DOKEZO Kwanini Serikali kupitia Wizara ya Nje, wasishirikiane na Wizara ya Nje ya Congo, kumkamata Tapeli alojiita Nabii kiboko ya wachawi?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kwa kosa gani?
Uchonganishi anaweza kuleta ushahidi mtu anayemwambia kalogwa na mama yake mdogo? Huo uchonganishi na mafundisho hayafundishi hivyo mtu anaweza kwenda kumuua mama yake mdogo kwa kuwa kiboko ya wachawi kamwambia amemloga hii ramli chonganishi mbona waganga wanakamatwa yy ni nani achonganishe watu aachwe?
 
Katapeli nini?

Wajinga ndiyo waliwao.
 
Hiyo ni kazi ya Interpol kabisa.Huyu mtu ni muhalifu halafu hana akili wala kifua.Kama kuna wakubwa alikua anakula nao wakae chonjo.Akishikiwa pliers au moto uelekezwa kwenye korodani atatamka yoootee!
Umepigwa na nondo ya kiboko ya wachawi nini?

Kiendacho kwa mganga hakirudi.
 
Hii nchi albadil ambazo zimewahi kutangazwa mtandaoni zitasomwa ninazozjiua ni mbili.

Ilikua ya Afande Sele na nyingine ilikua ni kwaajili ya mauaji yaliwahi tokea hapa nchini.
Na hizi albadil zote mbili hazikuleta matokeo waliyosema albadil huleta.

Juzi imetangazwa itasomwa albadil kwaajili ya mauaji tena. Uliona watu walivyokua wanacomment humu? Bado wanaamini albadil ndiyo dawa.

Unadhani wananchi hao watasita kumpa pesa akitokea mtu mwingine akasema ni kiboko ya wachawi? Unahisi shida ni nini?
 
Unataka watu wajipatie dhambi kwa kuua mtu? Watu wameenda kupeleka fedha wenyewe so wacha tujifunze kupitia hili. Binafsi naamini Biblia kwamba watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa, lakini Biblia inasema siku za mwisho kutatokea manabii ya wengi wauongo so hili linadhihirisha kile kilichosemwa kwenye biblia kila mtu atafakari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…