Kubota
JF-Expert Member
- Oct 21, 2012
- 533
- 1,101
kwa sasa nchi nyingi hasa zilizoendelea zinafanya biashara na china. Na China wanalitambua hilo. Kuhusu bidhaa zilizo chini ya kiwango zinazoingizwa Tanzania na Nchi nyingine hiyo biashara inafanyika kwa usiri mkubwa. [kimagendo] na serikali ya China kwa sasa iko makini na hilo. Ikiwa watakamata bidha bandia na iliyo chini ya kiwango katika container lako hata kama ni kidogo mali yote inataifishwa na wewe utachukuliwa hatua kali. Nchi ya China kwa sasa wanafanya biashara za mabilioni ya dollar na wako makini na watu wachache wanaoharibu sifa yao.
Siyo sahihi ku-generalize ki hivyo, kuna wakati hata mimi nilitaka kujipa moyo kama ulivyoandika hapo juu! China wamekuwa wakifanya biashara na mataifa miaka mingi tangu enzi za Mwalimu. Sifa ya bidhaa za China kuwa ni dhaifu ni ya toka enzi za Mwalimu. Tunajua China inabidhaa nyingi za viwango vikubwa, lakini pia China ni nchi ya kuogopwa duniani kama ilivyo Nigeria! Wachina wanasifika kwa kufanya biashara haramu aina nyingi tu ikiwamo biashara ya bidhaa duni au feki!! Wanapata faida kubwa sana kwa vile wanatumia mali ghafi duni. Mimi nimeingiza mashine za shamba ambazo nimeuziwa na Wachina wenyewe kupitia Alibaba.com hakukuwa na magendo wala mkono wa Mtanzania, mashine zimegoma kufanya kazi vyuma vinakatika tu, nimewasiliana nao story zikaingia mwishowe wameingia mitini! Asikudanganye mtu fanyeni biashara na wachina at great care!! Kuweni macho na Wachina, hao ni monsters for ages na wanayaheshimu zaidi masoko ya nchi zilizoendelea siyo masoko ya Africa!!!! Usifikiri shehena kubwa hizo nchi yao haina taarifa, hakuna mataifa yenye mfumo mzuri wa ulinzi na udhibiti kama nchi hizo zilizoendelea. Nimeandika kama muathirika wa ujambazi wa wachina, wameshaingia Zambia wanazalisha kuku Broiler wanakua kwa kuumuka, wanatumia hormones kunenepesha kuku haraka, wanauza samaki waliozalishwa China kwenye mazingira duni sana, waliwahi kupata kashfa ya kuuza maziwa duniani yeye sumu ambayo kashfa ilitikisa dunia, acheni kuleta ujuaji kushabikia mambo mnayoyaelewa juu juu tu!!