Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]

Kuna kaukweli hapa

Hahaha! Mkuu, mtamfanya jamaa aanze kuidharau kazi mapema kumbe kuna uwezekano yeye akaenda kuwa wa tofauti na waliopo.

Miaka ya nyuma wakati niko kwenye hustle kali, niliwahi kuitwa kwenye usaili fulani, na kweli nikaona uelekeo wa kufanya vizuri ni mkubwa sana.

Kilichonivunja moyo ni namna Hr anavaa mavazi ya yamechoka, na kibaya zaidi tulibadilishana namba nikashangaa naingia Whatsapp haujapita muda mrefu nikakuta amepost picha za vyumba vingi, kumbe anapiga na mishe mishe ya udalali wa vyumba.

Duh! Nikawapotezea sijarudi tena hata waliponiita.
 
πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€ hata mimi nina tabia hyo nikienda interview nikione furniture hata ofisi yenyewe haieleweki unaon hapa hmna jambo hapo
 

Asante sana Mkuu, nimekupata. Vipi au labda kwa upande wa kada za Sayansi kuna uwezekano sana kukutana na vitu vya darasani moja kwa moja ambavyo endapo ulibahatisha ukapitia inawezekana ukafanya vizuri?

Naona pia kama hawa wa masuala ya fedha kuna namna inabidi pia apambane na vitu vya nje ya darasani, kitu ambacho ni bahati nasibu sana, kwa mfano watu walileta maswali ya usaili wa Bunge, ile ilikuwa ni hatari sio usaili.

Au unaonaje mkuu?
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]hahhhh Kaka mfanyakazi mwenzetu alikuwa anafunga ndoa

Hahaha! Sawa Mkuu, naona kumbe ujobless bado unaumudu vizuri, mpaka kazi unayo, acha utumishi wakusubirishe kidogo, waanze na ambao kukicha hawajui pakwenda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…