Kwanini wakala wa Tigo Pesa, M-pesa, Airtel Money hawataki pesa itolewe na mtu wa mbali?

Kwanini wakala wa Tigo Pesa, M-pesa, Airtel Money hawataki pesa itolewe na mtu wa mbali?

Do santos

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2011
Posts
635
Reaction score
338
Tangu ongezeko la tozo kwa mitandao ya simu, mawakala wengi hususani Tigo Pesa na M Pesa wamekua wakigoma mtu kutoa pesa akiwa nje ya eneo la ofisi zao.

Jamaa yangu alikua anataka kunitumia pesa akashauri niende kwa wakala ili atoe hapo na nichukue pesa.

Wakala akakataa kwa hoja mtoaji yupo mkoa mwingine hivyo atapata kiasi kidogo sana. Ikabidi jamaa anitumie kwenye simu yangu ili nitoe.

Lakini leo kuna mtu nimemtuma kitu na akapungukiwa pesa nikaamua aende kwa wakala wa Tigo pesa ili nitoe pesa achukulie hapo lakini takribani wakala wote wamekataa wakimwambia atumiwe pesa na atoe yeye.

Nipo Mkoa mmoja na ninayetaka achukue pesa. Hivyo hoja ya kuwa mkoa mwingine haikuwepo.

Sijajua kwa nini wamekataa. Suala la miamala ya simu imekua na changamoto nyingi kwa sasa

Mwenye kujua atujuze.
 
Pia kuna wengine wanakataa kutuma pesa kwa mtu tofauti na aliyepo dukani kwake. Ukiiuliza wanasema wao wanalipwa commision kulingana na eneo lake la kazi . Minara inafatilia transaction zote so zile zilizo mkoani/ umbali fulani ndio iko na commission
 
Pia kuna wengine wanakataa kutuma pesa kwa mtu tofauti na aliyepo dukani kwake. Ukiiuliza wanasema wao wanalipwa commision kulingana na eneo lake la kazi . Minara inafatilia transaction zote so zile zilizo mkoani/ umbali fulani ndio iko na commission
Basi kama ndio hivyo basi Tena

MI naenda nakwambia naomba kuweka sisem kutuma.

Kuusu ilo jambo LA kukaataa kutoa ukiwa mbali lipo hivyo cha msingi ukitaka kufanikiwa usimwambie kama anae Toa yupo mbali aakitoa tuu jamaa a nakupa chako una sepa
 
Hebu Soma Terms and Condition
1637233261106.png

Kipengele cha pili Kinamtaka Mtoaji na Muwekaji Fedha kwa wakala kuonyesha KItambulisho Chake. Sasa Wakala uko naye Mwanza unataka mtu wa Dar atoe Hela, hicho kitambulisho atakionaje?
 
Tangu ongezeko la tozo kwa mitandao ya simu, mawakala wengi hususani Tigo Pesa na M Pesa wamekua wakigoma mtu kutoa pesa akiwa nje ya eneo la ofisi zao.
Kwahiyo mkuu kulikuwa na ulazima gani wa kumtaarifu wakala kuwa unaetoa sio wewe??
Ungemuuliza tu kama unaweza kutoa kiasi flani akikubali unamtext jamaa yako anatoa we unachukua cash
 
Tangu ongezeko la tozo kwa mitandao ya simu, mawakala wengi hususani Tigo Pesa na M Pesa wamekua wakigoma mtu kutoa pesa akiwa nje ya eneo la ofisi zao.

Jamaa yangu alikua anataka kunitumia pesa akashauri niende kwa wakala ili atoe hapo na nichukue pesa.
Hiyo miamala ya mbali hailipwi commission
 
Wapo wanaokataa hata kumwekea mtu aliyeko mkoa mwingine, wapo wanaokubali kutoa hata kama uko mkoa mwingine. Voda wangetwambia kanununi ni ipi
Inategemea na wakala uliye naye kuna mawakala wengine transaction zao ni ndogo hvyo, ukiwa unamtuma pesa kwa mtu wa mbali amakutoa, kamission inakuwa ndogo
 
Sababu ni kuogopa kutapeliwa matapeli wanatumia njia hii sana kutupiga Mawakala pia muamala wa mbali haina faida
Siyo kweli, kuna sababu za kimahesabu, na muongozo wa mawakala waliopewa na kampuni za simu ndio huo.

Ila mawakala wenye utu huwa hawana tatizo na hilo unaweza kupokea ela kutoka mbali direct kwa wakala.

Kwa mfano wewe upo Dar unataka kutuma pesa kijijini na hauna salio kwenye simu, unaweza kumpa wakala Dar akatuma kwa wakala kijijini mtu anapewa cash kule, lakini muongozo wa makampuni ya simu hawataki transaction zifanyike hivi ili wawapige vizuri wanyonge hawa.

Tukumbuke si kila mtu anayemiliki simu, kwahiyo hata asiyemiliki simu ana haki na anastahili kupata huduma za kifedha kupitia kwa mawakala kutuma na kupokea.
 
Basi kama ndio hivyo basi Tena

MI naenda nakwambia naomba kuweka sisem kutuma.


Kuusu ilo jambo LA kukaataa kutoa ukiwa mbali lipo hivyo cha msingi ukitaka kufanikiwa usimwambie kama anae Toa yupo mbali aakitoa tuu jamaa a nakupa chako una sepa
Kama mtu anayekufahamu anaweza kutuma kutoka kwa wakala kwenda kwa wakala bila shida.

Tatizo nchi ngumu hii imekaa kiconnection tu kila kitu kujuwana.
 
Siyo kweli, kuna sababu za kimahesabu, na muongozo wa mawakala waliopewa na kampuni za simu ndio huo.

Ila mawakala wenye utu huwa hawana tatizo na hilo unaweza kupokea ela kutoka mbali direct kwa wakala.

Kwa mfano wewe upo Dar unataka kutuma pesa kijijini na hauna salio kwenye simu, unaweza kumpa wakala Dar akatuma kwa wakala kijijini mtu anapewa cash kule, lakini muongozo wa makampuni ya simu hawataki transaction zifanyike hivi ili wawapige vizuri wanyonge hawa.

Tukumbuke si kila mtu anayemiliki simu, kwahiyo hata asiyemiliki simu ana haki na anastahili kupata huduma za kifedha kupitia kwa mawakala kutuma na kupokea.
Mkuu Wewe ni wakala au unataka ligi,Mimi ni wakala na nimeandika uhalisia
 
Back
Top Bottom