Kwanini uongozi wa Club ya Simba pamoja na TFF walishindwa kutuma salamu za pole kwa club ya Sevilla kufuatia kifo cha mchezaji Jose Antonio Reyes?

Kwanini uongozi wa Club ya Simba pamoja na TFF walishindwa kutuma salamu za pole kwa club ya Sevilla kufuatia kifo cha mchezaji Jose Antonio Reyes?

Infantry Soldier

JF-Expert Member
Joined
Feb 18, 2012
Posts
15,892
Reaction score
16,476
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums. Mimi mdogo wenu Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Leo swali langu lipo kama ifuatavyo;

Kwanini uongozi wa Club ya Simba ulishindwa kutuma salamu za pole kwa uongozi na mashabiki wa club ya Seville kufuatia kifo cha mchezaji Jose Antonio Reyes?

Nimeuliza hivi kwa maana kwamba Jose Antonio Reyes alifariki (tarehe 1 mwezi wa 6) ndani ya wiki moja tu baada ya mchezo wa kihistoria (tarehe 23 mwezi wa 5) baina ya Simba na Seville katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Angalia tarehe kwenye picha hapo chini.

IMG_20190921_103407_788.jpg


IMG_20190921_103323_913.jpg

Ikumbukwe ya kuwa Sevilla si sawa na akina Ruvu Shooting ama Ndanda FC. Ule mchezo umeifanya Simba pamoja na Taifa la Tanzania kutangazwa vema kimataifa.

Kitendo cha Club kubwa kama Sevilla kukubali kuja kucheza mechi katika nchi ya dunia ya tatu kama Tanzania ni suala la uungwana sana walitufanyia hawa wazungu lakini viongozi wetu wa kandanda mmeshindwa kuwaonesha uungwana huo Sevilla at least by sending your sincere condolences.

SIMBA NA TFF MMETUAIBISHA SANA KIMATAIFA KAMA NCHI.

OUR MOTTO: KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.

NB: NSSF NIPENI PESA ZANGU MTAANI MAISHA NI MAGUMU SANA. MUNGU ANAWAONA MJUE NYIE WATU?
 
Wewe unajuaje kama hawajawatumia salamu?
Orodhesha Salamu kutoka FIFA na Club zote walizocheza nazo.
Tatizo wajifanya mjuaji
 
Tatizo wajifanya mjuaji
Asante sana boss. Kejeli zako ndio chachu yangu ya kuzidi kuanika uzembe wa watu. Nimekusoma tabia zako kitambo sana. You'll never have me discouraged.
 
Wewe unajuaje kama hawajawatumia salamu?
Orodhesha Salamu kutoka FIFA na Club zote walizocheza nazo.
Tatizo wajifanya mjuaji
Simba ikicheza na Kagera Sugar si sawa na Simba kucheza na Seville. Ile ni heshima kubwa sana boss
 
Idara yao ya habari imeshindwa kufanya vizuri ktk Public Relations.
 
kuna mchezaji wa zamani wa mtibwa na azam amefariki mmeshatuma rambirambi?
Misiba yote inauma kwa viongozi pamoja na mashabiki wa mpira pasipo kujali ni mchezaji wa ulaya ama Africa.

Lakini Sevilla sio sawa na Azam wala Mtibwa.
 
Angekufa mchezaji wa simba alafu sevilla wasitume pole/rambi rambi ungesikia miafrika ingeloloma "hawa wazungu wabaguzi sana na wana roho mbaya"

Nachosema ni hivi; watume pole wasitume hawawapunguzii wala kuwaongezea sevilla kitu...


Wazee wa maslahi
 
Hao Mikia wamewahi kupata salamu zozote toka Sevilla? Au wao waanze kujipendekeza kwanza.
Tukio limetokea ndani ya wiki moja baada ya mchezo wa kihistoria. Kumbukumbu hisia za mchezo zilikuwa bado hazijafutika akilini mwa watu
 
Back
Top Bottom