Kusema Mungu hayupo kwa utafiti wa lisaa limoja umewaza tu na kukonclud kuwa hayupo ni kosa pia kukubali tu kuwa yupo bila we we mwenyewe kuona au kushudia matendobyake utakuwanafiki pia.
Watu wamafanya utafiti kwa zaid ya miaka elfu moja wewe unatumia lisaa utapata jibu LA uongo.
Ukweli ni kwamba kabla ya science tulikuwa tunaamini uwepo wa Mungu lakini baada ya kupata kaufahamu kidogo ambako hujiulizi kanatoka wapi ka kuchunguza mambo tunatoa kauli za ajabu na za kishenzi kusema hakuna Mungu.
Sisi ni nani, tumetoka wapi???? Ni baadhi tu ya maswali ambayo wanasayansi wameshindwa kuthibitisha ukweli halisi kwasababu kila dhana walioibua INA mapungudlfu mengi hivyo hazina ukweli wowote.
Mwanafizikia Isaac Feynman aliwa kusema Mungu ni jibu LA kila swali.....fikiria dhana yoyote ambayo haijajibiwa ndani ya biblia.
Kila tunachokiona na kukiwaza biblia ilishamaliza hilo huthibitisha kuwa Mungu ni zaid ya mile tunachowaza sisi.
Uovu ulitoka wapi uliza wanasayansi wakitoa jibu sahihi nijulishe.
Umetuelewesha vizuri
mkuu.
Hapa naona kama kuna kuna tatizo la Kitaaluma.
Baadhi ya watu wanamini sana utafiti uliofanywa na akina , Aristotor, Sharkesphere,
Socrates, Lenin, Abbott, Archimedes, Newtons nk, kama chanzo cha
maarifa sahihi.
Lakini bila kutoa sababu hawauamini utafiti ulipelekea kuandikwa kwa vitabu vya Torati ya Musa, Manabii, Zaburi ya Daudi, na Injili ya
Yesu Kristo,
Hawaviamini vitabu hivi licha ya ukweli kuwa mkusanyiko wake unaoitwa Biblia
Ndio unaosomwa na watu wengi zaidi duniani,
Ndio unaouza nakala nyingi zaidi duniani,
Ndio ulioandikwa kwa lugha nyingi zaidi kupita vitabu vyote vilivyowahi kuandikwa.
Wakati vitabu vya akina Lenin, vinapitwa na wakati na kuanza kusahaulika katika soko la vitabu duniani,
kitabu Cha biblia ndicho kinacho endelea kuwa na soko kubwa kadri siku zinavyoongezeka, kwa kuwa jinsi watu wanavyoongezeka duniani na ndivyo nakala zake zinavyozidi kuongezeka.
Jambo hili lina maanisha kuwa.
Waandishi wa vitabu vilivyo unda Biblia ndio waliofanya utafiti bora zaidi.
Maarifa yaliyoko katika Biblia ndiyo yanayoaminika zaidi na wasomi wa dunia hii.
Hekima iliyoko katika Biblia inahitajika zaidi na jamii ya sasa na inayokuja
Mafundisho ya kwenye Biblia yanategemewa na watu wengi zaidi kadri siku zinavyo ongezeka.
Watu walioandika Biblia wameuhakikishia ulimwengu kuwa kuna ukweli wa uhakika katika tafiti zao.
Elimu ya Biblia ambayo inatoa jibu la UWEPO WA MUNGU imekubalika na watu bila shinikizo lolote, maana watu wanaukubali ukweli huo kwa hiari yao.
KINACHO STAAJABISHA.
Utaona mtu wa kawaida kabisa.
Katika umri wake hajawahi kutoa hata chapisho moja la maarifa anaanza kuipinga Biblia.
Utafiti wowote unapingwa na utafiti mwingine.
Mtu anayepinga maarifa ya mtu wakati yeye hajawahi kuandika hata kitabu chenye kurasa mia na kikakubalika na jamii yake anaushangaza ulimwengu wa wasomi.
Ivi mwenzetu ulishamaliza hata shule ya msingi na ukaandika hata shairi lenye vina na mizani na likaimbwa na watu wanaokuzunguka ?
Kama sivyo au ndio, ni vipi unapinga toka hewani tu utafiti wa akina,
Musa, Prof of theology,
Daudi, Prof of Philosophy,
Suleimani, Prof Philosophy , na tajiri mkubwa katika historia ya dunia.
Luka, Dr of Medicine,
Paulo Dr of Law,
Yesu Kristo, The All Mighty God in human nature.
Kama kweli wewe ni msomi, ukisoma vitabu vya Social Science vya kitaaluma vyote vinawatambua hao wasomi na kuwakubali kuwa ni wana Falsafa waliobobea na kukubalika na mihimili ya Elimu.
Ambao wamefanya utafiti kwa muda wa mamilioni ya miaka na kuja na mafundisho ya Biblia.
Wewe mwenzetu ndo umemaliza chuo mwaka jana leo unawapinga bila utafiti wenye mashiko, hao wasomi wenzako wa kada mbalimbali waliokubalika na jamii zao kipindi chote hiki.
Eti hata ninyi mlioachishwa kazi na awamu ya tano kwa vyeti feki leo mna ujasiri wa kuwaita akina, Dr Paulo kuwa hawana wanachokijua
Unaishia kusema tu÷
"Mungu hayupo"
Huo ndio utafiti wako na unataka uaminiwe na jamii.
Kwanza inabidi mtupe CV zenu na marejeo ya machapisho yenu ili tujue mna kiwango gani cha elimu.
Kamwe haijawahi kutokea mtu mwenye elimu ya Ngumbaru akaugomea utafiti uliofanya kwa karne nyingi na jopo la wasomi.
Hao wasomi wamethibitisha katika utafiti wao kuwa
MUNGU YUPO
Basi na wewe kabla ya kutoa tamko la kupinga, tunauomba utuoneshe utafiti wako unaopinga uwepo wa MUNGU kwanza, ili sisi wasomi tukuelewe.
Kama hamna utafiti wowote basi ni busara zaidi kujifunza maarifa kwa hao wasomi waliotutangulia.
Au sivyo ?