Kwanini ujenzi wa bwawa la umeme la Nyerere ni muhimu?

Kwanini ujenzi wa bwawa la umeme la Nyerere ni muhimu?

My county

Member
Joined
Aug 6, 2016
Posts
22
Reaction score
60
KWANINI MRADI WA UZALISHAJI UMEME WA MAJI BWAWA LA NYERERE MTO RUFIJI NI MUHIMU?

Mradi huu unatarajia kuzalisha megawati 2,115 za umeme hatua ambayo inaelezwa kwamba itasaidia kupunguza tatizo la nishati hiyo muhimu kiuchumi na kijamii hapa nchini. Wasomi wanaeleza kukamilika kwa mradi huu kutakuwa ni habari njema kwa sekta nyingi ikiwemo viwanda ambavyo wawekezaji wake wamekuwa wakilalamikia gharama kubwa za bei ya nishati ya umeme na ambao sio wa uhakika hali ambayo inapelekea kuwepo kwa gharama kubwa katika uzalishaji wa bidhaa hapa Tanzania ukilinganisha na bidhaa zinazotoka nje hivyo kushindwa katika ushindani wa soko.

Kwa sasa Tanzania inalipa dola za kimarekani senti 10.7 kwa uniti moja ya umeme kiasi ambacho ni kikubwa tofauti na nchi kama Misri inayolipa dola za kimarekani senti 4.6, Korea Kusini na China dola za kimarekani senti 8, Afrika Kusini dola za kimarekani senti 7.4, India dola za kimarekani senti 6.8, Ethiopia dola za kimarekani senti 2.4, Uingereza dola za kimarekani senti 0.15 na Marekani dola za kimarekani senti 0.12.

Kukamilika kwa mradi huu kutashusha bei za umeme hapa nchini kwa kati ya asilimia 35-40 hivyo kuchochea ukuaji wa uchumi na maendeleo ya wananchi kwa ujumla.


Gulatone Masiga.
masigag1987@gmail.com
images%20(19).jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi hamna majina mengine zaidi ya nyerere? Wale wazee walikuwa wanamsaidia kwa nini michango yao haienziwi? Ndio maana wanasahaulika sababu kila kitu ni nyerere... nahisi daraja la selander lile jipya nalo litaotwa nyerere. Inatika wakati hata kimuelewesha mtu iakuwa ngumu, daraja la nyerere, lipi? Unaanza elezea tena!
 
Mradi huu wa JNHPS ulipigwa vita saana wabunge na wasomi mbali mbalia nadhani kwa maslahi binafsi.

Ulipingwa hadi bungeni eti utaharibu mazingira, lakini utafiti uliofanywa na RUBADA pomoja na mashirika mengine yaliunga mkono mradi.

Ukosefu wa umeme wa uhakika ukalazimisha kuwa na miradi mingi iliyolitia taifa hasara kubwa saana.

Wazee hawakujali maana ni shamba la bibi, wakaleta maje nereta hadi ya ndege sijui symbion, Agreco, Songas na IPTL iliyochota ESCROW.

Tukaaminishwa kuwa hizo fedha sio za wananchi sijui ni za na ni?

Kwa hili la JNHPS utakuwa ni ukombozi kwa taifa kiuchumi na kimaendeleo. Ila
a wapigaji wote wapo tena wengine wapo bungeni wanatunga sheria.

Gari ni lile lile Isuzu bali limebadishwa rangi.

Mungu tuokoe Watanzania!!
 
Praise team mmeanza! Watu tuko bize na Corona nyie mnturudisha nyuma. Hv Stiglers na uhai wa watu bora nini? Tumechoka na misifa yenu,hebu tumsadie Rais kwanza kupambana na Covid-19 hayo ma Stiglers fanyeni km mna mute hv!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Praise team mmeanza! Watu tuko bize na Corona nyie mnturudisha nyuma. Hv Stiglers na uhai wa watu bora nini? Tumechoka na misifa yenu,hebu tumsadie Rais kwanza kupambana na Covid-19 hayo ma Stiglers fanyeni km mna mute hv!

Sent using Jamii Forums mobile app
Nani kasema hatuungi mkono mapambano ya Corona, tatizo lako umebeba roho ya kwanini serikali itekeleze mradi mkubwa kama huu!!!! Kazi inaendelea na tahadhari ya Covid-19 inafanyika pia
IMG-20200419-WA0007.jpg
HGK.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
KWANINI MRADI WA UZALISHAJI UMEME WA MAJI BWAWA LA NYERERE MTO RUFIJI NI MUHIMU?

Mradi huu unatarajia kuzalisha megawati 2,115 za umeme hatua ambayo inaelezwa kwamba itasaidia kupunguza tatizo la nishati hiyo muhimu kiuchumi na kijamii hapa nchini. Wasomi wanaeleza kukamilika kwa mradi huu kutakuwa ni habari njema kwa sekta nyingi ikiwemo viwanda ambavyo wawekezaji wake wamekuwa wakilalamikia gharama kubwa za bei ya nishati ya umeme na ambao sio wa uhakika hali ambayo inapelekea kuwepo kwa gharama kubwa katika uzalishaji wa bidhaa hapa Tanzania ukilinganisha na bidhaa zinazotoka nje hivyo kushindwa katika ushindani wa soko.


Kwa sasa Tanzania inalipa dola za kimarekani senti 10.7 kwa uniti moja ya umeme kiasi ambacho ni kikubwa tofauti na nchi kama Misri inayolipa dola za kimarekani senti 4.6, Korea Kusini na China dola za kimarekani senti 8, Afrika Kusini dola za kimarekani senti 7.4, India dola za kimarekani senti 6.8, Ethiopia dola za kimarekani senti 2.4, Uingereza dola za kimarekani senti 0.15 na Marekani dola za kimarekani senti 0.12.

Kukamilika kwa mradi huu kutashusha bei za umeme hapa nchini kwa kati ya asilimia 35-40 hivyo kuchochea ukuaji wa uchumi na maendeleo ya wananchi kwa ujumla.


Gulatone Masiga.
masigag1987@gmail.comView attachment 1422704

Sent using Jamii Forums mobile app
Mawazo tofauti.
Kwann tusiyaboreshe dams zilizopo tayari kwa kufunga mashine za kisasa pia kuondoa matope yaliyojaa kwenye dams zetu ili yazalishe umeme efficient pia kuokoa cost za kujenga new dam
 
Back
Top Bottom