Kwanini wachezaji wa Tanzania wanawahi kuchoka mapema sana?

jf user

JF-Expert Member
Joined
Aug 22, 2018
Posts
777
Reaction score
623
Huwa najiuliza sana na kukwazika pale ninapoona wachezaji vijana wa Tanzania vijana kabisa damu inachemka wanastaafu wakifikisha miaka 30!
Sijui tatizo ni nini ila ningetegemea wakipige mpaka 38-40 ndio wastaafu.
Tatizo ni nini hasa?
Watu kama kaseja, musa hassan mgosi na wengineo walistaafu na 30!
Afadhali canavaro kakipiga mpaka 37 au 38 ndipo akatundika daluga.
Kwa namna hii kuna ulazima wa mastaa wetu wajiangalie kwa kweli kwani hawatupi burudani tunayoipenda.
Kwa waliozaliwa 1985 ni mapema mno kustaafu,

 
Sio wachezaji wabongo karibu wote tunawahi kuchoka
Wabongo wanakua mdebwedo kwenye 30 wakati wazungu na south America wanakipiga mpaka 38-40?
At least nchi za west Africa kama ivory coast, Nigeria, Ghana, Senegal, na north africa kama Egypt, morocco, Algeria wako vizuri sana.
Wale ni qualified players unlike tz.
 
Unajua kilo anazoshishia drogba wewe?

Labda ungesema mlo mbovu ningekuelewa.
Mchezaji huwezi shindia chipsi utegemee kufanya makubwa uwanjani.

Drogba atakuwa amefanana na weupe katika mlo...wenzetu hawali vitu vigumu kama vile ugali na viazi,,, wenzetu wanakula vitu laini laini na mazoezi kwa wingi. Ni hilo tu mkuu,, sisi huku tunashindia ugali na chips mayai yenye mafuta mengi wapi mwili utapata afya babaa
 

Umeongea ukweli...
 
Wachezaji wengi wa Tanzania wanadanganya umri. Utakuta mtu tayari ana miaka 25 lakini atadanganya ana miaka 17 hapo tayari amejichota miaka nane.

Hii hata mimi imeshanitokea kipindi fulani cha nyuma kwenye michuano ya Copa Coca-cola Arusha ilibidi tufoji miaka ili tuweze kuahiriki. Hata ile ya Airtel Rising Star nayo tulifanya hivyo hivyo.

Unakuta kwenye team nzima waliopo kihalali sio zaidi ya watato wengine wote tumefoji umri. Sasa kwa wale wenzetu waliofanikiwa kuendelea pamoha na kutengeneza vyeti vya kuzaliwa vyenye taarifa za kufoji ndio hao ambao huishia kuchoka mapema kabisa.

Utashangaa mchezaji kama Okwi pale simba unaambiwa ana miaka 25 sasa hivi. Ni maajabu kwa kweli.

Ulizia umri wa Ngassa ucheke. Wachezaji wa kibongo kufoji umri ndio kitu kinacho waumbua na kuonekana wanachoka mapema ila sio kwamba wanachoka mapema bali ndio mda sahahi umefika.

Akili inataka mwili unagoma.
 
Unataka unaiambie benchi la ufundi huwa hawaambii namna ya kujenga mwili pamoja na vyakula wanavyopaswa wale "Diet"?
Vipi daktari wa timu?
Halafu mtu kama mimi nisingeshindwa kujiandalia misosi yangu ya maana kulingana na kazi yangu uwanjani.
Hata wewe hapo mkuu naamni hauli hovyo sasa mbona wachezaji hawafanyi hivyo?
 
Hahaha mkuu ni kweli kabisa nakubaliana na wewe kuhusu swala la umri.
Kwa mfano okwi mwaka 2012 nilisikia kazaliwa kati ya 88 au 89 leo anasema kazaliwa 92? hahahah uongo mkubwa sana huo kwanza ukimuangalia hata mwili wake ni mtu anaegongwa 30 sio chini ya hapo.

Ngasa kazaliwa 89 sawa na tegete.
Mgosi, henry joseph na kaseja ni 85 hapo sioni shida.
Canavaro kazaliwa 80 hapa hamna tatizo.

Okwi msanii sana ila ataweza umbuka siku moja kwa sabt tupo ulimwengu wa kidigitali.
 
Uzuri kinachombeba ni kiwango. Hajawahi kuchuja hivyo haleti sintofahamu sana kwa mashabiki.
 
Umeniibia idea yangu

Hahahaa just kidding, Ila umemaliza Mzee baba
 
Mi bado si mwelewi yule Diego Costa, hakuna uwiano wa sura na umri wake! Kwa bongo hii George Kavila na Shabani Nditi wamedumu vya kutosha katika soka
 
Kuna mtu anaitwa SHABAN NDITI!
Alianza kuichezea MTIBWA SUGAR 2002 ma ilipofika 2006 akaenda SIMBA! Akacheza kwa misimu miwili tu, akarudi zake MTIBWA na mpaka leo bado anacheza! Aliwahi kuchezea TAIFA STARS ya Marcio Maximo kabla hajaomba mwenyewe Kuachwa! Kwa ufupi ni kwamba, Shaban Nditi amekuwepo Ktk TPL kwa miaka 16 mfululizo na sasa ana miaka 35 kwa mujibu wa passport ya kusafiria!

Next time nitamzungumzia Juma Kaseja Juma!
 
Wanatoka kimpira na miaka 32 alafu wana edit kuchoka lazima tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…