Kwanini ukiota umekojoa kitandani unaamka umekojoa kweli?

Charles Gerald

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2016
Posts
1,403
Reaction score
1,837
Wakuu habarini tena,

Nataka kujua kwanini ukiaota umekojoa kitandani unaamka umekojoa kweli, wakati huo huo unaota umeokota pesa unaamka empty, umeokota dhahabu unakuta hamna kitu au umeoa kimwana unaamka na shuka tu.

Wajuzi wa ndoto hebu nisaidieni hiki kitendawili.
 
unajua kuota ni kuota tu, shida ni kwako kuifanya ndoto iwe kweli , ukiota una kojoa inakuwa ndoto ila mwili unaifanya iwe kweli sasa ukiota unaokota pesa ifanye iwe kweli pambana upate pesa kweli sawa mkuu
 
Sasa mkojo si upo ndani ya uwezo wako mjomba? Ndio maana ukiota na wenyewe una kutunuku
 
Sasa siku usiombe uote umeingiliwa.mjomba utakuwa umeingiliww kweli.
 
Sijasema nakojoa ila kuna dogo advance alikuwa na tabia ya kukojoa mkojo kitandani na anasema alikuwa ndotoni. Na watu wanasema ukiota unakojoa lazima uamke umekojoa kweli, ndio maana nimeuliza ni kweli?
 
Mi mbona huwa sikojoi kitandani niotapo nakojoa?
 
Sababu we ni kikojozi
 
Mkojo upo standby kwenye kibofu chako siyo wa kuutafuta ndiyo maana ukiota tu umetoka...


Pesa ni za kutafuta... Hujui kama kutafuta ni kugumu hata ndotoni..


Cc: mahondaw
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…