Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
- Thread starter
-
- #41
Waheshimiwa wabunge wangetusaidia sana kuhakikisha hizi hospitali zetu zinaboreshwa. Lakini inasemekana na wao wako entitled kutibiwa nje !!
Nilkuwa India karibuni kwa matibabu, self paid!!!
Afya ya mtu si mahali pa pata potea if you are serious with your health.Kama una fanya kazi basi unafanya hivyo kwa vile you are healthy.
Sekta ya afya nchini imezorota sana na si siri katika miaka 20 iliyopita.
Madaktari wanaingia mgomo, wahudumu vilevile.
Nenda Mwanyanyamala at your own risk!!
Katika siku ya leo ambapo unaweza katwa kichwa badala ya operation ya mguu is a serious problem.Tena very serious kwa Hospitali kuu nchini, MNH, Muhimbili Medical Centre.
Mgonjwa wa akili anaua wagonjwa wenziwe wodini!
Madaktari na matibabu karibu wote hawalipwi vizuri na wana miradi yao ya pembeni, concentration kazini hakuna.Daktari atafanya operation akifikiria ukata uliopo nyumbani.
Katika scenario hii mkuu MKJJ ukijipeleka Muhimbili ukiwa na kauwezo ka kujilipia , then you are not serious with your health.
Najua vizuri kuwa kupelekwa katika hospitali zetu kwa wakati mwingine ni jambo ambalo haliepukiki lakini nawahurumia sana wazalendo wenzangu.
Kwanini huyu ndugu yetu ambaye amekuwa akitafuta wawekezaji kote duniani hajapata wawekezaji (siyo wahisani) wa kusaidia huduma ya afya?
a. Wawekezaji ambao watasponsor kufundisha madaktari wetu kwenye vyuo vyetu katika specialities mbalimbali?
b. Wawekezaji ambao wataleta vifaa vya kisasa kuupgrage our aging ones?
c. Wawekezaji ambao wataona kuwa ilipo Hospitali ya Muhimbili sasa hivi pamepitwa na wakati na kutusaidia kujenga the New Muhimbilli Healthy Systems badala ya kuongeza majengo na kupaka rangi mpya. Hiyo Muhimbili ilivyo sasa ibakie kuwa a true Medical Teaching University..
d.
that is exactly my point.. kwanza tuwakatalie hiyo "haki" waliyojipa halafu tuone watafanya nini wakiumwa.. haiwezekani hospitali ziwe mahali pa kupumzikia tu halafu hao wanatimkia SA, India, au kwingine huko.
Halafu katika wazimu wa fikra zao wanakaa na kutuambia wana mpango wa kujenga barabara za kwenda mbinguni!
Mimi nimekaa India na nina ifahamu kwa kiasi fulani na wagonjwa wengi wanaopekwa huko ni baada ya magonjwa yao kuwa jameshindikana hapa Tanzania na sababu huwa ni vifaa na madaktari.
Kiukweli watanzania tuna matatizo sana katika suala la utaalamu si wa kitabibu tu hata wahandisi na technolojia kwa ujumla.maana hata ujenzi wa barabara si wataalamu wote wanatoka nje.sasa tujiulize na hilo!
Nenda pale Apollo Hyderabad hadi wahudumu wa Kihindi sasa wanajua kiwahili maana ndo wangojwa wanao wahudumia kila kukicha.
Na kwa mwaka huu ukienda Apollo Hospital pale Hyderabad au Ahmedabad utakuta watanzania ni wengi kuliko wageni wote wanaofika India kwa matibabu.
Na Tanzania ni nchi inayotajwa kuwa ni wateja wakubwa wa Apollo Hosptials India,kwa ushahidi bofya hapa:
http://www.apollohospitals.com/hosp...-installed-at-apollo-hospitals-hyderabad.html
watanzania tunabidi tujiulize wapi tunaelekea maana ni aibu.
Kuna mwana JF mmoja aliniponda niliposema kwamba Mbunge Sigfrid Ng'itu alikuwa mzalendo kwa sababu "Aliugulia Muhimbili hadi mauti yalipomfika". Mheshimiwa huyu hakwenda "kutibiwa" nje!
Huenda alikuwa na sababu zake!
