Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Habari wakuu, nimeona leo tushee pamoja kuhusu muda wa mchakato wa ajira tokea kutanga nafasi hadi barua za kuita watu kazini

Kipengele (x) kinaongelea kutoa matokeo ya usahili wa mahojiano siku 30 baada ya kikao cha bodi.

Note; bodi ya utumishi huwa inakaa mara 4 kwa mwaka kama inavyoelezwa kwenye sheria za uendeshaji mchakato wa ajira


kitu kingine mchakato wa ajira unavyoendeshwa muajiri huwa anatoa muda ambao anawahitaji watu wake hivyo kinacho fanyika utumishi huwa wanafanya usaili mapema zaidi na kukaa na majina hadi bodi itakapo idhinisha.

Baada ya bodi kuidhinisha huwa wanawapangia watu vituo vya kazi pamoja na kuandaa barua.

Kuitwa kazini ni hadi pale ambapo muda ambo muajiri (taasisi) kuwahitaji watu wake umefika ndipo huandaa PDF la kuitwa kazini.

Walipata placemente wanaweza kutupa mrejesho zaidi kuhusu barua na muda barua zao zilisainiwa.

Thanks.

 
Sema nazo taasis zinazingua washajijua wanahitaj wafanyakazi,nafikir PSRS wangekua na order yao kwamb pale wanapotufanyish interview,waajir wachukue watu wao km ni mwez mmoja au miwili wawape muda maalum,kuliko kuacha watu miez na miez mpk muajir atakapojiskia,wakabaki na data base tu
 
Tusiwalaumu waajiri ....
CAG haya mapungufu ya wafanyakazi anayawasilisha serikari kuu...
shida ipo serikari kuu kutoa vibari ndo ukilitimba ulipo....
Sijui ndo Hao Mkuu wa Majeshi alisema kunawakimbizi sehemu nyeti za serikali!!Maana wasiokuwa na huruma na Vijana wao ...
Inakela sanaaaaa tuuuu na Kufikirisha sana...
 
Hizi ndo ajira zilizo semwa zitakuja kama 44000 😁😁?
 

Attachments

  • 3B51D3DE-A470-4788-BB92-8DF8013B2CCF.jpeg
    171 KB · Views: 10
  • 24B74E9C-6304-4C73-97D1-29A5AFE10016.jpeg
    169.6 KB · Views: 11
  • 9C4735E6-ECCC-4D9A-8539-DF3DDB3BA060.jpeg
    118 KB · Views: 10
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…