Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Kutokana na makato ya namna hii, take home inabaki kuwa ya ugali tu, kuhusu maendeleo lazima tujiongeze kwa namna nyingine

Hahahahaaah! Na ndipo linapokuja suala la utekelezaji wa agizo la muheshimiwa Rais la tule kwa urefu wa kamba zetu.

Sasa kama ajira utakayopata au uliyonayo haina kamba au kamba yake ni fupi sana, ndipo mtu unakuta anakata kamba kabisa au ananunua ya kichina inayovutika sana japo ni fupi kwa muonekano.

NB: Ukifoji ukatumia kamba inayovutika ikikatika bahati mbaya ni lazima ikuchape mpaka uzimie kama ilivyomtokea Shujaa wetu Majaliwa wa Precision Air.

Suala la kukata kamba ni kuacha kazi, ndugu zangu hili sishauri hata upate kazi yenye magumu kiasi gani, motivational speakers wasikudanganye ukaacha kazi kabla haujajipanga.

Pamoja na ugumu uliopo lakini Serikali bado inapaswa kupambana kuongeza uwezo wa kuajiri na kuzifanya sekta binafsi zitanuke kumudu kuajiri zaidi huku wakiendelea kuboresha masilahi ya waajiriwa hasa kwa taaluma zinazohitaji nguvu kazi kubwa.

(Lengo ni tutabasamu kidogo lakini kuna ujumbe hapa).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…