Kwanini siku hizi watoto wanapozaliwa hawalii kama ilivokuwa zamani?

Puyugu 01

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2018
Posts
573
Reaction score
455
Juzi nilifika Hospitali moja ya rufaa itwayo Ligula mkoani Mtwara kwa lengo la kumjulia hali mke wa ndugu yangu ambae alifanyiwa Operation week 1 baada ya kujifungua.

Nikiwa pale Hospitalini nilibahatika kubadilisha mawazo na watu tofauti wengi wao wakiwa wamama ambao walikuja kwa lengo la kuwasaidia ndugu zao ambao walishafikia kilele cha kushusha injini, lakini uwepo wangu pale nilisikia minong'ono toka kwa wamama wakisema kuwa 95% ya watoto wanaozaliwa hawalii mara watokeapo nje hali ambayo ni tofauti na zamani.

Jee ni kwa nini hali hii hutokea siku hizi?
 
Ukiona halii ujue kafa it is either alie mwenyewe au wamlize ili kuzibua mapafu sawasawa?
 
Anayejua kama mtoto kalia au hajalia ni mkunga,hata mama mzazi anaweza asijue ila mi ninavyojua mtoto lazima alie hata kwa makofi na vifinyo.
 
Mtoto asipolia anasaidiwa kulia ni lazima alie kwa namna yeyote niliwahi sikia kuwa asipokuwa sharp kulia akili inaweza hitaji tuition muda wote( hizi ni tetesi tu)[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Hao akina mama waliokua wananong'ona na wewe ukiwepo wana watoto? Kwa kuwatazama tu? Mtoto asipolia ni tatizo.
Unaposema asilimia kadhaa inamaana umefanya utafiti na kujiridhisha na hizo taarifa, hizo itakua ni kesi chache lakini kwa mazingira ya kawaida, mtoto anatakiwa alie anapozaliwa.

Mie nilishuhudia kidume changu kikilia japo baadae nilijutia maamuzi yakuingia kwenye kile chumba, lakini imeniongezea heshima kwa wanawake na wazazi kwa ujumla.
 
Anayejua kama mtoto kalia au hajalia ni mkunga,hata mama mzazi anaweza asijue ila mi ninavyojua mtoto lazima alie hata kwa makofi na vifinyo.
kina mama wanajua kama kalia au la ukizingatia siku hizi hata katika operation huwa wanawachoma sindano za mgongoni hivyo wanashuhudia kila kitu.....
 
kina mama wanajua kama kalia au la ukizingatia siku hizi hata katika operation huwa wanawachoma sindano za mgongoni hivyo wanashuhudia kila kitu.....
Basi siku hizi hawazai kwa uchungu, Kama wanazaa kwa uchungu basi uchungu kumbe ni wakawaida tu. Maana Kama wanavyoongeaga kujifungua ni nusu kuta, sidhani kama wataweza ku-notes Kama mtoto kalia au la! Naongea kwa hisia zangu, sikubishi maneno yako.
 
Kulia kwa mtoto ni moja ya furaha ya kuja duniani,hali ilivyo katika awamu hii mtoto anapozaliwa anakuwa hana furaha ajionea bora anyamaze tu,
😱😱😱😱 kashausoma usawa tangu tumboni
 
😱😱😱😱 kashausoma usawa tangu tumboni
Watoto wanakuwa wanawasikia wazazi wao wakiwa tumboni,wazazi wa siku hizi hapa Tanzania maongezi yao ni:-,kupigwa risasi wanasiasa,kuvunyiwa nyumba kwa raia,watu wanaokotwa kwenye viroba,maandamano ya Mange Kimambi...
Watoto wanakuwa hawana furaha wanapozaliwa wanaamua wajimazie tu...,kujimazia ndio maandamano yaoπŸ˜€πŸ˜€
 
Njia za uzazi zimekuwa pana kwahyo watoto hawabanwi banwi wanapo zaliwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…