Kwanini sisi tusiwaombe hawa jamaa zetu waturuhusu kununua ya mafuta ya bei nafuu?

Kwanini sisi tusiwaombe hawa jamaa zetu waturuhusu kununua ya mafuta ya bei nafuu?

Mimi nina mashaka huko wanakonunua sasa kuna cha juu wanapata, maana sio kwa ujinga huu wa kuumiza watu kiasi hiki.

Kule UN wakisema tupige kura kulaani uvamizi wa Urusi tunakula kona, alafu kwenye kununua mafuta ndio tujifanye tuko bega kwa bega na mabeberu?

Moja ya mambo yanayonikera sana awamu hii ni uhuni uliopo kwenye sekta ya nishati.
 
Japan wamekea Russia vikwazo kwa mambo mengine, lakini mafuta hayamo kwenye orodha ya vikwazo. Sisi hatujaiwekea Russia vikwazo kabisa, kwa nini tuombe ruhusa kununua mafuta ya Russia?
Kama wao wenyewe wenye vikwazo wananunua, kwa nini sisi tusinunue kwa uhuru?
 
Tumekopa mpk hela ya kulipa mishahara ya wafanyakazi toka nchi za magharibi kwahiyo siyo rahisi tukapinga jambo ama msimamo wao.
Hatupingi jambo au msimamo wao wowote bali tunataka tu tuwaombe na sisi waturuhusu kuyanunua hayo mafuta ya bei nafuu kama walivyo iruhusu Japan.
Japan wamekea Russia vikwazo kwa mambo mengine, lakini mafuta hayamo kwenye orodha ya vikwazo. Sisi hatujaiwekea Russia vikwazo kabisa, kwa nini tuombe ruhusa kununua mafuta ya Russia?
Kama wao wenyewe wenye vikwazo wananunua, kwa nini sisi tusinunue kwa uhuru?
Nadhani ni kwa sababu ya kuogopa kuharibu mahusiano yetu ya kidiplomasia na jamaa zetu ambao wanaweza pia kutuwekea vikwazo (sanctions) kama ambavyo wameanza kuiwekea sanctions nchi ya Uganda kwa kupitisha sheria kali sana dhidi ya mashoga na wana LGBTQQIP2.

Pia inaweza kabisa kuwa kuna watu wananufaika kwa kutonunua mafuta hayo ya Russia, mafisadi. Ni jambo la busara kuwaomba jamaa zetu wa USA na EU wakaturuhusu na sisi kununua mafuta haya. Ni mambo ya kidiplomasia tu. Tunamwomba Waziri wetu wa mambo ya nje ambaye pia ni mama alivalie njuga suala hili. Hatutegemei hata kidogo kwamba watatukatalia.
Mimi nina mashaka huko wanakonunua sasa kuna cha juu wanapata, maana sio kwa ujinga huu wa kuumiza watu kiasi hiki.
Hiyo ni kweli kabisa. Serikali na bunge limwagize CAG na TAKUKURU kulifanyia special audit jambo hili linaloangamiza uchumi wa nchi yetu. Hawa jamaa watashiba lini na kuacha upigaji huu? Imefikia hadi wanabadili tarakimu za invoice za wanaotudai hususani ile invoice ya ndege ya mizigo aliyoigundua raisi wetu.

Tanzania bila ufisadi inawezekana sana kama kila mtu atacheza kadi zake vizuri. Ni wajibu wa kila mtanzania kutokomeza ufisadi.
 
Kwanza Ujue Nchi Ombaomba Huwa Masuala Mazito Ya Migogoro Hasa Ya Mataifa Yenye Nguvu Duniani Hubaki Njia Panda Yakitazama Tu Yasijue Yafanye Nini
Lazima Huwezi Kununua Mafuta Ya Nchi Iliyowekewa Vikwazo Wakati
Sisi Hatujiwezi, Maana Yake Endapo Utanunua Vikwazo Vikiwekwa Ndani Saa 24
TTutakuwa Hoi Maeneo Yote Na Uchumi Utazorota
 
Japan waliruhusiwa na G7 kununua haya mafuta yaliyowekewa international sanction ya bei nafuu. Kwa nini na sisi tusiwaombe hawa rafiki zetu waturuhusu na sisi kuyanunua haya mafuta ili kunusuru uchumi wetu?


Una uhakika ni wapi mafuta yetu yanapatikana?
 
