Kwanini tunaenzi wanasiasa peke yao?

Kwanini tunaenzi wanasiasa peke yao?

Fundi Mchundo

Platinum Member
Joined
Nov 9, 2007
Posts
10,448
Reaction score
8,705
Kuna taarifa kuwa stesheni za SGR zitapewa majina ya marais wetu. Huu ni muendelezo wa karibu kila kitu cha maana kupewa jina la aliyekuwa Rais (hivi karibuni ni Rais aliyekuwa madarakani).

Tuna shule zinazoitwa Mkapa, Vitengo vya Hospitali vinavyoitwa Kikwete, stesheni za basi za Magufuli, Kiwanja cha ndege cha Nyerere, na sasa hivi tunajenga uwana wa michezo wa Samia Suluhu Hassan Arusha! Hivi ni wana siasa peke yao ndio walioifikisha nchi yetu hapa tulipo?

Kwa nini hizi stesheni hazikupewa majina kama Shaaban Robert (Dar es Salaam), Mbaraka Mwinshehe (Morogoro), Isike (Tabora) na mashujaa wetu wengine ambao tumewasahau! Ingekuwa nafasi nzuri yakuibua watu waliochangia historia yetu kutoka kila sehemu ambayo reli inapita. Kutumia majina ya wanasiasa kunageuza kitu ambacho watanzania wote tumechangia kuwa na sura ya kichama maana hamna mwanasiasa wa upinzani atapewa heshima kama hiyo.

Inabidi tubadilike na tuandike upya historia yetu kwa kutambua kuwa sio lazima uwe Rais ndio uthaminiwe na nchi yetu.

Amandla.

Pia, soma: Si kila jengo, eneo na barabara lazima ipewe jina la Mwanasiasa au Kiongozi. Kuna Wanamichezo na Wasanii wanaopaswa kuenziwa ili kulinda historia yetu
 
Japo kuezi jambo kwa majina ya viongoji ni kawaida , ila hili lina harufu kubwa ya uchawa na unafki.
Hatukatai viongozi wa serikali kuenziwa lakini hii ya sasa imezidi. Ni kweli kuna harufu ya uchawa na unafik. Na uvivu wa kufikiri.

Nchi yetu ina mashujaa wengi sana katika kila fani. Tunashindwa nini kuwaenzi?

Amandla...
 
Kuna taarifa kuwa stesheni za SGR zitapewa majina ya marais wetu. Huu ni muendelezo wa karibu kila kitu cha maana kupewa jina la aliyekuwa Rais ( hivi karibuni ni Rais aliyekuwa madarakani)! Tuna shule zinazoitwa Mkapa, Vitengo vya Hospitali vinavyoitwa Kikwete, stesheni za basi za Magufuli, Kiwanja cha ndege cha Nyerere, na sasa hivi tunajenga uwana wa michezo wa Samia Suluhu Hassan Arusha! Hivi ni wana siasa peke yao ndio walioifikisha nchi yetu hapa tulipo?

Kwa nini hizi stesheni hazikupewa majina kama Shaaban Robert ( Dar es Salaam), Mbaraka Mwinshehe ( Morogoro), Isike ( Tabora) na mashujaa wetu wengine ambao tumewasahau! Ingekuwa nafasi nzuri yakuibua watu waliochangia historia yetu kutoka kila sehemu ambayo reli inapita. Kutumia majina ya wanasiasa kunageuza kitu ambacho watanzania wote tumechangia kuwa na sura ya kichama maana hamna mwanasiasa wa upinzani atapewa heshima kama hiyo.

Inabidi tubadilike na tuandike upya historia yetu kwa kutambua kuwa sio lazima uwe Rais ndio uthaminiwe na nchi yetu.

Amandla...
Hii inaitwa "Status anxiety".

Kwa sasa unaweza kutua uwanja wa ndege wa Nyerere Dar, ukapita barabara ya Nyerere, ukapita daraja la Nyerere, ukafika chuo cha Nyerere, ukaenda ukumbi wa mikutano wa Nyerere, ukapanda treni Dar mpaka Mwanza, huko Mwanza utashuka kituo cha treni cha Nyerere.

