DOKEZO Kwanini Serikali kupitia Wizara ya Nje, wasishirikiane na Wizara ya Nje ya Congo, kumkamata Tapeli alojiita Nabii kiboko ya wachawi?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Hiyo ni kazi ya Interpol kabisa.Huyu mtu ni muhalifu halafu hana akili wala kifua.Kama kuna wakubwa alikua anakula nao wakae chonjo.Akishikiwa pliers au moto uelekezwa kwenye korodani atatamka yoootee!
Akili anayo ndio maana akaweza kuwanyoosha nyie wapumbavu
 
Na wale ma board guard wake kina mwarabu faighter warudishwe Tz wafunguliwe kesi
 
It takes a special kind of a corn artist to get rich without paying taxes by selling people an invisible product for 10%(zaka) of their income that they can't see until they die(Mbinguni)..
 
mawazo safi sana haya, tukianza kuwakata wanaoenda makanisani na misikitini, moto wake utakuwa ni hatari sana...
Ila si watu weusi tuna matatizo sana 🀣 yani kweli unaenda kwa mtu unaeamini anatoa huduma za kiroho, ila anakuambia kiingilio laki tano..... Daaaah na mtu anatoa, ila kiingilio cha kumuona daktari elf 20 raia hawana. Kiboko ya wachawi amevuna na amevuna sanaa mwenyewe anasema mtajua hamjui

Your browser is not able to display this video.
 
akamatwe kwa kosa gani mkuu?
hakua analazimisha watu wazima na akili zao kwendea huduma yake.
 
Tz kuna Majasusi au Matahira.
Utasikia tunasubiri taarifa za kiintelijensia .
 
Haya ndio maajabu ya Musa... laki tano anapewa mtu kiulaini (kisa tu Nabii wa Mungu), elfu ishirini za matibabu yake hanazo (tena ni songo mbingi haswa na lawama kibao)... inabidi sasa serikali ijifunze toka kwa hawa manabii mbinu wanazo tumia kuwaingiza waumini wao Kingi...
 
Msotumie hisia kuhukumu watu na kuwaita majina mabaya, kisheria utamshitaki kwa kosa gani embu tuambie?
watu wenyewe wameombq kuombewa yeye kawatoza pesa hapo kuna jinai kweli? Yani serikali iache kushughulikia mambo ya msingi ya nchi ihangaike kutumia nguvu na gharama kuhangaika na mtu mmoja ambaye hana makosa kisheria
Ukimshitaki yule mcongo itabidi uyafunge makanisa karibia yote maana wote wanafanya hicho hicho sema huyu mcongo ada yake kubwa hiyo ndio tofauti
 
akamatwe kwa kosa gani mkuu?
hakua analazimisha watu wazima na akili zao kwendea huduma yake.
Makosa ni mengi sana yakiwemo:
money laundering
Mis representation
udanganyifu wa kuombea watu...etc

DPP Atoke huko mafichoni afanye kazi yake... DPP Wetu bado amelala.. labda ataamka na kufanya kazi inayompa ulaji wake wa kila siku baada ya kuona hizi video za huyu Juha wa Kongo...
 
Tunachekesha
 
Hakuna kosa hata moja linaloweza kumtia hatiani hapo ni kupoteza rasilimali za nchi kufuatilia mambo ya kijinga
Hakuna kosa kwenye jinai linaloitwa misrepresentation
Na hapo hakuna money launderung
Na hakuna kosa kwenye penal code la idanganyifu wa kuoombea watu, maana maombezi ni imani ,wote tunaomba kwa kuamini yule kisheria hana makosa, ni kama walivyo kina mwamposa na wengine ,sema labda kinachowauma kuwa anatoza hela nyingi, ila hakumlazimisha mtu ,wote wameenda kuombewa kwa hiari yao
 
Yaani serikali itumie gharama na muda kukimbizana na mwendawazimu???
Mwendawazimu? ,😳
Mwendawazimu anaweza kutapeli mandondocha ya Kitanzania mabilioni ya hela na kukimbilia kwao kujenga na kujitapa? No Dearie ni mhalifu.
 
Mwendawazimu? ,😳
Mwendawazimu anaweza kutapeli mandondocha ya Kitanzania mabilioni ya hela na kukimbilia kwao kujenga na kujitapa? No Dearie ni mhalifu.
Aliwapora??? Si walipeleka wenyewe sadaka kanisani??
Mbona matapeli wa dini wako wengi tu wanawaibia ndugu zetu na wako huru hapa tanzania???
Tuache uzwazwa wa imani tuache kutapeliwa
 
Watanzania wao watapeliwe forex,Mr kuku,kiboko ya wachawi em ifike mahala tujionee huruma khaaπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…