Kwanini TFF wanataka kumhujumu Samatta

Kwanini TFF wanataka kumhujumu Samatta

Mnaonaje mkichanga nauli tumia hii namba spesho tigo pesa 0713567098
 
Sioni hoja zozote hapo zaidi ya kuwasakama TFF kwa uvivu wako wa kuamka! Kama kweli watanzania ni wazalendo amkeni hiyo saa 8 mmpokee shujaa wetu acha kumpa lawama malinzi zisizo na tija!
 
Hakuna Samatta bila ya TP Mazembe..... Wabongo tunadandia tu Treni kwa mbele.


Wanaopaswa kusherehekea ni Kongo sio Tanzania.


Ninveungana na wewe kama angekuwa anachezea Timu zetu za nyumbani.


Hongera Samatta, Hongera TP Mzembe.
 
Hakuna haja ya kuilaumu CAF. shirikisho letu, TFF ndo la kulaumiwa
Umenena vema mkuu, shirika la TFF+malinzi wameshindwa kuthamin mchango wa SAMATTA.nawataka maramoja kuhakikisha mchezaji wetu anabadilishiwa ndege ikiwezekana na muda wa kuondoka il aweze kupokelewa na wananchi na washabiki wa michezo

#viva_samatta_viva
 
Hakuna Samatta bila ya TP Mazembe..... Wabongo tunadandia tu Treni kwa mbele.


Wanaopaswa kusherehekea ni Kongo sio Tanzania.


Ninveungana na wewe kama angekuwa anachezea Timu zetu za nyumbani.


Hongera Samatta, Hongera TP Mzembe.
Au sio? Jirani kanunua gari unashangilia wewe
 
Sioni hoja zozote hapo zaidi ya kuwasakama TFF kwa uvivu wako wa kuamka! Kama kweli watanzania ni wazalendo amkeni hiyo saa 8 mmpokee shujaa wetu acha kumpa lawama malinzi zisizo na tija!

ningekushangaa kama usingejitokeza kumtetea " mhaya " mwenzio Jamal Malinzi. leo ngoja sisi Watani zenu tuwaache msemwe kupitia huyo inshomirye mwenzenu.
 
Umenena vema mkuu, shirika la TFF+malinzi wameshindwa kuthamin mchango wa SAMATTA.nawataka maramoja kuhakikisha mchezaji wetu anabadilishiwa ndege ikiwezekana na muda wa kuondoka il aweze kupokelewa na wananchi na washabiki wa michezo

#viva_samatta_viva
Kwanini usiamke saa 6ukaenda kumpokea? hebu acha uvivu...
 
sijajua samatta kabila gani lakini angekua wa lile kabila la tff angeandaliwa msafara wa hatari niwe mkweli hawa tff wachunguzwe ikiwa ni watanzania kweli haiingii akilini mtu aongoze africa afu nyumbani hakuna shamra zozote za kumpokea
 
Hii nchi kuna watu wanapaswa kufungwa au kupewa adhabu kali iwe fundisho. Miongoni mwao ni Rais wa TFF Jamal Malinzi na safu yake ya uongozi. Ningekua na mamlaka Malinzi leo angelala "Keko au Segerea".

Mbwana Sammata ameleta HESHIMA KUBWA sana Tanzania ambayo viongozi wa kisiasa wameshindwa kutuletea kwa miaka zaidi ya 50. Ushindi wa tuzo ya Mwanasoka bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani ni ushindi mkubwa sana kwa taifa letu. Sammata ameitangaza nchi yetu kwa kiwango kikubwa sana. Waliokua hawaijui Tanzanua sasa wataijua bila kupenda.

Brother Anthony Mtaka ambaye ni mwanasiasa hodari, msomi na miongoni mwa watu wachache ndani ya CCM wanaonivutia kisiasa; amesema kuwa Sammata ametangaza Tanzania vizuri kuliko viongozi wa Serikali waliotumia mabilioni ya fedha kwa miaka kumi mfululizo (2005 -2015) kutangaza vivutio vya utalii na wakashindwa.

