?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…