Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
Kwa muda mrefu sasa nimeanza kuona mambo fulani makubwa mawili yakitokea inapokuja huduma ya afya.
a. Magonjwa mbalimbali ambayo awali yaliweza kutibiwa katika hospitali zetu yanaanza kupelekwa India. Mtu kamwagiwa tindikali anapelekwa India, mtu anaumwa meno anapelekwa India, mtu kavunjika mguu hadi aende India. Nakumbuka zamani kubwa ilikuwa ni masuala ya moyo. Sasa hivi imefikia hata regular check up inafanywa India, japo zamani tulikuwa tunakimbia hata Nairobi na kwa sisi wengine tunaenda Ndanda au Peramiho.. au hata Bugando. Tumefikaje hapa?
b. Kwa kadiri ya kwamba tunaendelea kutafuta njia mbadala ya kupata tiba na hasa kwa kadiri ya kwamba tunaendelea kuwalipia watawala kwenda kufanyiwa check up na tiba ya magonjwa ya aina yote nje ya nchi, watu hawa hawatofikiria kamwe kuboresha huduma ya afya ya nchini na kuileta kwenye kiwango cha juu cha kimataifa. Zaidi ya yote wataendelea kufungua cliniki na vituo vya afya lakini hawatofikiria kuanzisha kitu kama National Children Hospital au kuigawanya Muhimbili kuwa Muhimbili Healthy Systems badala ya sasa walivyoifanya kuwa tu National Hospital (whatever this means!). Je, kwa kuendelea kuwalipia hawa kana kwamba ni "haki" hatuoni kwamba tumewapa kibali cha kufikiria suala la afya kwa Watanzania kama ni suala "letu" kuliko "lao" kwani wao hawana wasiwasi wapi watatabiwa na nani atawalipia wakiumwa?
Je ipo haja ya kuangalia upya utaratibu wa kuwagharimia viongozi mbalimbali kwenda nchi kwa uchunguzi wa kawaida? Je, tukitaka uchunguzi wa kawaida wote ufanyike nchini yawezekana wakaona uharaka na ulazima wa kuupdate our medical and health facilities?
Ni kwa namna gani suala la afya linaweza kuwa kwenye ajenda ya mwaka huu iili kuweza kuwalazimisha wanasiasa wetu waanze kufikiria hayo mambo mawili hapo juu na kutuongoza kuelekea mabadiliko ambayo yatabadilisha mwelekeo wa sekta yetu ya afya na kuiinua?
a. Magonjwa mbalimbali ambayo awali yaliweza kutibiwa katika hospitali zetu yanaanza kupelekwa India. Mtu kamwagiwa tindikali anapelekwa India, mtu anaumwa meno anapelekwa India, mtu kavunjika mguu hadi aende India. Nakumbuka zamani kubwa ilikuwa ni masuala ya moyo. Sasa hivi imefikia hata regular check up inafanywa India, japo zamani tulikuwa tunakimbia hata Nairobi na kwa sisi wengine tunaenda Ndanda au Peramiho.. au hata Bugando. Tumefikaje hapa?
b. Kwa kadiri ya kwamba tunaendelea kutafuta njia mbadala ya kupata tiba na hasa kwa kadiri ya kwamba tunaendelea kuwalipia watawala kwenda kufanyiwa check up na tiba ya magonjwa ya aina yote nje ya nchi, watu hawa hawatofikiria kamwe kuboresha huduma ya afya ya nchini na kuileta kwenye kiwango cha juu cha kimataifa. Zaidi ya yote wataendelea kufungua cliniki na vituo vya afya lakini hawatofikiria kuanzisha kitu kama National Children Hospital au kuigawanya Muhimbili kuwa Muhimbili Healthy Systems badala ya sasa walivyoifanya kuwa tu National Hospital (whatever this means!). Je, kwa kuendelea kuwalipia hawa kana kwamba ni "haki" hatuoni kwamba tumewapa kibali cha kufikiria suala la afya kwa Watanzania kama ni suala "letu" kuliko "lao" kwani wao hawana wasiwasi wapi watatabiwa na nani atawalipia wakiumwa?
Je ipo haja ya kuangalia upya utaratibu wa kuwagharimia viongozi mbalimbali kwenda nchi kwa uchunguzi wa kawaida? Je, tukitaka uchunguzi wa kawaida wote ufanyike nchini yawezekana wakaona uharaka na ulazima wa kuupdate our medical and health facilities?
Ni kwa namna gani suala la afya linaweza kuwa kwenye ajenda ya mwaka huu iili kuweza kuwalazimisha wanasiasa wetu waanze kufikiria hayo mambo mawili hapo juu na kutuongoza kuelekea mabadiliko ambayo yatabadilisha mwelekeo wa sekta yetu ya afya na kuiinua?