Kwanini walinda mlango weusi sio wengi ligi za ulaya?

Kwanini walinda mlango weusi sio wengi ligi za ulaya?

Sababu kubwa ni nafasi ya goalkeeper ni chache hivyo timu inakua na goalkeeping wawili hivyo nafasi inakua chache na watu wengi kutoipenda. Ingekua timu inakua na wachezaji wengi kwenye hiyo nafasi...weusi wangekua wengi sana.
 
Nakumbuka enzi za utoto matipwatipwa ndo walikuwa wanakaa golini[emoji3][emoji3]. Anyway, sehemu ya goalkeeping ni nafasi nyeti sana inahitaji mtu anayeaminika, pengine wazungu bado hawatuamini watu weusi. Pia umesahau kuuliza kuhusu makocha, ni nadra pia kuona makocha weusi kwenye ligi kubwa barani Ulaya
Kwenye suala la makocha weusi pia kuna tatizo.

Paul Ince aliwahi kupewa timu ya Blackburn Rovers ikiwa ligi kuu ya Uingereza akaishusha daraja.

Hata hapa Afrika, klabu nyingi kubwa zinafundishwa na weupe, ina maana tatizo linaanzia kwanza kwetu wenyewe!
 
Kwenye suala la makocha weusi pia kuna tatizo.

Paul Ince aliwahi kupewa timu ya Blackburn Rovers ikiwa ligi kuu ya Uingereza akaishusha daraja.

Hata hapa Afrika, klabu nyingi kubwa zinafundishwa na weupe, ina maana tatizo linaanzia kwanza kwetu wenyewe!
Hahaha hapa nadhani umemaliza kila kitu, hao makocha weusi tuu hata sisi hatuwaamini ije kuaminiwa kwa wazungu big NO!
 
Sababu kubwa ni nafasi ya goalkeeper ni chache hivyo timu inakua na goalkeeping wawili hivyo nafasi inakua chache na watu wengi kutoipenda. Ingekua timu inakua na wachezaji wengi kwenye hiyo nafasi...weusi wangekua wengi sana.
No way....
 
Kwa muda mrefu Afrika imekuwa ikitoa viungo, washambuliaji na mabeki wazuri wanaotamba kwenye ligi mbalimbali barani ulaya. Toka enzi za akina George Weah, Samuel Etoo, Jayjay Okocha, Michael Essien, Yaya Toure nk.

Lakini habari ni tofauti kwa makipa, idadi ya magolikipa ni ndogo sana barani ulaya hasa katika ligi kubwa. Je magolikipa hao hawana uwezo mbele ya wazungu wanaotamba kama vile akina De Gea, Alisson Becker, Jan Oblak na wengineo.

Golikipa pekee mweusi kutoka barani Afrika anayetamba kwasasa katika ligi kubwa za ulaya ni Andre Onana wa Ajax.

Je, tatizo ni nini?

Makipa weusi huko nyuma walipata kung’ara ingawa hawakuwa wengi
Tomas Nkono (ambae ndio idol wa Buffon)
Jacques Songoo
Peter Rufai
Idris Kamen
 
Kwa muda mrefu Afrika imekuwa ikitoa viungo, washambuliaji na mabeki wazuri wanaotamba kwenye ligi mbalimbali barani ulaya. Toka enzi za akina George Weah, Samuel Etoo, Jayjay Okocha, Michael Essien, Yaya Toure nk.

Lakini habari ni tofauti kwa makipa, idadi ya magolikipa ni ndogo sana barani ulaya hasa katika ligi kubwa. Je magolikipa hao hawana uwezo mbele ya wazungu wanaotamba kama vile akina De Gea, Alisson Becker, Jan Oblak na wengineo.

Golikipa pekee mweusi kutoka barani Afrika anayetamba kwasasa katika ligi kubwa za ulaya ni Andre Onana wa Ajax.

Je, tatizo ni nini?
kuna namba ambazo zinahitaji sana kutumia akili ikiwemo kipa na wazungu wanaamini kwamba mtu mweusi hana akili,that's a reason!
 
Makipa weusi huko nyuma walipata kung’ara ingawa hawakuwa wengi
Tomas Nkono (ambae ndio idol wa Buffon)
Jacques Songoo
Peter Rufai
Idris Kamen
Goalkeeping kwenye modern football inahitaji skills zaidi tofauti na zamani talent tu ilikua inatosha kuwa goalkeeper mzuri
 
Kwa muda mrefu Afrika imekuwa ikitoa viungo, washambuliaji na mabeki wazuri wanaotamba kwenye ligi mbalimbali barani ulaya. Toka enzi za akina George Weah, Samuel Etoo, Jayjay Okocha, Michael Essien, Yaya Toure nk.

Lakini habari ni tofauti kwa makipa, idadi ya magolikipa ni ndogo sana barani ulaya hasa katika ligi kubwa. Je magolikipa hao hawana uwezo mbele ya wazungu wanaotamba kama vile akina De Gea, Alisson Becker, Jan Oblak na wengineo.

Golikipa pekee mweusi kutoka barani Afrika anayetamba kwasasa katika ligi kubwa za ulaya ni Andre Onana wa Ajax.

Je, tatizo ni nini?
Soon Air Manula, aka Aishi Manula wa Mo Fc atatamba Ulaya
 
Wazungu wanataka goalkeeper sio walinda mlango
 
Back
Top Bottom