Ni wazi kuwa heshima aliyotupa Sammata ni kubwa sana na tunapaswa kuheshimu mchango wake hasa ukizingatia kwamba amefika hapo kwa juhudi binafsi. Sio TFF wala Serikali zilizochangia mafanikio ya Sammata. Ni yeye mwenyewe na Mungu wake.

So ilitakiwa TFF waweke utaratibu mzuri wa kumpokea Samatta kwa heshima. Ikiwezekana watu wafanye maandamano ya amani kuanzia pale Airport wanapompokea hadi mahali watakapokutanikia. Kama tunaandamana kwa sababu za kisiasa kwanini tusiandamane kumpongeza mtanzania mwenzetu aliyeitangaza vema nchi yetu kimataifa?

Tena ingepaswa tuwe na Media Campaign maalum ya kumpongeza Samatta. Na tufanye "hashtag" kwenye mitandao ya kijamii kama FB, Tweeter, Instagram etc. Tujenge ushawishi watu wajitokeze kwa wingi uwanja wa ndege wa JNIA hadi Sammata mwenyewe asikie fahari na ajivunie kuwa Mtanzania.

Lakini cha ajabu TFF kwa kushirikiana na CAF wameamua kumhujumu Samatta. Na serikali imekaa kimya as if ni sawa. Rais wa TFF Jamal Malinzi ameandika kupitia ukurasa wake wa Tweeter kuwa Samatta atatua nchini saa 8 za usiku kesho jumamosi. Seriously?? Saa 8 usiku? Apokelewe na "wanga" au?

Rafiki yangu Ezekiel Kamwaga amehoji kwanini isitafutwe ndege ya saa 4 asubuhi kesho ili watu waweze kujitokeza kwa wingi kumpokea? Hivi kweli hatuwezi kum-market shujaa wetu?? Kama tulishindwa kumsaidia kufika hapo alipofika, hata kumfanyia marketing tunashindwa? Hivi mnadhani Samatta angekua Mkenya angepokelewa saa 8 za usiku? TFF kuweni serious kidogo, acheni ujinga.!

Saa 8 za usiku watu wanakoroma vitandani, wengine wako club wameshalewa "ndovu baridi" ndio mmeona ni muda mzuri wa kumpokea Sammata? Wanaopokelewa usiku wa manane ni "majambazi" sio shujaa kama Samatta.

Halafu Malinzi kwa kujishtukia anajaribu kupunguza ukali wa maneno na kusema eti Sammata atatua kesho "saa 8 alfajiri". Hakuna kitu kinachoitwa "saa 8 alfajiri" kwenye Kiswahili. Ni saa 8 usiku. Alfajiri inaanza saa 10. Sasa hiyo alfajiri ya Malinzi ya saa 8 usiku ameitoa wapi?

Pia utetezi wa Malinzi ni wa "kitoto sana". Sio utetezi wa kiongozi tena wa taasisi kubwa kama TFF. Malinzi anasema saa 8 usiku ndio muda ambao Sammata amekatiwa ticket na Shirikisho ls Soka Afrika (CAF ) ambaao ndio waandaaji wa tuzo hizo. Hivi kwani kila wanachofanya CAF lazima tukubaliane nacho bila kuhoji?

Ilipaswa TFF wajiulize kwanini CAF wamemkatia Samnata ndege ya usiku wakati ndege za asubuhi au mchana zipo.? Jibu ni rahisi tu kwamba CAF wanaendeleza juhudi zao za kuhujumu nchi za Afrika Mashariki. Hawapendi kabisa kuona nchi zetu za Afrika Mashariki zikifanikiwa kisoka. Ndio maana hata kwenye michuano ya kimataifa wamekua wakitupanga na timu ngumu kama "Ghana, Senegal, Cameroon, Algeria, Misri, Nigeria" etc ili tusifike mbali.

Kwahiyo hili la kumpangia Sammata kurudi saa 8 usiku sio bahati mbaya. Itz a planned and organized matter. Lengo lao tushindwe kumpa Sammata mapokezi mazuri na ya heshima. Kwahiyo ilitakiwa viongozi wa TFF waione hujuma hii na waikatae.

