Kwanini vijana tunakufa Sana siku hizi?

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
21,643
Reaction score
51,642
Mpaka wazee wanashangaa Mambo haya hayakuwepo wakati wa miaka ya nyuma.nini sababu tufanyaje ili tuishi kwingi na sisi tuone mengi?maana bongo kuna Mambo mengi Muda mchache mchache ukifa inauma Sana kukosa stori zinazoendelea.tunatamani tuishi angalau tuone haya maajabu yajayo yanafurahisha.mwezi huu TU wamekufa watu ninaowajua zaidi ya kumi na vijana ndio wengi haswa.kuna Nini?
 
mbona wewe upo?Mshukuru Mungu kwa uhai ulio nao
Alafu punguza ukali wa maneno..wanafariki.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mshahara wa dhambi ni mauti.
 
Kujitunza,(Kiutamaduni,kijamii, kiafya na kimaadili) imekuwa ngumu.Mambo mengi tumeyavamia,na tumepitiliza sio kwa wanaume hata wanawake!
 
Mmomonyoko wa maadili. Hakuna kukemea maadili mabovu. Amber lulu na wengine wanakuwa maarufu kwa kufanya ngono na kuzisambaza ktk mitandao.
Michepuko inafika wakati ni kitu cha kawaida.
Sababu kubwa ya hivi vifo ni ngono na mtindo maisha wa sasa.
 
Dah...Bosi..maswali mengine kabla ya kuyaibua yanataka utafiti....unawajua wazee wangapi?...vijana wangapi? na huko nyuma kulikuwa na takwimu gani za vifo? nk nk.nk...kujua kwako vijana 10 waotutoka mwezi huu bado haihitimishi kufa kwa vijana zaidi ya wazee [emoji41]

Sent using Beretta ARX 160
 
Baadae watasema uliaga kiaina na wewe
Ooh alijua kifo chake

All in all vijana wa siku wanakufa bado wakiwa wadogo kwa sababu nyingi tu
Moja wapo ni vyakula na lingine ni madawa ikifuatiwa na ukiherehere wa kuamini kila kitu kinaongeza nguvu za kiume
Wazee hawa unaowaona ujana wao walikuwa na nguvu bila kutumia madawa
Leo kijana mdogo anatumia viagra hadi unawahurumia
Halafu moyo ukisimama ghafla mnaanza ooh ngoma

Mbona wanawake hawafi hivyo kama takwimu za wanaume wakati wao ni wengi zaidi?


Sent from my SM-G570F using Tapatalk
 
Science & technology (GLOBALIZATION)

A Philanthropist&£conomist.
 
mungu ndio mjuzi binadamu hana jibu sahihi


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…