IDIMI.. sidhani kukubali kuugulia bongo tu hivi hivi ni uzalendo; kwangu ni uzalendo kama angesema nia yake hiyo ya kutaka kutibiwa bongo kwa sababu hataki kutibiwa nje ya nchi. Watu wengi wanaugua na kufia bongo kwani ndiyo hali halisi. Lakini tukiwapiga marufuku hawa wanasiasa kupata "haki" ya kufanyiwa uchunguzi sijui mara mbili kwa mwaka huko majuu kwa gharama ya walipa kodi na kama wakiumwa watatibiwa mahali popote duniani.. labda wataanza kufikiria wafanye nini kuboresha sekta yetu ya afya badala ya kuwaachia wafadhili na wahisani.
IDIMI.. sidhani kukubali kuugulia bongo tu hivi hivi ni uzalendo; kwangu ni uzalendo kama angesema nia yake hiyo ya kutaka kutibiwa bongo kwa sababu hataki kutibiwa nje ya nchi. Watu wengi wanaugua na kufia bongo kwani ndiyo hali halisi. Lakini tukiwapiga marufuku hawa wanasiasa kupata "haki" ya kufanyiwa uchunguzi sijui mara mbili kwa mwaka huko majuu kwa gharama ya walipa kodi na kama wakiumwa watatibiwa mahali popote duniani.. labda wataanza kufikiria wafanye nini kuboresha sekta yetu ya afya badala ya kuwaachia wafadhili na wahisani.
Mkuu Mtazamji
Hii mfano unajenga hoja ambayo inasumbua sana jamii yetu.
Kwa kuongeza tu kwenye Elimu ni hivyo, wenye uwezo wa elimu na fedha wanasomesha watoto wao kwenye Expensive English Medium schools. Kufanya hivi [japo hawataki tuamini hivyo] kunawaondoa wao kabisa kwenye mchakato wa kuboresha Shule za Serikali.
Mifano iko mingi na yote ukiangalia chanzo chake utaona inafanana kitu kimoja muhimu sana "Priority za Taifa", sasa hivi ni tuna kauli mbiu tu. Taifa linapokuwa na priority kila mtanzania anakuwa anajua wajibu...
Nitatumia kipindi cha kwanza cha Rais Mkapa; Serikali iliamua kwa dhati kuwa Taifa ni lazima tulipe madeni ya ndani na nje...sidhani kama kuna Mtanzania asiyejua kuwa Serikali inalipa madeni.
Tunahitaji vipaumbele vya aina hii, mfano kwa nini tusiifanye muhimbili kuwa ndio hospitali bora kuliko zote Afrika? Tukiipa kipaumbele inawezekana....
- Wamarekani walijifunza one thing na mambo ya kukataza ishus muhimu kwa wananchi, kwamba wananchi watatfuta njia zingine hata kuvunja sheria kupata wanachokitaka, ukiwakataza viongozi wetu kutibiwa nje kwa hela za serikali wataenda kwa hela zao na ndipo tutakapoibiwa than never before!
Respect.
FMEs!
Ni muda mrefu sasa tangu nimeanza kusikia kwamba kuna mpango wa kutaka kujenga hospitali kubwa hapa nchini kwa kushirikiana na hospitali ya Apollo, India. Nasikia wazo hilo lilitolewa na uongozi wa hospitali za Apollo baada ya kuona Serikali yetu inapeleka wagonjwa wengi India. Wakashauri kwamba ili kupunguza gharama hizo wako tayari kuisaidia Serikali yetu kujenga hospitali ya aina hiyo na Apollo watatoa wataalamu kuja kuanzisha matibabu na wakati huo huo kuwafunza madaktari hapa kwetu kutumia vyombo ambavyo watakuwa hawajui namna ya kuvitumia. Labda mpango huo ungetekelezwa idadi ya watu 'kukimbilia' India ingepungua.
Siyo Watanzania tu wanaoenda huko. Bali hata Wamarekani, Waingereza, Wacanada na watu wa Mataifa mengine mbali mbali. Madaktari wa Kihindi wamegundua kuna biashara nzuri ya kutibu Wagonjwa. Wengine wamefunga virago toka nchi za Magaribi na kuamua kurudi kwao kufungua hospitali zenye usafi wa hali ya juu, huduma 1st class na bei poa kabisa ukilinganisha na nchi nyingi za Magharibi. Sasa wanavuna walichopanda, na niliwahi kuona CNN Wamarekani mbali mbali walioenda kutibiwa India wakihojiwa na wote walikuwa wanasifia sana huduma kule India na kubaki kuuliza kama India wanaweza kutoa huduma nzuri kiasi kile tena kwa bei poa kabisa kwanini na sisi hapa kwetu tushindwe kufanya hivyo?