Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Nadhani lazima huwa wanakua na makubaliano kati ya psrs na taasisi na ndio maana psrs huwa wanasimamiwa hata kama hawahusika πŸ’―..na kama yapo kwa vyovyote wale waliwapa go ahead kwa sababu flaniflani na kwakujua pia kwamba wahusika wote wamepatikana na wamereport kazini uzende wa kuapload matokeo ukafanyika..
 
Vyuo vikuu vya umma hujipa u-special uliopitiliza hasa Chuo kikuu Dsm na washirika wake. Case kama hiyo ilitokea DUCE, kuna mdau alilalamika sana namna usaili wa written ulivoendeshwa na namna matokeo yalivotolewa kwa wahusika, ilikua mambo ya simu hayo hayo.

Hili la MUCE wote wa kulaumiwa, mara mia wangepost katika official website ya chuo, wahusika wakutane na matokeo huko. Hili la kupigiana sim huibua hisia za kukosekana kwa usawa katika ushindani na uwazi.
 
Sawa lakini tujiulize nani aliwapa barua za kuripot kazini hapo watumishi wapya je ni PSRS au MUCE alitoa moja kwa moja? Kama ni psrs basi taarifa wanayo nadhan waliofaulu walipopigiwa simu wakiambiwa wamefauku usaili hivyo wakachukue barua psrs ili waripot kwa mwajiri (muce)
 
Basi muce na duce kuna shida pale maana hata duce walipigiwa simu
 
Nadhani udsm na campus zake wanajionaga wao Wana uspecial fulani kumbe wanazingua hizi ishu zakupiga simu sio fair
 
Kweli mkuu, bora wangepost kwenye website then, PSRS waje wapost pia baadae kwa kuchelewa pasingekuwa na maswali mengi namna hii.

DUCE pamoja na kuwapigia simu ila walipost mapema kwenye website yao, then minong'ono ikabakia kwa process nzima jinsi ilivyofanyika.

Hawa MUCE wamezingua sana
 
Vyuo Vikuu vinaanzishwa kwa sheria, sheria husika ndo imevipa nguvu/hadhi ya kuwa mamlaka za ajira za watumishi wake, yaani wamepewa mamlaka ya kuendesha michakato ya ajira ya watumishi wake.

Ukiangalia saili nyingi za vyuo vikuu, PSRS imekuwa kama watch dog na kutumiwa kufanya shortlistings, tofauti kabisa na taaisi/instituties zingine ambazo PSRS huhusika moja kwa moja.

Nini kifanyike? Ni ukweli usiopingika kwamba PSPRS ukiacha mapungufu yake madogomadogo ni taasisi inayoaminiaka sana hasa na jobless na umma wa watanzania kwa ujumla, BUnge (Mbunge wako) ndo chombo pekee kinachoweza kufanya mabadiliko ya sheria zilizoanzisha vyuo vikuu na ile iliyoanzisha PSPRS ili kuhamishia majukumu hayo PSRS na kuifanya kuwa chombo pekee kinachosimamamia na kuendesha michakako ya kuajiri kwenye utumishi wa umma na kuwaongozea bajeti hasa ya rasilimali watu, ili michakato yake ifanyike kwa muda unaotajwa kwenye mkataba wa PSRS na wateja wake.
 
Hizi taasisi za Vyuo vikuu nimeona barua wanazichukua moja kwa moja kwa mwajiri.

Niliona Mzumbe, ARU, DUCE, SUA, MUHAS,MUST walielekeza watu wakachukue barua moja kwa moja vyuoni then ndio wakakamilishe taratibu za ajira.

Sasa kwa kuwa hivi vyuo vinapewa mamlaka ya kuendesha sahili zikiwa chini ya PSRS mwanzo mwisho na wakitaka kutangaza/kuita matokeo/kazini inabidi watoe nakala kwa PSRS ili nao watangaze kwa Umma, lakini MUCE hawakufanya hivi badala yake wakaita watu kwa simu na kutopeleka matokeo PSRS kwa wakati.
 
Umeeleweka kiongozi ngoja nikagombee ubunge sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…