Kwanini unapaswa kununua bond au Hati fungani ya NMB?

Kwanini unapaswa kununua bond au Hati fungani ya NMB?

Uzi ufufuke, mwenye kujua kuhusu bonds za CRDB tafadhali
 
Hat I TE="Bavaria, post: 16249485, member: 295384"]Unajua hati fungani ni nini hasa? Au unazijua tu hizi za NMB? Unajua zinavyonunuliwa? Unajua kwanini mabenki wanapigana vikumbo kununua hati fungani za serikali? Kuna watu wengi sana wamekuwa mabilionea kwa kununua hati fungani. Na hata nikikuambia huwezi kuwajua.

Kwa Tanzania;

1. Reginald Mengi, sio kwamba ananunua hati fungani za Tanzania tu, nchi nyingi nje ya Tanzania.

2. Ali Mufuruki,

3. Wengine hata nikikutajia huwezi kuwafahamu.
Hati fungani hizihizi za 13%[/QUOTE]Kwenye hicho kitabu, huyo Kiyosaki si anasema; Financial market is the playground of the rich?
 
Waliosoma vitabu vya Kayosaki hawajawahi kuwa mamilionea achilia mbali kufanikiwa.

Utaishia kuwa inspired tu.

Baada ya miaka mitano ujipime kama umetimiza vingapi kupitia stories za Kayosaki.
Hahahaa mkubwa, umewahi kuvisoma? Naam, miaka mitano hii, watupe mrejesho wa mafanikio hasa ya kifedha, na hatua walizopiga hadi sasa!
 
Ni mpaka uwe na mipango thabiti na uhakika wa kurudisha msingi na faida...wengi wamepoteza pesa nyingi kwa kufanya biashara na uwekezaji mwingine kisha wakaishia kutapeliwa kuibiwa au kupata hasara
Mkuu nimekupata ingawa muda umepita! Naomba kama una uelewa wa jinsi treasury bills zinavyouzwa na kununuliwa pale benki kuu unieleweshe mkuu. Nahitaji hii elimu mno
 
Hizo bond wanaweka watu wenye hela ngingi ambazo hawajui wazitumiaje.
Sasa ww na mshahara wako wa 1m unataka ukanunue bond?!.. utachekesha..
Kwani hela nyingi ni kuanzia shilingi ngapi?
Iko hivi, kwa nini Wabongo lukuki (pamoja na munyambugha) hawashiriki kwenye kumiliki hisa (shares) ni kutokupata elimu ya kutosha kuhusu hatifungani (bonds), Vipande (units) na hisa.
 
Kitabu cha "Cashflow quadrant" cha Robert Kiyosaki kinatuhusu sana hapa.

Jamaa anayaponda sana haya mabenki. Tabia ya mabenki ni kukopesha kwa riba kubwa lakini yenyewe yanauza hati fungani zao kwa riba ndogo sana. Lengo lao ni kupata faida kupitia hela ambayo hawajaifanyia kazi. Kwa kifupi, taasisi za kifedha si rafiki wa watu ila wapo kifaida.

Sasa hivi ni kweli mtu uweke mil 2 kwa mwaka halafu eti upewe 260,000 kama faida. Hivi hii inaingia akilini kweli?

Kutatua tatizo, Kiyosaki anashauri watu wawekeze muda wao kwenye Financial intelligence. Kila mtu akiwa na uelewa wa pesa atakuwa na jicho la tatu na kuona fursa zinazomzunguka na kuzifanyia
kazi kupata faida.

Fursa zipo nyingi sana. Tatizo ni kukosa macho ya kuziona. Kwa mfano mmoja tu: Kununua nafaka kipindi cha mavuno na kuziuza kipindi cha masika. Debe la mahindi kipindi cha mavuno maeneo ya Gairo huwa ni shs 7000. Lakini kipindi cha masika debe hilohilo hufika hadi shs 14,000. Kwahiyo ukiwa na mil 2 unanununua madebe 300. Baada ya miezi 5-6 unakuja kuyauza kwa shs 4000000. Ukitoa gharama za dawa na usafiri unabakiwa na 3.5 m. Unaweza kuona hapo profit margin.

Na huo ni mfano mmoja tu lakini kuna mifano lukuki ya aina hii. Tatizo kubwa tulilo nalo ni kutokuweka kipaumbele kwenye kuwekeza kwenye elimu ya fedha na biashara. Matokeo yake wanakuja hao watu wa NMB na kujifanya wanatupenda sana kiasi cha kutuhifadhia HELA ZETU ili zizae. Hawana upendo mkubwa kiasi hicho.

K
Biashara za matikiti na vitunguu Ruvu...
 
Back
Top Bottom