Kwanini ulijiunga JamiiForums na uliijulia wapi?

Mie nilikuwa nasikia kijiweni kila siku. Umeona alichoandika kule Jambo Forums yule Mzee ES? Nikiuliza washkaji wananitolea nje hawaniambii kitu wanasema we tinga jambo forums ukamsome Mzee ES. Ilikuwa inaniudhi sana mpaka nikahisi walikuwa wanaitangaza Jambo Forums. Basi siku moja nikatinga humu kuja kumsoma Mzee ES AKA Le Mutuz hahahahahaha lol! Basi nikawa natafuta kusoma posts za Le Mutuz tu lol! wakati ule alikuwa anashusha nondo zenye shibe basi nikajikuta nimelowea. Wakati ule wanachama hata 200 hawafiki akina dada hata 10 hawakufika. Basi kulikuwa na mkakati humu wa kuongeza idadi ya akina dada. Leo hii wamejaa tele toka wanachama mia na kitu sasa tunakimbizana na 400k si hapa hata kidogo.
 
Nami pia nulingia JF Oct 14.2011wakati siasa zimepamba moto chini ya Dr Slaa katibu chadema.
Nilivyoingia nikawa mwerevu wa kujua mambo na kuzungumza mbele za watu MAKINIKIA yote nilikuwa nayachukuqa huku JF watu kitaani wakawa wananielewa hatari mpaka wazee.

Almanusura nigombee udiwani!!!
JF is never boring..!

Sent from my TECNO-C5 using JamiiForums mobile app
 
Hii ni story ndefu mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaaaa kwahiyo saiv huwaogopi mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ha ha mkuu kwenye simu wewe ni kama Mimi dah nilikuwa natumia Nokia express music! Kipindi hiko majina ya JF yalikuwa yakunitesa haswa kuyakariri kumchwa.
Watu maarufu ni Rejao sijui yuko wapi siku hizi, Mingoi sijui ni mwamke? Alikuwa akikwaruzana na makamanda wakawa wanamwiita wewe mama mingoi nenda katumbuize twang a pepeta.

The Boss yupo mpaka Leo! Maalim @kanah bingwa wa kutukana Christian.
2013 .
@khaatan
Katavi
@nguruv3 makamanda ulingo wa siasa kutoka Arusha Arushaone Mungi Mungu akupe maisha mareeefu!! Wengine majina ya menitoka since 2012

Sent from my TECNO-C5 using JamiiForums mobile app
 
Kuna watu wana wivu sana mkuu yaan mtu unamuuliza haya mstory wayatoa wapi mtu hakwambii nilikuwaga nachukia kinoma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
...lakini nawashukuru maana nisingetinga humu. Na bila wao labda ingechukua miezi mingine michache au hata miaka michache kabla ya kuijua jamiiforums/jambo forums.

Kuna watu wana wivu sana mkuu yaan mtu unamuuliza haya mstory wayatoa wapi mtu hakwambii nilikuwaga nachukia kinoma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamii forum amekua rafiki kwangu wa mda wote,nakumbuka girlfriend mmoja ndo alikua na hii app akanimbia iko poa sana ndo kuidownload that was 2013.Hapa nikiwa na jina halisi.
Baada ya mda kuona watu wanatumia ID tofauti ikabidi nibadili i think 2015.
Napata raha sana kucheka peke yangu mda wote.

Sent from my SM-G925F using JamiiForums mobile app
 
Umenichekesha sana tu,eti watu wa jf ni wasomi saaana

ploudly ngosha [emoji243][emoji243][emoji243]
 
Reactions: BAK
Nilianza kuingia Jf mwaka 2011 nikajiunga rasmi 2014.Kilichonileta ni mada za kilimo na ufugaji.
 
Mimi ilikua mwaka 2008 kuna mshikaji wangu mmoja tulikua naye chuo akaenda UK kufanya masters,kwenye kuchart facebook ndio akanidokezea hii habari ya jamiiforum,wakati huo tunatumia PC tu,nilikua nalala saa 8 au 9 na kucheka pekeyangu usiku wa manane kama kichaa,wakati huo kulikua wachache naowakumbuka BUBU ATAKA KUSEMA,MASAMILO,ES (sauti ya umeme),NYANI NGABU,Alikuwepo FIDEL 08,pakajimmy,mariarosa

ploudly ngosha [emoji243][emoji243][emoji243]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…