Kwanini wanaotoa ushuhuda makanisani huwa hawachukuliwi hatua za kisheria?

Kwanini wanaotoa ushuhuda makanisani huwa hawachukuliwi hatua za kisheria?

Moja kwa moja....

Nilimsikia mama mmoja anasema katika ulimwengu wa roho amechinja wachawi karibu mia, alipewa upanga na malaika. Sasa watu mia kuchinjwa rohoni ni upotevu mkubwa wa nguvu kazi.

Mwingine unamsikia anasema walikuwa wachawi, wanasababisha ajali, wanakinga damu. Wanajinadi kuwa wameua watu wengi. Hii ni kama Genocide ukijumlisha mauaji hayo ya ajali zetu kwa mwaka.

Mwingine alienda mbali eti hadi Hayati Mkapa alipopata ajali akiwa kwake Ikulu yeye na team ya wachawi walikuwa wanapambana naye. Hii sio ajabu maana Ikulu hadi Brazili na Malawi tulishasikia hayo ya watu kupigwa kishirikina hadi kukimbia Ikulu.

Hapo achilia mbali majambazi, wauwaji na watenda maovu ya kutisha wanapotoa shuhuda zao live tena kwa kushangiliwa na hatuoni wanapelekwa Jela kutumikia kifu go cha uharifu huo wakati hawajamjua Bwana Yesu.

Najiuliza kama mtumishi

Huwa tunapangwa tu na Serikali huwa inajua na kuamua kupotezea?

Hakuna ushahidi wa kisheria kuwachukulia hatua kwenye mambo ya kiimani?

Au Serikali inatambua makanisa ni chombo saidizi cha kubadili mienendo ya jamii hivyo wanasaidiwa kazi na wachungaji

Wakuu kitaalam hii imekaaje. Au wewe ulishawahi kusikia shuhuda gani za kutisha hadi ukageuka kuona kama kuna Polisi anasikia?
Ndugu m2mishi,serikali inaelewa umuhimu wa haya makanisa kwani ni moja wapo ya kazi za makanisa haya ni kama therapy kwa wenye matatizo ya akili,,,wengi wa wanaoenda kwenye makanisa haya wana matatizo ya akili kutokana na msongo mkali wa maisha,maradhi sugu,kutopata watoto,matatizo ya ya makazini,n.k,,,,so sio wote wanaosema wamepewa upanga ni kweli{nani kamwona malaika?] si unamkumbuka MALKIA ZAMURADI alisema yeye ni MUNGU? na akasema alienda mpaka mbinguni na kuna magorofa marefu na akapiga story na YESU??{sasa utasema huyu ni mzima kweli????],,,,matokeo yake waumini wake wakaamini na kuanza kumwabudu mpaka wakawa kama mataaira na hapo TISS wakaingia kazini kwani wangechelewa tu yangetokea kama yale ya kenya ya msitu wa shakahoza{wa2 walifunga mpaka kufa ili waende MBINGUNI!!!,,,,so sio kwamba serikali inaacha,no wanawachunguza kwa kuchomeka wa2 wao kujifanya nao ni walokole,ila wakiona dalili za hatri ndo wanaingilia kati!!
 
Ndugu m2mishi,serikali inaelewa umuhimu wa haya makanisa kwani ni moja wapo ya kazi za makanisa haya ni kama therapy kwa wenye matatizo ya akili,,,wengi wa wanaoenda kwenye makanisa haya wana matatizo ya akili kutokana na msongo mkali wa maisha,maradhi sugu,kutopata watoto,matatizo ya ya makazini,n.k,,,,so sio wote wanaosema wamepewa upanga ni kweli{nani kamwona malaika?] si unamkumbuka MALKIA ZAMURADI alisema yeye ni MUNGU? na akasema alienda mpaka mbinguni na magorofa marefu na akapiga story na YESU??{sasa utasema huyu ni mzima kweli????,,,,matokeo yake waumini wake wakaamini na kuanza kumwabudu mpaka wakawa kama mataaira na hapo TISS wakaingia kazini kwani wangechelewa tu yangetokea kama yale ya kenya ya msitu wa shakahoza{wa2 walifunga mpaka kufa ili waende MBINGUNI!!!,,,,so sio kwamba serikali inaacha,no wanawachunguza kwa kuchomeka wa2 wao kujifanya nao ni walokole,ila wakiona dalili za hatri ndo wanaingilia kati!!
Hii nimeipenda.
Serikali itakuwa makini sana ikiwa kutakuwa na watu wao ndani ili kuwa na taarifa za mapema.

