Kwanini TFF wanataka kumhujumu Samatta

Mnaonaje mkichanga nauli tumia hii namba spesho tigo pesa 0713567098
 
Sioni hoja zozote hapo zaidi ya kuwasakama TFF kwa uvivu wako wa kuamka! Kama kweli watanzania ni wazalendo amkeni hiyo saa 8 mmpokee shujaa wetu acha kumpa lawama malinzi zisizo na tija!
 
Hakuna Samatta bila ya TP Mazembe..... Wabongo tunadandia tu Treni kwa mbele.


Wanaopaswa kusherehekea ni Kongo sio Tanzania.


Ninveungana na wewe kama angekuwa anachezea Timu zetu za nyumbani.


Hongera Samatta, Hongera TP Mzembe.
 
Hakuna haja ya kuilaumu CAF. shirikisho letu, TFF ndo la kulaumiwa
Umenena vema mkuu, shirika la TFF+malinzi wameshindwa kuthamin mchango wa SAMATTA.nawataka maramoja kuhakikisha mchezaji wetu anabadilishiwa ndege ikiwezekana na muda wa kuondoka il aweze kupokelewa na wananchi na washabiki wa michezo

#viva_samatta_viva
 
Hakuna Samatta bila ya TP Mazembe..... Wabongo tunadandia tu Treni kwa mbele.


Wanaopaswa kusherehekea ni Kongo sio Tanzania.


Ninveungana na wewe kama angekuwa anachezea Timu zetu za nyumbani.


Hongera Samatta, Hongera TP Mzembe.
Au sio? Jirani kanunua gari unashangilia wewe
 
Sioni hoja zozote hapo zaidi ya kuwasakama TFF kwa uvivu wako wa kuamka! Kama kweli watanzania ni wazalendo amkeni hiyo saa 8 mmpokee shujaa wetu acha kumpa lawama malinzi zisizo na tija!

ningekushangaa kama usingejitokeza kumtetea " mhaya " mwenzio Jamal Malinzi. leo ngoja sisi Watani zenu tuwaache msemwe kupitia huyo inshomirye mwenzenu.
 
Kwanini usiamke saa 6ukaenda kumpokea? hebu acha uvivu...
 
sijajua samatta kabila gani lakini angekua wa lile kabila la tff angeandaliwa msafara wa hatari niwe mkweli hawa tff wachunguzwe ikiwa ni watanzania kweli haiingii akilini mtu aongoze africa afu nyumbani hakuna shamra zozote za kumpokea
 

kama tuliweza KUKESHA kusubiria MATOKEO ya UCHAGUZI karibia maeneo mengi tu ya Tanzania huku TUKIFURAHIA iweje tushindwe kujitokeza kwa moyo ule ule na morali ile ile kumpokea SHUJAA wetu POPA? naona huu UZI wako umeuandika KINAFIKI sana na hukuushughulisha UBONGO wako sawa sawa. halafu inaonyesha kuwa una BIFU lako tu na Mtani wangu wa Kihaya JAMAL MALINZI kwani umeshindwa kujua kuwa TFF ni TAASISI na si ya MALINZI kama MALINZI. wakati UNAJITUTUMUA kuandika hii kitu ulijaribu kutafuta references zingine za tukio kama hili na ukaona labda wenzetu waliwezaje? tena mimi ndiyo nina hamu kweli aje muda huo huo wa saa nane ( 8 ) usiku mnene ili tupime UZALENDO wa Watanzania hasa wapenda michezo. tuache KULALAMIKA sana vitu hivi vingine vina PROTOKALI zake jamani. halafu kila mara kutulinganisha sisi na Wakenya unataka tukueleweje mkuu? wao hao Wakenya kuna lipi wanalokuiga wewe Mtanzania? kaishi huko Kenya basi shabaaaaaaaaash!
 
Badala ya kujaza posts humu, changeni pesa mlipieni hotel kwa siku moja zaidi na kisha mlipie gharama za kubadilisha tiketi ya ndege yake.
 
Mbona hasira sasa, kwani saa nane usiku umekatazwa kwenda?
 
Watanzania acheni kelele na maneno. Badala ya kuanza vijembe na alipofikia Samatta mnasahau kwamba ni tabia na juhudi zake binafsi. Na uenda akawa bado ana ndoto za kucheza champions league na kuchukua kikombe sasa unadhani kumpokea eapoti ndiko kutamfikisha huko!?
 
Paragraphs 4 zimentosha... ni kweli kabisa unayosema mkuu.... watu baadhi wana vimtima nyongo ..... ila wengi tumeiona heshima kubwa aliyotupatia Samatta
 
Samatta hahitaji hiyo staili ya upokeaji ili apate
soko ,anajimarket mwenyewe tengenezeni akina samatta wengine,yuko wapi Yusuph soka,Notkelly masasi na wengine? Tuache kudandia lory kwa mbele.samatta na kasongo washamaliza kazi yao
 

Wana JF, hii ni hoja nzito na ina MANTIKI, ni vema rais wetu Mh. jogn Pombe Magufuli akalipa uzito wa kipee suala hili, angalau amuagize Naibu wake au Waziri Mkuu atuongoze kwenda kumpokea uwanja lakini iwe baada ya kufanya mipango kurekebisha ratiba ya safari yake ili afike mchna kweupe ili wana dar es salaam waandamane kumpokea tena kwa ning'ora...huyu ni SHUJAAAAAAAA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…