Kwanza Ujue Nchi Ombaomba Huwa Masuala Mazito Ya Migogoro Hasa Ya Mataifa Yenye Nguvu Duniani Hubaki Njia Panda Yakitazama Tu Yasijue Yafanye Nini
Lazima Huwezi Kununua Mafuta Ya Nchi Iliyowekewa Vikwazo Wakati
Sisi Hatujiwezi, Maana Yake Endapo Utanunua Vikwazo Vikiwekwa Ndani Saa 24
TTutakuwa Hoi Maeneo Yote Na Uchumi Utazorota
Ni kweli kabisa Bw. Kennedy. Inabidi kuwa wanyenyekevu na kuyaomba kwa heshima na taadhima, mataifa haya makubwa duniani yaturuhusu kufanya hivyo. Kazi hii waziri wetu wa mambo ya nje anaimudu sana kwa niaba ya raisi wetu.
Una uhakika ni wapi mafuta yetu yanapatikana?
Yanapatikana kule ambako hayajawekewa sanctions. Kule ambako USA na EU wanakonunua. Ni kule nchi za Uarabuni isipokuwa Iran ambayo iko kwenye sanctions kwa mingi. Baada ya vita ya Ukraine kuanza na Urusi kuwekewa sanctions kwenye mafuta na gesi yao, hawa Waarabu walipandisha maradufu bei za mafuta yao na gesi na bado wanaendelea kuyapandisha hadi sasa.

Hawa Waarabu ni wajanja sana. Vita ya Ukraine ilitoa fursa ya kunufaika kiuchumi kwa nchi zao. Wahenga walisema, 'Kufa kufaana'. Hii imesababisha malalamiko makubwa kwa nchi za America na nchi za NATO za kuporomoka kiuchumi na maisha kuwa magumu sana nchini kwao. Ndiyo maana nchi kama Japan wameamua kujiondoa kwenye hizo sanctions za mafuta na gesi ya Russia. Nchi kubwa duniani za China na India wao tangia mwanzo hawakuzikubali wala kuzitambua hizo sanctions lukuki alizowekewa Urusi na nchi za America na washirika wake wa NATO. Hivyo nchi hizi hazijaathirika cho chote kiuchumi kutokana na vita hivi, bali zimenufaika sana kiuchumi. Nchi hizi zimewezesha uchumi wa Russia kuendelea kuwa imara zaidi na kuifanya sarafu ya USD kuendelea kuporomoka thamani duniani na benki kuu zake kufirisika! Bei ya mafuta ghafi ya Uarabuni kwa sasa ni dollars 130 kwa pipa wakati yale ya kutoka Urusi ni dollar 70 tu kwa pipa. Sisi tunalazimika kununua hayo ya dollars 130 kwa kuogopa kukosana na mataifa hayo ya USA na NATO ambayo yatatuwekea sanctions kali kama tutathubutu kununua mafuta ya Urusi.

Nadhani sasa Bw. TUJITEGEMEE tuko pamoja.
 
Nadhani sasa Bw. TUJITEGEMEE tuko pamoja.
Naam tupo Pamoja, Mkuu.

Sema sasa, yameshuka maswali kibao kichwani mwangu:

1. . Sasa najiuliza, sanction amewekewa Russia ama amewekewa Russia na Sisi(Tanzania)? Hivi kutoelewana kwa US na Russia juu ya suala la Ukraine inakuwaje sisi tuwekewe vikwazo (haturuhusiwi kununua mafuta ya bei nafuu huko Russia)?

2. Kwanza sera yetu ya mambo ya nchi za nje nadhani haijabadilila, kuwa sisi kama nchi ya Tanzania hatufungamani na upande wowote. Sasa inakuwaje sasa tunaamua kukubali kumuunga mkono (kufungamana) US kujizuia(sina hakika kama tumezuiwa) kutonunua mafuta ya bei nafuu kutoka Russia na Iran ikiwezekana? Kwa nini, yaani ?

3. China na India wananunua mafuta Russia ya bei nafuu, na hizo ni nchi huru, na sisi Tanzania ni nchi huru, Sasa iweje sisi tushindwe kwenda kununua mafuta ya bei nafuu huko Russia? Au inatakiwa itakangazwe rasmi kuwa Tanzania siyo nchi huru kiasi haiwezi kujiamulia mambo yake yenyewe? Yaani kwamba sasa inatakiwa kuanza 'movement' mpya ya kupigania uhuru upya wa kujiamulia mambo yanayotuhusu kiuchumi hasa kama anavyofanya J. Malema wa Afrika Kusini? Kwamba sasa ni muda muafaka kuanzisha 'EFF' nchini?

4. Russia ina ubalozi nchini na sisi tuna ubalozi Russia, ni kwa nini tunasusia kununua mafuta ya Russia ili tuweze kupata unafuu wa kupunguza gharama za maisha nchini, maana mafuta ni bidhaa muhimu kwenye maendeleo?

