Kwanini Rais Samia na chawa wake hawajifunzi toka kwa Hayati Magufuli?

Kwanini Rais Samia na chawa wake hawajifunzi toka kwa Hayati Magufuli?

Father of All

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2012
Posts
7,672
Reaction score
9,039
1696943156890.png
Kama kuna mtu tutamkumbuka kwa kuanzisha sera za kuabudia na kumsifia rais si mwingine bali Mwendazake.

Alitegeneza kile ambacho kiingereza huitwa cult sina kiswahili chake.

Alisifiwa hadi kuitwa Mungu tena na profesa aliyejisifu usomi sana japo alikuwa kihiyo wa kawaida. Samia naye hakubaki nyuma.

Alikuwapo kama hakuwapo. Alisifia kiasi cha kupewa fursa ya kugombea na mwendazake tena. Sasa amechukua madaraka, anarudia mchezo ule ule.

Je Rais Samia hajajifunza kuwa binadamu si lolote bali mavumbi na anaweza kutoweka wakati wowote na mipango yake ikatibuka?

Pili, Rais Samia hajui hawa wanomsifia hawamsifii yeye kama ambavyo alimfanyia mwenzake bali kitumbua? Je anayajua ya kesho?

Chawa wanaanza kutangaza atagombea, je nani kampitisha? Je inakuwaje chawa waanze kampeni mapema?

Je unamshauri nini Samia Suluhu Hassan kuhusiana na changa la macho analopigwa na chawa?
 

Attachments

  • 1696943538102.png
    1696943538102.png
    218.3 KB · Views: 3
View attachment 2777783
Kama kuna mtu tutamkumbuka kwa kuanzisha sera za kuabudia na kumsifia rais si mwingine bali Mwendazake. Alitegeneza kile ambacho kiingereza huitwa cult sina kiswahili chake. Alisifiwa hadi kuitwa Mungu tena na profesa aliyejisifu usomi sana japo alikuwa kihiyo wa kawaida. Samia naye hakubaki nyuma. Alikuwapo kama hakuwapo. Alisifia kiasi cha kupewa fursa ya kugombea na mwendazake tena. Sasa amechukua madaraka, anarudia mchezo ule ule. Je Samia hajajifunza kuwa binadamu si lolote bali mavumbi na anaweza kutoweka wakati wowote na mipango yake ikatibuka? Pili, Samia hajui hawa wanomsifia hawamsifii yeye kama ambavyo alimfanyia mwenzake bali kitumbua? Je anayajua ya kesho? Chawa wanaanza kutangaza atagombea, je nani kampitisha? Je inakuwaje chawa waanze kampeni mapema?
Je unamshauri nini Samia Suluhu Hassan kuhusiana na changa la macho analopigwa na chawa?
U chawa siku hizi ni Tunu ya Taifa kwenye Ilani ya CCM
 
Hizo ni fedha za walipa kodi wananchi, Hao chawa wabadili kauli waseme serikali imetekeleza miradi ya maendeleo kwa fedha za wananchi na siyo mama katoa hela kwani ni zake?
 
Jiulize kwa nini mwendazake alisifiwa na wasomi na watu wanaojielewa wakati huyu wa sasa anasifiwa na kina steve nyerere, babalevo, maulid kitenge na mwijaku.

Sent from my SM-A225F using JamiiForums mobile app
 
Jiulize kwa nini mwendazake alisifiwa na wasomi na watu wanaojielewa wakati huyu wa sasa anasifiwa na kina steve nyerere, babalevo, maulid kitenge na mwijaku.

Sent from my SM-A225F using JamiiForums mobile app
Kwangu wote ni sawa. Wasomi waliomsifia mwendazake walifanya hivyo kwa sababu zile zile njaa na kutojiamini na kutegemea hisani
 
Back
Top Bottom