Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Jamaa kuna tangazo la Nafasi za kazi lilitoka mwezi May mwaka 2022. ***** ni mpaka leo kimya
 

Sawa Professor, naamini pia unajiamini kwa kuwa huwa unatoa michango isiyohitaji sana kujificha.

Maana kwa mtu aliyeshusha visa vya kutosha kwenye uzi wa rikiboy halafu siku majina yake halisi yakijulikana kupitia placements nadhani kidogo kuna ukakasi.
 

Duh! Mkuu umesomea nini kwa mfano?

Masuala ya mapishi au?

Navuta picha ni kozi gani hizo, naona haiji.

Au uendelee kuvuta subira, watawaita tu. Kwa sababu kwa uzoefu mfumo wa ajira portal umeundwa kwa kujumuisha vyuo vyote vinavyotambulika pamoja na kozi zinazotolewa kwenye hivyo vyuo.
 
Kaka pamoja na yote namshukuru Mungu nimetoboa kuingia oral Mungu amekua upande wangu.
 
Kozi gan izo mkuu ambazo hazieleweki?
 
Kwenye uzi wa kimasihara sijawahi kuchangia kwa kutoa kisa kwani sina hicho kisa zaidi tu nilikuwa nachangia kufurahishwa na hivyo visa.

Nina muda mrefu sana sijatia mguu kwenye ule uzi pamoja na kuoona ukiwa unatrend mara kwa mara
 
Kaka pamoja na yote namshukuru Mungu nimetoboa kuingia oral Mungu amekua upande wangu.
Kumbe ulikuwa bado unasubiri majibu na ule mrejesho!? nilidhani tayari majibu yashatoka na ukakandwa.

Hongera sana, green light ndio hiyo, imebaki juhudi za mwisho sasa kukamilisha mission.

Oral mumeitwa wangapi na mnapambania nafasi ngapi?
 
Kwenye uzi wa kimasihara sijawahi kuchangia kwa kutoa kisa kwani sina hicho kisa zaidi tu nilikuwa nachangia kufurahishwa na hivyo visa.

Nina muda mrefu sana sijatia mguu kwenye ule uzi pamoja na kuoona ukiwa unatrend mara kwa mara
Mimi ni mdau mkubwa kule kwa kijana wetu wa hovyo rikiboy ingawa ni kama mpenzi msomaji. Although siku hizi hauna visa zaidi ya kua kijiwe cha kupiga soga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…