5. Kwa nini tusitumie India na China marafiki zetu wanunue mafuta ya Russia kwa niaba yetu watueletee ama tukachuke kwao, kama labda wanunuzi kutoka kwetu hawawezi kuongea kirussia wakati wa manunuzi?

Yaani maswali maswali maswali...sielewi kabisa kinachoendelea?

Dr Akili na wengineo kama mtapata wasaa pitia na maswali haya.

Natanguliza shukrani kwa majibu.
 
Issues zote za uagizaji mafuta, karibu mitaa hii
P

Asante sana kwa kulipigania suala hili muhimu kwenye huo mtaa wako. Kufuatia suala hili kuwa la muhimu sana kwa ustawi wa taifa letu, bado kuna umuhimu wa kulipigania suala hili kila mtaa, kila kona na kwa kila mbinu. Ni muhimu kuikumbusha serikali mara kwa mara, kuishauri mbinu mbali mbali inazoweza kufanya na hata kuipigia kelele pale tunaponusa harufu ya ufisadi. Kwa mfano hao waagizaji wa mafuta wa pamoja ni kitu gani kinawazuia kuagiza hayo mafuta kutoka Urusi ambako bei yake ni nusu ya yale ya Uarabuni wanakoagiza? Huyo Kamishena hakuulizwa swala hilo kwenye hiyo video clip.
 
Naam tupo Pamoja, Mkuu.

Sema sasa, yameshuka maswali kibao kichwani mwangu:

1. . Sasa najiuliza, sanction amewekewa Russia ama amewekewa Russia na Sisi(Tanzania)? Hivi kutoelewana kwa US na Russia juu ya suala la Ukraine inakuwaje sisi tuwekewe vikwazo (haturuhusiwi kununua mafuta ya bei nafuu huko Russia)?

2. Kwanza sera yetu ya mambo ya nchi za nje nadhani haijabadilila, kuwa sisi kama nchi ya Tanzania hatufungamani na upande wowote. Sasa inakuwaje sasa tunaamua kukubali kumuunga mkono (kufungamana) US kujizuia(sina hakika kama tumezuiwa) kutonunua mafuta ya bei nafuu kutoka Russia na Iran ikiwezekana? Kwa nini, yaani ?

3. China na India wananunua mafuta Russia ya bei nafuu, na hizo ni nchi huru, na sisi Tanzania ni nchi huru, Sasa iweje sisi tushindwe kwenda kununua mafuta ya bei nafuu huko Russia? Au inatakiwa itakangazwe rasmi kuwa Tanzania siyo nchi huru kiasi haiwezi kujiamulia mambo yake yenyewe? Yaani kwamba sasa inatakiwa kuanza 'movement' mpya ya kupigania uhuru upya wa kujiamulia mambo yanayotuhusu kiuchumi hasa kama anavyofanya J. Malema wa Afrika Kusini? Kwamba sasa ni muda muafaka kuanzisha 'EFF' nchini?

4. Russia ina ubalozi nchini na sisi tuna ubalozi Russia, ni kwa nini tunasusia kununua mafuta ya Russia ili tuweze kupata unafuu wa kupunguza gharama za maisha nchini, maana mafuta ni bidhaa muhimu kwenye maendeleo?

5. Kwa nini tusitumie India na China marafiki zetu wanunue mafuta ya Russia kwa niaba yetu watueletee ama tukachuke kwao, kama labda wanunuzi kutoka kwetu hawawi kuongea kirussia wakati wa manunuzi?

Yaani maswali maswali maswali...sielewi kabisa kinachoendelea?

Dr Akili na wengineo kama mtapata wasaa pitia na maswali haya.

Natanguliza shukrani kwa majibu.
Nadhani jibu la maswala yako yote ni ufisadi, ufisadi, ufisadi tu. Hii ndiyo sababu iliyotufanya na inayoendelea kutufanya tusinunue mafuta hayo ya bei nafuu toka Urusi. Hizo sababu zingine ni visingizio tu.

Ukweli ni kwamba tangia vikwazo hivyo viwekwe kwa Urusi kuhusiana na mafuta (gasoline) yao hadi Januari 2023, nchi za Afrika zinazo ongoza kuendelea kununua mafuta haya kutoka Urusi ni Egypt, Nigeria na Morocco. Zingine ni Senegal, Sudan, Ivory Coast na Togo.