Sifa ya kiongozi (Leader) ni kuona pale ambapo wengine hawawezi kuona. So TFF walitakiwa waone kuwa muda aliopangiwa Sammata (saa 8 usiku) ni hujuma za CAF, then wafikirie mbinu mbadala ya kukataa hujuma hiyo. Ikiwezekana kumfanyia booking upya Samatta ili atue nchini Asubuhi, Mchana au jioni muda ambao watu wengi wanaweza kujitokeza kumpokea.

Lakini viongozi wa TFF wanakaa na vitambi vyao vya "majani ya chai" wanakubaliana tu na CAF bila hata kufikiri kidogo. Huu ni ujinga ambao hata Mwenyekiti wa "vichaa duniani" hawezi kuufanya.

Ingekua Sammata ni mKenya; kwanza wangekataa hiyo ticket ya CAF ya saa 8 usiku. Then wangemfanyia booking upya Samatta kwa pesa zao ili aweze kutua kwa muda wanaotaka wao. Na ingewezekana wangemtumia hata ndege maalumu ya kwenda kumchukua.

Lakini hapa bongo TFF wamekaa tu kama "mazuzu" wanakimbilia kuandika Tweeter bila aibu eti Samatta atatua kesho saa 8 usiku. Nani akampokee saa 8 usiku? Labda Malinzi na familia yake.

MY TAKE.!
Natoa wito kwa watumiaji wote wa mitandao Tushikamane kwa umoja wetu bila kujali vyama vyetu, dini, kabila au timu tunazoshabikia, tupige kelele mitandaoni kuhakikisha Samatta anatua nchini muda ambao watanzania tunaweza kwenda kumpokea.

Kama itakosekana ndege ya kesho mchana bora aje Jumapili asubuhi kuliko kuja hiyo kesho saa 8 usiku. Share ujumbe huu, mtag kiongozi yeyote wa Serikali au wa TFF. Kama una namba zao wapigie au watumie sms kuonesha kulaani hujuma inayotaka kufanywa dhidi ya Sammata ya kumpokea saa 8 za usiku.

Tunamtaka Sammata muda ambao tunaweza kumpokea sio saa 8 za usiku.

#JUSTICE_4_SAMMATA.!

kama tuliweza KUKESHA kusubiria MATOKEO ya UCHAGUZI karibia maeneo mengi tu ya Tanzania huku TUKIFURAHIA iweje tushindwe kujitokeza kwa moyo ule ule na morali ile ile kumpokea SHUJAA wetu POPA? naona huu UZI wako umeuandika KINAFIKI sana na hukuushughulisha UBONGO wako sawa sawa. halafu inaonyesha kuwa una BIFU lako tu na Mtani wangu wa Kihaya JAMAL MALINZI kwani umeshindwa kujua kuwa TFF ni TAASISI na si ya MALINZI kama MALINZI. wakati UNAJITUTUMUA kuandika hii kitu ulijaribu kutafuta references zingine za tukio kama hili na ukaona labda wenzetu waliwezaje? tena mimi ndiyo nina hamu kweli aje muda huo huo wa saa nane ( 8 ) usiku mnene ili tupime UZALENDO wa Watanzania hasa wapenda michezo. tuache KULALAMIKA sana vitu hivi vingine vina PROTOKALI zake jamani. halafu kila mara kutulinganisha sisi na Wakenya unataka tukueleweje mkuu? wao hao Wakenya kuna lipi wanalokuiga wewe Mtanzania? kaishi huko Kenya basi shabaaaaaaaaash!
 
Badala ya kujaza posts humu, changeni pesa mlipieni hotel kwa siku moja zaidi na kisha mlipie gharama za kubadilisha tiketi ya ndege yake.
 
Watanzania acheni kelele na maneno. Badala ya kuanza vijembe na alipofikia Samatta mnasahau kwamba ni tabia na juhudi zake binafsi. Na uenda akawa bado ana ndoto za kucheza champions league na kuchukua kikombe sasa unadhani kumpokea eapoti ndiko kutamfikisha huko!?
 
