Kwanini tunapenda kutuma pesa (kwa njia ya simu) kuliko benki ambazo huwa na gharama nafuu?

Nenda bank hizi zina gharama nafuu sana
1. DTB
2. Equity Bank
 
Nenda bank hizi zina gharama nafuu sana
1. DTB
2. Equity Bank
 
Mimi binafsi sipogo comfortable na huduma za bank kwasababu zifuatazo.

1. Too much paperwork na wakati wa kufanya hizo paperwork unakutana na ngebe za wafanayakazi wa bank ambao wengi wanakuwa na nyodo sana.

2. Mobile money ni simple and convenient kwa mtu wa kipato cha chini na kati, hatupendi mambo mengi. Ni line ya simu nakwenda kwa mangi naweka hela natumia navyotaka.... No urasimu na kukutana na masura ya watu wanaokudharau wakati hiyo elfu kumi ninayo weka ndio inafanya yeye analipwa mshahara.

3. Mimi huwa sijisikii safe pesa yangu ikiwa bank unless iwe ni pesa kubwa like milioni kuanzia 20. But hizi milioni sijui kumi na kuja tatu mbili naweka tu kwenye line zangu za simu tofauti tofauti zote zinakuwa na hela. Hii ni kunisaidia kuwa na uhakika pesa yangu ipo safe bila makato ya kipuuzi.

4. Sio kweli kuwa hatuoni gharama, tunaiona sana ila its better gharama za wazi kuliko wizi wizi wa kutumia maneno ya kiingereza. Utasikia tumekata subscription fee, mara tumekata joint ventures control maintenance, mara tumekata BOT conference confirmation fee, mara sijui nini na hakuna sehemu utaonyeshwa details za hayo makato ni wizi mtupu.

Ila nikienda kwa wakala, bei ya makato naiona na hakuna zaidi ni ile tu nayoona katika ubao wa charges. Sasa why nihofie na naona ninachokatwa.

5. Bank nilitaasisi likuuubwa na linawafanyakazi wengi sana hapo ndani, how do u expect me kuwa nitakwenda kuweka 50,000 yangu pale kwenye account yao nikaicha miezi sita na still nikaja kutoa hamsini ile ile..... Yaani wale maofisa wanaulambia, wanakuja kazini na magari, wanaingia ofisi inakiyoyozi na furniture za kisasa ili kulinda 50,000 yangu, mmmmmmhmn ngumu kumeza.....
 

Waimize kutumia app zao na ussd code
 
Kiongozi, Chukulia mazingira ya Dar, Jinsi ambavyo ATM ziko maeneo mengi tofauti tofauti, plus unaweza kutoa hela kwa mawakala wa huduma za kifedha kama fahari Huduma na Nmb wakala
Sasa natoa zinatoka wapi, nani aliniwekea hapo ndani?!
 
Benk nyingi unafungua account kwa Tsh 20,000 kwa hiyo kama uko chini ya laki mbili pia unaweza kufuwa na account na ukatoa muda unataka

Je na hili nalo ni shida au ni some complexities tu?
Mobile money nafungua bure..... Hivi hata kujiongeza hapo ni tatizo?!
 
Ni 3500 bro, kama umetumwa hebu kuwa muwazi.....
 
Ukitumia akili ya kisomi utagundua mobile money banking is more convenient than banking directly......

Unajua bank hawapo transparent na shughuli zao.... Hadi uwaulize na unapowauliza utaona wahudumu wanakukodolea yale macho ya unauliza ili iweje sasa, au yale macho ya "heeeeeh brother man wa maana halafu unaulizia kukatwa mia tano looooh" sasa zile noma na kero zingine huwa zinanifanya nijiulize kwan kuna ulazima gani wa kugombana na watu na wakala yupo nje tu hapo.
 
MIMI NINA SWALI MOJA.
KWA NINI HAWAPRINT GHARAMA ZA KUWEKA,KUTOA,KUTUMA NA KUHAMISHA IWEPO KARATASI NTU UKIFIKA TU KWENYE ATM UNAIONA NCHANA KWEUPEE.....
??
 
Mkuu hili andiko lako ni kama hearsay. Ningetamani utoe ulinganifu wa viwango vya kutuma na kutoa fedha kupitia benki na simu ili watu wafanye ulinganifu kuliko hivi ulivyoandika kimipasho.
 
Mkuu siku hiyo boom langu lishatoka napanga foleni kwa teller watu kibao nikasema hapa natoa hadi mia ya mwisho. Sasa upumbavu wa teller nafika foleni yangu eti anauliza kwanini usitolee ATM gharama nafuu kuliko hapa. Ikabidi nikatoe ATM ela iliyobaki nikainunulia vocha. . Mana ku benk fulani ukiacha pesa ukija kesho no salio.

Kimsingi bank za bongo no convenience ya wateja wao wanakera sana foleni lote harafu hakuniudumia.
Nikuulize kwa nn utoe kwa ATM?

Wakati ndani bank teller anakusubiri?
 
Pole chifu
 
Nimetuma saa nzima kulipia hela benki Holland house leo foleni kubwa cashier mmoja yaani benki ovyo Sana ni wastage of time tu
 
Na nauli unayotumia kufika benki usisahau....
 
Aliyesema kufungua akaunti bank ni 20,000 namwambia hivi kesho kutwa aende NMB au CRDB akawaambie Hu kasema kufungua akaunti ni bure, hakuna cha barua ya serikali ya mtaa wala nini! ni NIDA tu.
Mimi binafsi nilifungua akaunti hizo bure kabisa ila huwa napokelea mshahara kisha nakwangua wote nahamishia BANCABC.
Huko hakuna makato yoyote, ukiweka 10000 utaikuta 10000 yako mwezi ujao. Sio hizo njemba hapo juu uki-request statement hadi unajiuliza haya makato nimekatwa mimi kama nani?! kwa BANCABC kutoa hadi milioni makato hayazidi 2000 ukitolea kwenye ATM zao, ukitumia VISA makato ni 3000.
Huko EQUITY BANK nasikia nako kumenoga, hawana makato ya mwezi na pia hata kuangalia salio ni bure kabisa.
 
na je wana malipo ya online payments

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimependa umefikiria out side the box.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…