Kwanini Sayansi na Teknolojia isitumike kufahamu mwezi utaandama siku gani?

Kwanini Sayansi na Teknolojia isitumike kufahamu mwezi utaandama siku gani?

mafutamingi

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2011
Posts
2,773
Reaction score
2,183
Jumuia ya Waislamu duniani kote imekuwa katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Hapa Tanzania na Afrika Mashariki nzima sikukuu ya Idi inatarajiwa kuwa Alhamisi au Ijumaa, kutegemea na kunadama kwa mwezi.

Swali langu ni kwamba kwa nini sayansi na teknolojia isitumike kufahamu mwezi utaonekana siku gani? Teknolojia hii imekuwapo siku nyingi na ni rahisi kabisa kufahamu mwezi utaonekana siku gani na saa ngapi na dakika ipi.

Hata ukitaka kufahamu mwezi wa Julai 2027 mwezi utaonekana lini, saa ngapi na dakika ipi, utaambiwa. Binafsi naona inaleta mantiki
kutumia sayansi kufahamu na kutangaza mfungo utaisha lini ili kuwawezesha watu kufanya mipango ya sikuu hiyo kuliko kubahatisha ama ilivyo sasa.
 
Tehama
Screenshot_2021-05-05-12-10-46.jpeg
 
Jumuia ya Waislamu duniani kote imekuwa katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani. Hapa Tanzania na Afrika Mashariki nzima
sikukuu ya Idi inatarajiwa kuwa Alhamisi au Ijumaa, kutegemea na kunadama kwa mwezi. Swali langu ni kwamba kwa nini sayansi na teknolojia
isitumike kufahamu mwezi utaonekana siku gani? Teknolojia hii imekuwapo siku nyingi na ni rahisi kabisa kufahamu mwezi utaonekana siku gani
na saa ngapi na dakika ipi. Hata ukitaka kufahamu mwezi wa Julai 2027 mwezi utaonekana lini, saa ngapi na dakika ipi, utaambiwa. Binafsi naona inaleta mantiki
kutumia sayansi kufahamu na kutangaza mfungo utaisha lini ili kuwawezesha watu kufanya mipango ya sikuu hiyo kuliko kubahatisha ama ilivyo sasa.
Maisha ni maamuzi,

we funga kwa kujibu wa tarehe za Waaarabu, uko sawa. funga kwa mujibu wa www.moonsighting.com, uko sawa. Funga kwa mujibu wa BAKWATA, uko sawa.

Ambao taarifa zao za Ramadhani na Eid huwa hivi, RAMADAN and EID-AL-FITR.

Huo ni kwa mujibu wa muandamo na muonekano wa mwezi kisayansi, ambapo huwa kamainavyoonekana kwenye link hii Crescent Moon Visibility Maps 1438-1465 AH.

Ni maamuzi yako.
 
Unauliza au unashauri yakhe?
Ukweli ni kuwa elimu juu ya mwezi ipo na ilikuwepo ELIMU YA MIIKATI, lakini ukweli kutokana na masheikh kutoweza hesabu vizur elimu hiyo inapotea na kubakia watu wanaojadili kitu bila elimu.

Elimu juu ya MANAZILI LI KAMARI/mashukio/vituo vya mwezi ni hesabu zilizoshiba ambazo hufanya masheikh kutoweza mahesabu kutokana na kutokuwa na ujuzi wa hesabu.

UKWELI NI KWAMBA HAKUNA MIANDAMO MIWILI YA MWEZI BALI TUNATOFAUTIANA MATULUGH TU.

Zingatia mwezi uko na vituo 28 tu sawa na idadi ya herufi za kiarabu.
 
Unauliza au unashauri yakhe?
Ukweli ni kuwa elimu juu ya mwezi ipo na ilikuwepo ELIMU YA MIIKATI, lakini ukweli kutokana na masheikh kutoweza hesabu vizur elimu hiyo inapotea na kubakia watu wanaojadili kitu bila elimu.

Elimu juu ya MANAZILI LI KAMARI/mashukio/vituo vya mwezi ni hesabu zilizoshiba ambazo hufanya masheikh kutoweza mahesabu kutokana na kutokuwa na ujuzi wa hesabu.

UKWELI NI KWAMBA HAKUNA MIANDAMO MIWILI YA MWEZI BALI TUNATOFAUTIANA MATULUGH TU.

Zingatia mwezi uko na vituo 28 tu sawa na idadi ya herufi za kiarabu.
Kwa hiyo mkuu maana yake mwezi ukiandama sehemu moja means watu wa sehemu nyingine wafanyie kazi mwezi huo ?
 
Kabisa.

