Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Kuna mtu alinambia MNH mishahara yao ni tofauti na hospitali zingine
Ndiyo, Ni tofauti, MNH hata NPHL pia Salary ni tofauti... Hata ukiangalia kwenye tangazo lao, hawajaweka salary scale.. Kiujumla tu ukipata pale umeula maisha..
 
We Acha tu 🤣🤣🤣
Ngumbaru wana midharau sana mitaani huku ,unaweza ukawa unawavunja mataya hawa washenzi kila siku kwa ngumi za uso
 
DAh kuna mwamba yeye kaenda leo kufuata barua anasema kapangiwa health centre labda kama ananipanga tu
Ina maana jina lake lilitoka chini ya wizara ya afya halafu akapangwa kituo cha afya au? Maana vitiuo vya afya vyote viko chini ya halmashauri (LGA), na post zilizotoka ni chini ya wizara ya afya (MDA). Hebu mwulizie vizuri tupate mwanga hapo! Maana kuna watu kibao bado wanasubiria halmashauri (LGA) ziteme!! Vinginevyo kama waajiriwa wa halmashauri majina yao yametoka kwa mwamvuli wa wizara ya fedha hapo watu waanze kuhesabu maumivu!
 
Anasema mwajiri ni wizara
 
IKo hivi huyu jamaa yeye ni laboratory technologist, anasema aliomba arusha na orala alifanyia uko ila kapangwa Uvinza Dc kigoma, nikamuhoji how comes umeitwa kwa mwajiri wizara na upangiwe kituo cha afya au halmashauri ,na je mwajiri katika barua yako ni nani, alijibu mwajiri ni wizara sasa sijajua kama yeye ndo anachanganya mafile hajuhi kwa kureport au ni vipi, make kuna jamaa zangu wengine wote barua iko dedicated kwa katibu mkuu wa wizara ya afya na vituo wengi wamepangiwa RRH na zile kama mirembe,mwananyamala ila ni mikoa ambayo hawakuomba( roundamly)
 
Muhimbili National Hospital (MNH) wametangaza kazi hizo hizo zilizokuwa zimetangazwa na MDA & LGA kwa kada za afya. Hii ina maana kuwa huko kwenye data base wamekomba na kumaliza kabisa hivyo kulazimika kutangaza tena. Kuna mtu alisema sehemu nyingi ya placement chini ya wizara ya afya zilikuwa kutoka database, ndio maana wamepangwa mikoa ambayo hawakuchagua. If that is the case tusubiri LGA (halmashauri) na zenyewe ziteme!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…