Kwanini TRA wametangaza kazi kwenye website yao ikiwa kuna ajira portal (Utumishi)?

Loading failed

JF-Expert Member
Joined
Sep 14, 2023
Posts
2,603
Reaction score
7,501
Ndugu zangu.

1: Ni kwanini basi TRA watangaze kazi kwenye website yao na maombi yatumwe kwao direct ikiwa kuna ajira portal ?


2: Na ikiwa kama serikali imewapa mamlaka na kibali cha kuajiri , kwanini haijafanya hivyo kwa mashirika na taasisi zingine zote kufata mfumo huo huo wa kuajiri wenyewe na kuachana kabisa na ajiral portal?

3: i) Je, kwanini kunachangamoto kubwa sana ya kusingn up kwenye website ya TRA ili uweze kubahatisha nafasi zao pasi na kuhusisha waombaji ni wengi , kwanini isiwe easy kama ajira portal?

ii) Na kwanini basi ikiwa umepata kadhia ya kusingup , ukidirectiwa kwenye ku-click "Ok" ili upate support haileti msaada wowote ule ?
 

Wahusika wanapaswa wajitokeze na kujibu Hoja hii.
Lakini huenda pengine wamepata Kibali Cha kufanya hivyo.
Ila wasi wasi wangu mkubwa sana ni kuwa Mchakato wa Recruitment ya Ajira hizo utagubikwa kabisa na vitendo vya rushwa na Upendeleo.

TRA mpaka sasa tayari ina madoa ya kuwepo kwa ajira za upendeleo kwa misingi ya Ukabila (Kabila la Watu wengi wa kutoka Ukanda ule kule juu wanatuhumiwa kutoa ajira za upendeleo katika Taasisi hii). Katika hili, TRA wanapaswa wajiepushe kabisa na kadhia Kama hii ya upendeleo wa ajira kwa misingi ya Ukabila.
 
Nakumbuka mwaka 2017 kuna mama mmoja alipata ajira TRA kama management officer bila hata kufanya interview yoyote, ilileta gumzo sana, na kipindi hicho zoezi zima la recruitment lilikuwa linasimamiwa na secretariat ya ajira, sasa imagine sasa hivi ambapo kila kitu kinaendeshwa na TRA wenyewe itakuwaje tena chini ya serikali hii ambayo haina muda wa kufuatilia ufanisi wa waajiri wake..
 
 

Attachments

  • IMG-20250209-WA0004.jpg
    183.7 KB · Views: 2
Rais alishatoa maagizo kwa taasisi za kiserikali ambazo zinahitaji kuajiri na zikaona kuwa utumishi wanaweza kuwachelewesha ziajiri. Kwa hivo hawajavunja utaratibu wowote
 
Rais alishatoa maagizo kwa taasisi za kiserikali ambazo zinahitaji kuajiri na zikaona kuwa utumishi wanaweza kuwachelewesha ziajiri. Kwa hivo hawajavunja utaratibu wowote
Kama kweli hali iko hivyo, basi hapa watoto wa walalahoi wahesabie wameumia.
Hapa kazi itakuwa ni moja tu: No Corruption No Job!
Period!
 
Nafasi 50 Wahitaji elfu 50 hata ingekuwa wewe unasimamia unafanyeje?Mkimaliza vigezo vya cv wanabaki elfu 40,mnatafuta Wajomba,Baba Wadogo,jirani wanabaki elfu hatimaye mnahamia kwenye ukanda,ukabila,ukoo,kukutana n.k.Then wanamalizia kwa bwana adui wa haki.
 
TRA NI WAHUNI SANA MWAKA JANA NILI APPLY KAZI ZAO ILA SIKWENDA KWENYE INTERVIEW CHA KUSHANGAZA NILIKUJA KUTUMIWA EMAIL YA MATOKEO YA INTERVIEW HADI MARKS ZANGU AMBAZO ZILIKUWA HAZITOSHI KWENDA HATUA YA ORAL INTERVIEW NA MKUMBUKE SIKUFANYA KABISA INTERVIEW YA KWANZA ,KWA IYO INTERVIEW ZAO ZIMEJAA UHUNI MWINGI SANA
 
Kila mtu anataka kuweka ndugu yake hapo, ikipitia utumishi watashindwa
 
Duh inamaana matokeo niya kuforge mzee aisee kama huna connection ni hatari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…