Shida mtu kuona wenzie hawsko sawa
Hata sasa hivi mwezi ukionekana sehemu moja, kwa mfano Mombasa, Mtwara au Tanga, Dar es Salaam watatangaza kwamba mwezi umeonekana hata kama haujaonekana Dar Es Salaam. Vivyo hivyo endapo teknologia inatumika, watu waliopo Tabora, Mbeya, Musoma na Zanzibar wote wakitumia teknologia watapata jibu hilo hilo. Kazi kwenu BAKWATA, endeni na wakati!
 
Jumuia ya Waislamu duniani kote imekuwa katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani. Hapa Tanzania na Afrika Mashariki nzima
sikukuu ya Idi inatarajiwa kuwa Alhamisi au Ijumaa, kutegemea na kunadama kwa mwezi. Swali langu ni kwamba kwa nini sayansi na teknolojia
isitumike kufahamu mwezi utaonekana siku gani? Teknolojia hii imekuwapo siku nyingi na ni rahisi kabisa kufahamu mwezi utaonekana siku gani
na saa ngapi na dakika ipi. Hata ukitaka kufahamu mwezi wa Julai 2027 mwezi utaonekana lini, saa ngapi na dakika ipi, utaambiwa. Binafsi naona inaleta mantiki
kutumia sayansi kufahamu na kutangaza mfungo utaisha lini ili kuwawezesha watu kufanya mipango ya sikuu hiyo kuliko kubahatisha ama ilivyo sasa.
Hapa teknoloji inaweza kutumika kuuona mwezi iwapo tu mwezi huo utakuwa umejificha kwenye mawingu. Vinginevyo swala la kuonekana kwa mwezi huwa halitokei kwa wakati huo huo kila mahali duniani kwa sababu dunia siyo tambarare.

Kwa mfano, ipo sehemu moja duniani kwa wakati huu ambayo jua linazama na kupelekea mwezi uonekane, na wakati huo huo kuna sehemu nyingine tena ambayo yenyewe ndiyo ni usiku wa manane. Now how are you technologically, going to harmionise this? Huwezi ukafanya synchronization ya kuonekana kwa mwezi duniani kwa sababu huwa unaonekana kwa kufuata majira ya mahali mtu alipo
 
Hapa teknoloji inaweza kutumika kuuona mwezi iwapo tu mwezi huo utakuwa umejificha kwenye mawingu. Vinginevyo swala la kuonekana kwa mwezi huwa halitokei kwa wakati huo huo kila mahali duniani kwa sababu dunia siyo tambarare.

Kwa mfano, ipo sehemu moja duniani kwa wakati huu ambayo jua linazama na kupelekea mwezi uonekane, na wakati huo huo kuna sehemu nyingine tena ambayo yenyewe ndiyo ni usiku wa manane. Now how are you technologically, going to harmionise this? Huwezi ukafanya synchronization ya kuonekana kwa mwezi duniani kwa sababu huwa unaonekana kwa kufuata majira ya mahali mtu alipo
Unaposema mahali mtu alipo unakusudia nn.

Mahali ni Nchi ?

Au mkoa ?

Au bara ?
 
Je kuna tofauti gani Kati ya Mwezi unaoonekana wakati huu wa Rmadhani na Mwezi kuonekana miezi mingine? Kisayansi huu Mwezi tunaambiwa unaandama maana yake Nini ?
 
Urithi tu wa miungu ya kiarabu, hata kijijini kwetu kila badiriko linamaana yake........
 
Mliambiwa sky is the limit mkakubali,ila likija suala la imani za watu kila mtu fundi
 
Je kuna tofauti gani Kati ya Mwezi unaoonekana wakati huu wa Rmadhani na Mwezi kuonekana miezi mingine? Kisayansi huu Mwezi tunaambiwa unaandama maana yake Nini ?
Kuandama (kuonekana mwezi) tena ule mweI mdogo wenye mithili ya kucha.

Ili iwe kuandama maana yake iwe ni siku ya 29 ya mwezi uliopo hivyo ukiuona mwezi mduchuu ule hapo ndo kuandama
 
Ila izi ni siasa tu Mwezi umeandama nchi zote za UAE na Misri,ghana,n.k ila bado anasimama mufti anapinga eid ijumaa aise[emoji34]
 
Je kuna tofauti gani Kati ya Mwezi unaoonekana wakati huu wa Rmadhani na Mwezi kuonekana miezi mingine? Kisayansi huu Mwezi tunaambiwa unaandama maana yake Nini ?
Mwezi huwa upo tu kila siku na unaizunguka Dunia na husanabisha Maji ya Bahari kupwa na kujaa

Mzunguko wake hutumiwa kwenye Kalenda za Jamii mbalimbali kama kwenye Kalenda ya Kiarabu Ramazani ikiisha unaingia Mwezi wa Shawali
 
Back
Top Bottom