Cha ajabu ni kwamba hata hizo nchi zenyewe za USA na NATO zilizoweka hizo sanctions ya mafuta ya Urusi, zimekuwa zikiendelea kuyanunua mafuta hayo kwa pesa ya Rubles kama shariti lililowekwa na Russia kwa nchi hizo zisizo rafiki wa Russia. Nchi rafiki zinaruhusiwa kuyanunua kwa currency yo yote.
The top importers of Russian gasoline, despite the sanctions as from March 2022 up to January 2023 in USD billions are as follows:
China $ 66.6 Billions, Germany 26.1, Turkey 25.9, India 24.1, Italy 14.8, Poland 12.18, France 9.5, Belgium 9.2, Hungary 8.68, Bulgaria 6.28, Japan 6.08, South Korea 6.08, Spain 5.88, Austria 5.78, Egypt 5.48, Greece 4.58, Czechia 4.28 and UAE 4.18

Kwa hiyo huo wasi wasi wetu hauna msingi wo wote na haukupaswa kuwepo. Na kama tulikuwa tunahisi wasi wasi huo, ilikuwa ni jambo rahisi tu ya kuongea nao kuondoa huo wasi wasi kwani na wao bado wananunua.
 
The top importers of Russian gasoline, despite the sanctions as from March 2022 up to January 2023 in USD billions are as follows:
China $ 66.6 Billions, Germany 26.1, Turkey 25.9, India 24.1, Italy 14.8, Poland 12.18, France 9.5, Belgium 9.2, Hungary 8.68, Bulgaria 6.28, Japan 6.08, South Korea 6.08, Spain 5.88, Austria 5.78, Egypt 5.48, Greece 4.58, Czechia 4.28 and UAE 4.18
Mkuu, Pascal Mayalla , ukipata wasaa naomba urudi Tena Wizara umtafute yule Mkurugenzi/kamishna wa "uagizaji mafuta" uliyezungumza kwa kirefu kwenye video uliyotuwekea.

Ukimpata, umueleze kuwa takwimu zinaonyesha bado Russia Anaendelea kuuza mafuta yake kama kawaida na Hata nchi zilizomuwekea vikwazo bado Zina nunua mafuta yake. Muonyeshe takwimu alizotuletea Dr Akili kudhibitisha hoja, hoja inayopingana na maelezo yake.

Baadaye tutamuomba Dr Akili atupe link ya chanzo cha takwimu zake hizi.

Kwa staili ya kupashana habari baina yetu wananchi kupitia JF kisha Baadaye kwa serikalini kupitia connection yetu hapa jukwaani ya Ndugu yetu wa Kwa maslahi ya Taifa' Bwana Pascal Mayalla tunaweza kulisaidia Taifa letu kusonga mbele endapo tu hakutakiwa na Hila ya aina yoyote kwa watendaji na wananchi pia.
 
Kwa nini na sisi tusiwaombe hawa rafiki zetu waturuhusu na sisi kuyanunua haya mafuta ili kunusuru uchumi wetu?
Mimi nadhani hakuna haja ya kuwaomba, bali ni kuwalazImisha, kama hawataki, tutafute wananunuaji wengine wa mafuta. Na hii ndiyo hasara ya kuwa na ununuzi wa " Bulk " Kwa namna moja ama nyingine, Bulk ni aina nyingine ya "cartel"!!!! Vinginevyo, labda Mimi sielewi haya mambo hivyo nahitaji kuelimishwa.
 
Mkuu, Pascal Mayalla , ukipata wasaa naomba urudi Tena Wizara umtafute yule Mkurugenzi/kamishna wa "uagizaji mafuta" uliyezungumza kwa kirefu kwenye video uliyotuwekea.

Ukimpata, umueleze kuwa takwimu zinaonyesha bado Russia Anaendelea kuuza mafuta yake kama kawaida na Hata nchi zilizomuwekea vikwazo bado Zina nunua mafuta yake. Muonyeshe takwimu alizotuletea Dr Akili kudhibitisha hoja, hoja inayopingana na maelezo yake.

Baadaye tutamuomba Dr Akili atupe link ya chanzo cha takwimu zake hizi.

Kwa staili ya kupashana habari baina yetu wananchi kupitia JF kisha Baadaye kwa serikalini kupitia connection yetu hapa jukwaani ya Ndugu yetu wa Kwa maslahi ya Taifa' Bwana Pascal Mayalla tunaweza kulisaidia Taifa letu kusonga mbele endapo tu hakutakiwa na Hila ya aina yoyote kwa watendaji na wananchi pia.
Naunga mkono hoja kwa asilimia 100% chini ya 100%.
JF tumsaidie Mama, tulisaidie taifa.
P
 
Hii hapa link ya hizo takwimu. Kumbe hadi mwisho wa February 2023, bei ya haya mafuta ilikuwa dollars 50 tu kwa pipa wakati kule tunakonunuaga ni dollars 130 kwa pipa.


cc: TUJITEGEMEE & Pascal Mayala
 
Back
Top Bottom