Guess what?

Mwanza nako utakutana na barabara ya Nyerere.

Ukatembelea mbuga ya Nyerere na kuona bwawa la Nyerere.

Huyo Nyerere mwenyewe angekuwepo asingependa jambo hili.
 
Kuna watu walinyongwa kwa sababu walikataa kutawaliwa. Kuna watu walijilipua ili wasitekwe na waliotaka kuwatawala. Kuna watu walikuza lugha ya kiswahili kufikia hapa ilipo. Kuna wachoraji wanaoheshimiwa dunia nzima. Kuna waliotuzwa Nobel Prize. Kuna waliotumia sehemu kubwa ya maisha yao kupigania uhuru wa nchi nyingine za kiafrika.

Kuna wanawake waliopambana kwa dhati ili wanawake wengine wapate haki sawa na wanaume. Kuna wana riadha (John Stephen, Filbert Bayi, Suleiman Nyambui n.k.) na wanamichezo wengine walioheshimisha taifa letu katika majukwaa makubwa duniani. Wote hawa sisi hatuwaoni.

Amandla...
 
Hii inaitwa "Status anxiety".

Kwa sasa unaweza kutua uwanja wa ndege wa Nyerere Dar, ukapita barabara ya Nyerere, ukapita daraja la Nyerere, ukafika chuo cha Nyerere, ukaenda ukumbi wa mikutano wa Nyerere, ukapanda treni Dar mpaka Mwanza, huko Mwanza utashuka kituo cha treni cha Nyerere.

Guess what?

Mwanza nako utakutana na barabara ya Nyerere.

Ukatembelea mbuga ya Nyerere na kuona bwawa la Nyerere.

Huyo Nyerere mwenyewe angekuwepo asingependa jambo hili.
Waliwahi kutaka kuipa jina la Nyerere stadium moja akakataa katakata. Akasema iiteni hata Mandela Stadium lakini sio Nyerere!

Amandla...
 
Kuna taarifa kuwa stesheni za SGR zitapewa majina ya marais wetu. Huu ni muendelezo wa karibu kila kitu cha maana kupewa jina la aliyekuwa Rais ( hivi karibuni ni Rais aliyekuwa madarakani)! Tuna shule zinazoitwa Mkapa, Vitengo vya Hospitali vinavyoitwa Kikwete, stesheni za basi za Magufuli, Kiwanja cha ndege cha Nyerere, na sasa hivi tunajenga uwana wa michezo wa Samia Suluhu Hassan Arusha! Hivi ni wana siasa peke yao ndio walioifikisha nchi yetu hapa tulipo?

Kwa nini hizi stesheni hazikupewa majina kama Shaaban Robert ( Dar es Salaam), Mbaraka Mwinshehe ( Morogoro), Isike ( Tabora) na mashujaa wetu wengine ambao tumewasahau! Ingekuwa nafasi nzuri yakuibua watu waliochangia historia yetu kutoka kila sehemu ambayo reli inapita. Kutumia majina ya wanasiasa kunageuza kitu ambacho watanzania wote tumechangia kuwa na sura ya kichama maana hamna mwanasiasa wa upinzani atapewa heshima kama hiyo.

Inabidi tubadilike na tuandike upya historia yetu kwa kutambua kuwa sio lazima uwe Rais ndio uthaminiwe na nchi yetu.

Amandla...
Jua nguvu ya ubinafsi na majivuno...Bora tunge Enzo MAJINA YA MAPROFESOR kuleta chachu Kwa watoto wako..Ila mitaan majina ya wanajeshi iko nyingi Sana kuliko mafundi mengine. Dr.Tulia street/law., prof Mkenda road /engineer. Prof Lwaitama campus/linguistics, Dr Butogo station/ locomotive, Prof Selam ferry. /Acquacultire...wanasiasa NI matokeo ya majibu mazuri ya walimu wao na mazingira hayo...
 
Waliwahi kutaka kuipa jina la Nyerere stadium moja akakataa katakata. Akasema iiteni hata Mandela Stadium lakini sio Nyerere!