Paragraphs 4 zimentosha... ni kweli kabisa unayosema mkuu.... watu baadhi wana vimtima nyongo ..... ila wengi tumeiona heshima kubwa aliyotupatia Samatta
 
Samatta hahitaji hiyo staili ya upokeaji ili apate
soko ,anajimarket mwenyewe tengenezeni akina samatta wengine,yuko wapi Yusuph soka,Notkelly masasi na wengine? Tuache kudandia lory kwa mbele.samatta na kasongo washamaliza kazi yao
 
Hii nchi kuna watu wanapaswa kufungwa au kupewa adhabu kali iwe fundisho. Miongoni mwao ni Rais wa TFF Jamal Malinzi na safu yake ya uongozi. Ningekua na mamlaka Malinzi leo angelala "Keko au Segerea".

Mbwana Sammata ameleta HESHIMA KUBWA sana Tanzania ambayo viongozi wa kisiasa wameshindwa kutuletea kwa miaka zaidi ya 50. Ushindi wa tuzo ya Mwanasoka bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani ni ushindi mkubwa sana kwa taifa letu. Sammata ameitangaza nchi yetu kwa kiwango kikubwa sana. Waliokua hawaijui Tanzanua sasa wataijua bila kupenda.

Brother Anthony Mtaka ambaye ni mwanasiasa hodari, msomi na miongoni mwa watu wachache ndani ya CCM wanaonivutia kisiasa; amesema kuwa Sammata ametangaza Tanzania vizuri kuliko viongozi wa Serikali waliotumia mabilioni ya fedha kwa miaka kumi mfululizo (2005 -2015) kutangaza vivutio vya utalii na wakashindwa.

Ni wazi kuwa heshima aliyotupa Sammata ni kubwa sana na tunapaswa kuheshimu mchango wake hasa ukizingatia kwamba amefika hapo kwa juhudi binafsi. Sio TFF wala Serikali zilizochangia mafanikio ya Sammata. Ni yeye mwenyewe na Mungu wake.

So ilitakiwa TFF waweke utaratibu mzuri wa kumpokea Samatta kwa heshima. Ikiwezekana watu wafanye maandamano ya amani kuanzia pale Airport wanapompokea hadi mahali watakapokutanikia. Kama tunaandamana kwa sababu za kisiasa kwanini tusiandamane kumpongeza mtanzania mwenzetu aliyeitangaza vema nchi yetu kimataifa?

Tena ingepaswa tuwe na Media Campaign maalum ya kumpongeza Samatta. Na tufanye "hashtag" kwenye mitandao ya kijamii kama FB, Tweeter, Instagram etc. Tujenge ushawishi watu wajitokeze kwa wingi uwanja wa ndege wa JNIA hadi Sammata mwenyewe asikie fahari na ajivunie kuwa Mtanzania.

Lakini cha ajabu TFF kwa kushirikiana na CAF wameamua kumhujumu Samatta. Na serikali imekaa kimya as if ni sawa. Rais wa TFF Jamal Malinzi ameandika kupitia ukurasa wake wa Tweeter kuwa Samatta atatua nchini saa 8 za usiku kesho jumamosi. Seriously?? Saa 8 usiku? Apokelewe na "wanga" au?

Rafiki yangu Ezekiel Kamwaga amehoji kwanini isitafutwe ndege ya saa 4 asubuhi kesho ili watu waweze kujitokeza kwa wingi kumpokea? Hivi kweli hatuwezi kum-market shujaa wetu?? Kama tulishindwa kumsaidia kufika hapo alipofika, hata kumfanyia marketing tunashindwa? Hivi mnadhani Samatta angekua Mkenya angepokelewa saa 8 za usiku? TFF kuweni serious kidogo, acheni ujinga.!

Saa 8 za usiku watu wanakoroma vitandani, wengine wako club wameshalewa "ndovu baridi" ndio mmeona ni muda mzuri wa kumpokea Sammata? Wanaopokelewa usiku wa manane ni "majambazi" sio shujaa kama Samatta.

Halafu Malinzi kwa kujishtukia anajaribu kupunguza ukali wa maneno na kusema eti Sammata atatua kesho "saa 8 alfajiri". Hakuna kitu kinachoitwa "saa 8 alfajiri" kwenye Kiswahili. Ni saa 8 usiku. Alfajiri inaanza saa 10. Sasa hiyo alfajiri ya Malinzi ya saa 8 usiku ameitoa wapi?

