Kwanini sisi Waafrika ni Masikini?

Kwanini sisi Waafrika ni Masikini?

Unatukana ovyo utadhani umelelewa kwenye banda la nguruwe

Hahahaa ! ebwana huyo Jamaa ni pasua kichwa ,we huoni post zake zilivyo Kama za kishoga ,sasa we acha na mimi nimpasue,umenichekesha sanasana !ebwana home mshua anafuga nguruwe kwa hiyo umelenga mulemule.
 
Msubilie JK akimaliza mda wake mwite home alafu muulize kwa upole ''ET! PROFFESSIONAL IV KWANINI WAAFRIKA MASIKINI'' atakwambia ''IKULU NI YA WAZUNGU''
 
Siamini kama kuna mtu alizaliwa aje kuwa maskini.Ila waafrika wengi ni maskini kutona na sababu kadhaa.Ngoja nikuelezee chache kama ifuatavyo:

1.UVIVU

Hapa utakubaliana na mimi kuwa uvivu ni tatizo kubwa sana kwetu waafrika.Japo tunatofautiana kiwango cha uvivu,lakini kwa ujumla wengi ni wavivu.

Tunapenda sana mteremko na easy way.Hakuna anayependa kujituma.Utendaji kazi wetu ni mdogo lakini starehe na matumizi yako juu.

Kwa mtindo huu wa maisha sidhani kama tutaweza kupiga hatua.Na hata tukipiga hatua,basi itakuwa ni za kunyata.

2. MENTALITY

Blacks and African kwa ujumla we got negative perspective in most of the things.

Tunaendekeza sana imani potofu na kukatishana tamaa au kuwa katisha tamaa wengine.

Mtu yuko radhi aghairi kufanya jambo mara tu baada ya kudhani litakuwa gumu.Tunakata tamaa hata kabla hatujajaribu.

Kwa kiasi flan uoga wa kushindwa umetukwamisha sana.

3.SELFISHNESS

Dah,mkuu ili ni tatizo kubwa sana sehemu nyingi.Ila kwa bahati mbaya kwetu ni janga kubwa sana.

Ni vigumu kuwa na maendeleo ikiwa wanaokuzunguka wana hali mbaya kiuchumi,maana kila siku watakuwa wanakupiga mizinga na kukurudisha nyuma.

Ila endapo jamii inayokuzunguka ikiwa walau ipo vizuri kiuchumi basi hata maendeleo huweza kuja haraka.

Watu hupenda kujifkiria wao wenyewe bila kujali wengine,ndio maana hata maendeleo yanagoma.

Mfani viongozi watajifkiria wao kwanza alaf ndio waje kuendeleza nchi.Miaka minne ya uongozi wanachumia matumbo yao kwanza.Alaf mmoja uliobaki watautumia kuwa karibu na wananchi kwa ajili ya kujitengenezea mazingira ya kuchaguliwa tena kipindi kijacho.

4.UPENDO

Matajiri usaidiana walau wawe juu na waweze kupiga hatua,ila wengi wetu (hasa Africans) huwa tunafurahia wenzetu wanapoanguka.Kuna siku nilimsikia mama mmoja akicheka huku anamwambia mwenzake "Afadhali mwanae amefeli kama mwanangu,maana angefaulu ingekuwa kero hapa mtaani" Nilibaki najiuliza tu,tutafika kwa mtindo huu??

Upendo hakuna kati yetu.Aliyenacho hataki kumsaidia walau mawazo yule hasiyenacho.

Na hasiyenacho ameshakata tamaa na hana mpango wa kujishughulisha zaidi.

Kiukweli tunasafari ndefu sana ili tuje kufika salama mwisho wa hii safari.

#Analyse
 
Right "We are selfish and very lazy" Hata jiran hutaki kumsaidia so unategemea u gonna win? Never happen at all 🙂, "work hard, love each other, help your fellow and God bless you all the time" Kwan wazungu wapoje? Kila kukicha utasikia wametoa msaada wa vitu mbalimbali, ww hata kiberiti tu jirani yako unamnyima!
 
Ujinga ni kusema umaskini umetokana na ukoloni....

Nchi ngapi zimetawaliwa lakini zimeendelea... India walitawaliwa na Uingereza, leo hii wapo wapi??.. Je hakuna ukoloni mambo leo kwao... Bei zao za mazao hazipangwi na mabepari lakini mbona wameendelea??
 
Ujinga ni kusema umaskini umetokana na ukoloni....

Nchi ngapi zimetawaliwa lakini zimeendelea... India walitawaliwa na Uingereza, leo hii wapo wapi??.. Je hakuna ukoloni mambo leo kwao... Bei zao za mazao hazipangwi na mabepari lakini mbona wameendelea??

umasikini wa India wabongo hatuingii hata asilimia 1.....we jidanganye na show offs za kwenye TV ,Net nk..ukienda kule physically ndiyo utajua kuwa bongo tunacheza kwa umasikini
 
umasikini wa India wabongo hatuingii hata asilimia 1.....we jidanganye na show offs za kwenye TV ,Net nk..ukienda kule physically ndiyo utajua kuwa bongo tunacheza kwa umasikini

hivi unajua india peke yao ni wengi zaidi ya waafrika wote??,,,,,,, lakini pamoja na hayo yote wametumia asilimia kubwa ya Population positively ukilinganisha na sisi ambapo nchi ni zina watu wachache ila tupo busy tunauwana tuuuu...kama congo
 
ningeshauri msome kitabu kinachoitwa'HOW EUROPE UNDERDEVELOPED AFRICA'cha WALTER RODNEY
 
Uvivu wetu na ilengojangoja ntatenda kesho yaani jambo la litatekelezwa wiki ijayo huo Mf mmoja wao..
 
Back
Top Bottom