Amandla...
Katika kitabu chake "Mlinzi Mkuu wa Mwalimu Nyerere" Peter D.M Bwambo ameandika kuwa, miaka ya sitini, kuna watu walitaka kuondoa sanamu la Bismin la pale Samora Avenue, ili waweke sanamu la Nyerere.

Lakini Nyerere alikataa katakata jambo hilo.
 
Katika kitabu chake "Mlinzi Mkuu wa Mwalimu Nyerere" Peter D.M Bwambo ameandika kuwa, miaka ya sitini, kuna watu walitaka kuondoa sanamu la Bismin la pale Samora Avenue, ili waweke sanamu la Nyerere.

Lakini Nyerere alikataa katakata jambo hilo.
Nyerere ndiyo maana hakuitwa Mhe alikataa mambo ya kijinga ya kutukuzwa
 
Kuna taarifa kuwa stesheni za SGR zitapewa majina ya marais wetu. Huu ni muendelezo wa karibu kila kitu cha maana kupewa jina la aliyekuwa Rais ( hivi karibuni ni Rais aliyekuwa madarakani)! Tuna shule zinazoitwa Mkapa, Vitengo vya Hospitali vinavyoitwa Kikwete, stesheni za basi za Magufuli, Kiwanja cha ndege cha Nyerere, na sasa hivi tunajenga uwana wa michezo wa Samia Suluhu Hassan Arusha! Hivi ni wana siasa peke yao ndio walioifikisha nchi yetu hapa tulipo?

Kwa nini hizi stesheni hazikupewa majina kama Shaaban Robert ( Dar es Salaam), Mbaraka Mwinshehe ( Morogoro), Isike ( Tabora) na mashujaa wetu wengine ambao tumewasahau! Ingekuwa nafasi nzuri yakuibua watu waliochangia historia yetu kutoka kila sehemu ambayo reli inapita. Kutumia majina ya wanasiasa kunageuza kitu ambacho watanzania wote tumechangia kuwa na sura ya kichama maana hamna mwanasiasa wa upinzani atapewa heshima kama hiyo.

Inabidi tubadilike na tuandike upya historia yetu kwa kutambua kuwa sio lazima uwe Rais ndio uthaminiwe na nchi yetu.

Amandla...
Uliza kwa nini tunaenzi wanasiasa wa CCM tu na siyo wanasiasa. Wakati kuna wanasiasa mahiri waliopigania maendeleo nchi hii na hawapo CCM... Refer Oscar kambona, babu, Mbowe Fundikira, Mapalala etc
 
Uliza kwa nini tunaenzi wanasiasa wa CCM tu na siyo wanasiasa. Wakati kuna wanasiasa mahiri waliopigania maendeleo nchi hii na hawapo CCM... Refer Oscar kambona, babu, Mbowe Fundikira, Mapalala etc
CCM ni wajinga na wabinafsi
 
Uliza kwa nini tunaenzi wanasiasa wa CCM tu na siyo wanasiasa. Wakati kuna wanasiasa mahiri waliopigania maendeleo nchi hii na hawapo CCM... Refer Oscar kambona, babu, Mbowe Fundikira, Mapalala etc
Wanaoenziwa ni viongozi wa juu wa serikali, Bunge na Mahakama. Wote hawa ni wa CCM. Watu kama Mtikila, Maalim hawawezi kupewa nafasi.

Amandla...
 
Wanaoenziwa ni viongozi wa juu wa serikali, Bunge na Mahakama. Wote hawa ni wa CCM. Watu kama Mtikila, Maalim hawawezi kupewa nafasi.

Amandla...
Kwa nini? Waenziwe hao tu? Kwa nini walio nje ya CCM wasienziwe? Mikoani na mijini naona shule zina majina ya kina Mary Nagu, maghembe etc hao ni viongozi wakuu?
 
Hadi inachosha, kila kona wapo. Wamekuwa kama Big Brother katika nafsi nyingi. Ya Moro iitwe Kisabengo. Nadhani tunahitaji sheria juu ya upaji majina wa vitu vya umma.
 
Back
Top Bottom