Pia utetezi wa Malinzi ni wa "kitoto sana". Sio utetezi wa kiongozi tena wa taasisi kubwa kama TFF. Malinzi anasema saa 8 usiku ndio muda ambao Sammata amekatiwa ticket na Shirikisho ls Soka Afrika (CAF ) ambaao ndio waandaaji wa tuzo hizo. Hivi kwani kila wanachofanya CAF lazima tukubaliane nacho bila kuhoji?

Ilipaswa TFF wajiulize kwanini CAF wamemkatia Samnata ndege ya usiku wakati ndege za asubuhi au mchana zipo.? Jibu ni rahisi tu kwamba CAF wanaendeleza juhudi zao za kuhujumu nchi za Afrika Mashariki. Hawapendi kabisa kuona nchi zetu za Afrika Mashariki zikifanikiwa kisoka. Ndio maana hata kwenye michuano ya kimataifa wamekua wakitupanga na timu ngumu kama "Ghana, Senegal, Cameroon, Algeria, Misri, Nigeria" etc ili tusifike mbali.

Kwahiyo hili la kumpangia Sammata kurudi saa 8 usiku sio bahati mbaya. Itz a planned and organized matter. Lengo lao tushindwe kumpa Sammata mapokezi mazuri na ya heshima. Kwahiyo ilitakiwa viongozi wa TFF waione hujuma hii na waikatae.

Sifa ya kiongozi (Leader) ni kuona pale ambapo wengine hawawezi kuona. So TFF walitakiwa waone kuwa muda aliopangiwa Sammata (saa 8 usiku) ni hujuma za CAF, then wafikirie mbinu mbadala ya kukataa hujuma hiyo. Ikiwezekana kumfanyia booking upya Samatta ili atue nchini Asubuhi, Mchana au jioni muda ambao watu wengi wanaweza kujitokeza kumpokea.

Lakini viongozi wa TFF wanakaa na vitambi vyao vya "majani ya chai" wanakubaliana tu na CAF bila hata kufikiri kidogo. Huu ni ujinga ambao hata Mwenyekiti wa "vichaa duniani" hawezi kuufanya.

Ingekua Sammata ni mKenya; kwanza wangekataa hiyo ticket ya CAF ya saa 8 usiku. Then wangemfanyia booking upya Samatta kwa pesa zao ili aweze kutua kwa muda wanaotaka wao. Na ingewezekana wangemtumia hata ndege maalumu ya kwenda kumchukua.

Lakini hapa bongo TFF wamekaa tu kama "mazuzu" wanakimbilia kuandika Tweeter bila aibu eti Samatta atatua kesho saa 8 usiku. Nani akampokee saa 8 usiku? Labda Malinzi na familia yake.

MY TAKE.!
Natoa wito kwa watumiaji wote wa mitandao Tushikamane kwa umoja wetu bila kujali vyama vyetu, dini, kabila au timu tunazoshabikia, tupige kelele mitandaoni kuhakikisha Samatta anatua nchini muda ambao watanzania tunaweza kwenda kumpokea.

Kama itakosekana ndege ya kesho mchana bora aje Jumapili asubuhi kuliko kuja hiyo kesho saa 8 usiku. Share ujumbe huu, mtag kiongozi yeyote wa Serikali au wa TFF. Kama una namba zao wapigie au watumie sms kuonesha kulaani hujuma inayotaka kufanywa dhidi ya Sammata ya kumpokea saa 8 za usiku.

Tunamtaka Sammata muda ambao tunaweza kumpokea sio saa 8 za usiku.

#JUSTICE_4_SAMMATA.!

Wana JF, hii ni hoja nzito na ina MANTIKI, ni vema rais wetu Mh. jogn Pombe Magufuli akalipa uzito wa kipee suala hili, angalau amuagize Naibu wake au Waziri Mkuu atuongoze kwenda kumpokea uwanja lakini iwe baada ya kufanya mipango kurekebisha ratiba ya safari yake ili afike mchna kweupe ili wana dar es salaam waandamane kumpokea tena kwa ning'ora...huyu ni SHUJAAAAAAAA.
 
Back
Top Bottom