Kwanini sala nyingi ujikita kuombea waliopo madarakani na kuacha vyama pinzani?

Kwanini sala nyingi ujikita kuombea waliopo madarakani na kuacha vyama pinzani?

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2018
Posts
539
Reaction score
3,507
Ukifuatilia sala na maombezi mengi yanayofanywa hasa na viongozi wa dini ya kikikristo ambayo Mimi Ni muumini utaja majina ya viongozi wa kitaifa, kimkoa, kiwilaya na hata mataifa mengine. Katika sala hizo utajwa kwa majina, Rais na Marais wastaafu, Makamu, Waziri mkuu, Jaji Mkuu, Spika ,vyombo vya dola na viongozi wengine. Msingi wa maombi huwa kuwaombea afya njema, kuwaombea watumiwe na roho mtakatifu, waendeshe maeneo yao ya utawala kwa haki nk

Lakini katika sala na maombi hayo uwezi kusikia maombaji wakiwaombea wanaodhulumiwa, uwezi kusikia wakitajwa viongozi wa upinzani, uwezi kusikia wakiombea makundi ambayo yanapingana kwa hoja na utawala. Hii dhana naamini inawanyima amani baadhi ya watu hasa wale ambao makundi yao hayatajwi popote na viongozi wao wa dini.

Swali langu; kwanini viongozi wa dini wameshindwa kufanya maombi ambayo siyo biased? Je ndivyo imani inavyotaka? Kwamba tuwaombee wenye madaraka tu na siyo makundi yote Tena kwakuwataja majina Kama tunavyofanya kwa viongozi wengine? Kwanini tunasali kwa ubaguzi?

Naomba kufungua mjadala huu kuwaweka sawa wahubiri, Wana mombi na watu wengine wanaoliombea Taifa kutokufanya ubaguzi maana amani ya nchi haitikani na viongozi inatokana na wananchi.....yamkini walikuwa hawajui sala zinaweza kuleta ubaguzi Sasa nawaomba wainuke waombe Mwongozo wa kiroho.

Wanashindwa kukemea maovu na dhulma Basi waombee dhulma na uovu viondoke kwenye jamii ili pawe salama kwao kutangaza neno. Wapo watu wanakwama kwenda kwenye nyumba za ibada maana wanaoongooza nyumba hizo awataki kusimama na Haki wanasimama na mahitaji ya wanadamu waliopewa utawwala.
 
Wivu tu, Waombee na wewe wanaosahaulika bhana!
 
Kuna umuhimu pia wa kuombea viongozi wa upinzani,
Ili wwaweze kupata courage ya kuendelea kuchallenge walioko madarakani
 
Huenda kuna mihimili isiyo tajwa haija jichimbia lakini ipo. Taasisi za kidini zaweza kuwa miongoni?
 
Ukifuatilia sala na maombezi mengi yanayofanywa hasa na viongozi wa dini ya kikikristo ambayo Mimi Ni muumini utaja majina ya viongozi wa kitaifa, kimkoa, kiwilaya na hata mataifa mengine. Katika sala hizo utajwa kwa majina, Rais na Marais wastaafu, Makamu, Waziri mkuu, Jaji Mkuu, Spika ,vyombo vya dola na viongozi wengine. Msingi wa maombi huwa kuwaombea afya njema, kuwaombea watumiwe na roho mtakatifu, waendeshe maeneo yao ya utawala kwa haki nk

Lakini katika sala na maombi hayo uwezi kusikia maombaji wakiwaombea wanaodhulumiwa, uwezi kusikia wakitajwa viongozi wa upinzani, uwezi kusikia wakiombea makundi ambayo yanapingana kwa hoja na utawala. Hii dhana naamini inawanyima amani baadhi ya watu hasa wale ambao makundi yao hayatajwi popote na viongozi wao wa dini.

Swali langu; kwanini viongozi wa dini wameshindwa kufanya maombi ambayo siyo biased? Je ndivyo imani inavyotaka? Kwamba tuwaombee wenye madaraka tu na siyo makundi yote Tena kwakuwataja majina Kama tunavyofanya kwa viongozi wengine? Kwanini tunasali kwa ubaguzi?

Naomba kufungua mjadala huu kuwaweka sawa wahubiri, Wana mombi na watu wengine wanaoliombea Taifa kutokufanya ubaguzi maana amani ya nchi haitikani na viongozi inatokana na wananchi.....yamkini walikuwa hawajui sala zinaweza kuleta ubaguzi Sasa nawaomba wainuke waombe Mwongozo wa kiroho.

Wanashindwa kukemea maovu na dhulma Basi waombee dhulma na uovu viondoke kwenye jamii ili pawe salama kwao kutangaza neno. Wapo watu wanakwama kwenda kwenye nyumba za ibada maana wanaoongooza nyumba hizo awataki kusimama na Haki wanasimama na mahitaji ya wanadamu waliopewa utawwala.

1 TIMOTHEO 2​

Mafundisho kuhusu sala
1Kwanza kabisa, nawasihi muombe dua, msali na kumshukuru Mungu kwa ajili ya watu wote, 2kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema. 3Jambo hili ni jema na lampendeza Mungu Mwokozi wetu, 4ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli.
 
Kuna umuhimu pia wa kuombea viongozi wa upinzani,
Ili wwaweze kupata courage ya kuendelea kuchallenge walioko madarakani
Mkuu samahani- viongozi wa upinzani wana mamlaka gani mpaka waombewe. Hata hivyo wanaombea kama watu wengine kwa mktadha na dhamira tofauti.
 
Kanisa katoliki Kuna sala ya kuombea watumishi wa umma
Ila hakuna sala ya kuombea wasio na ajira
 
Back
Top Bottom