Yule mama aliwafikisha mbali sana waumini wake, step moja kabla hajawatoa kafara. Ila hao wachunguzi wa kiserikali nao wawe makini maana sisi watu wa kanisani huwa tunaushawishi mkubwa kiasi kwamba anaweza kujikuta mtumishi kificho ameshapewa ushemasi na yeye ndiye anaongoza majukumu ya kimuujiza na kusahau wito wake
 
Hii nimeipenda.
Serikali itakuwa makini sana ikiwa kutakuwa na watu wao ndani ili kuwa na taarifa za mapema.

Yule mama aliwafikisha mbali sana waumini wake, step moja kabla hajawatoa kafara. Ila hao wachunguzi wa kiserikali nao wawe makini maana sisi watu wa kanisani huwa tunaushawishi mkubwa kiasi kwamba anaweza kujikuta mtumishi kificho ameshapewa ushemasi na yeye ndiye anaongoza majukumu ya kimuujiza na kusahau wito wake
yap!!
 
Dini zote ndgu, juzi manzese kuna shekhe nae anaombea, sijui ndo anasomea dua kwa wenye matatizo na blah blah kama za kina mwamposa tu.

Tuwe makini na hizi dini.
Kama huyu niliwahi kuhudhuria mahubiri yake Furahisha mwanza.
Alikuwa anauza maji ya upako kwenye tuchupa. Alitoa demo kidogo tu yale maji yaliibua majini kwa wakina mama karibu wote.

Anasema aliyatoa maji yake uarabuni, baada ya demo aliuza vichupa vya kutosha.
 
Kama huyu niliwahi kuhudhuria mahubiri yake Furahisha mwanza.
Alikuwa anauza maji ya upako kwenye tuchupa. Alitoa demo kidogo tu yale maji yaliibua majini kwa wakina mama karibu wote.

Anasema aliyatoa maji yake uarabuni, baada ya demo aliuza vichupa vya kutosha.
Huwa nashangaa kuona waislam wakisema ukristo unachezewa wakati hadi kwao iko hivyo hivyo.
 
Ni sawa uulize, mbona Rambo kwenye TV anaua Watu lakini serikali ya USA haimshataki
🙂🙂 lakini kuna jamaa katoa ushuhuda wa kanisa lilimuombea bibi mmoja, na mjukuu akachukua maji atatupia chumbani kwa bibi na bibi akafa kweli. Alipokufa kanisa lililipuka kwa furaha nderemo na vifijo.

Huoni kama kuna haja ya uchunguzi wa kifo cha bibi kama kanisa linahusika mkuu.
 
🙂🙂 lakini kuna jamaa katoa ushuhuda wa kanisa lilimuombea bibi mmoja, na mjukuu akachukua maji atatupia chumbani kwa bibi na bibi akafa kweli. Alipokufa kanisa lililipuka kwa furaha nderemo na vifijo.

Huoni kama kuna haja ya uchunguzi wa kifo cha bibi kama kanisa linahusika mkuu.

😆😆😆
Wapo kaole wenzako hapo.
 
Mkuu kwa mujibu wa hiyo sheria ungamo lolote nje ya hao watu waliopewa mamlaka ya ku record confession haliwezi kutolewa kama sehemu ya ushahidi,video hiyo itakayo enda viral haiwezi kutumika kama ushahidi kumbuka kazungumza hayo akiwa kanisani.

Labda akisha fanya confession kama hiyo,mamlaka husika za upelelezi zikusanye ushahidi mwingine nje ya confession yake ambao utamuunganisha kwenye hayo makosa aliyofanya alafu wataweza kumfikisha mahakamani,kumbuka jinai haiozi,kwa mantiki hiyo mahakamani watatumia ushahidi mwingine na sio confession yake ya kanisani.
Mkuu ni kwanini sasa confession ya kanisani haihesabiki, wakati anakuwa ameconfess mwenyewe, tofauti ya confession ya kanisani na ya sehemu nyingine ni nini
 
Uchawi bado ni imani. Labda mfano mwingine; hata kama mmoja atashuhudia waziwazi kwamba alikuwa jambazi na alipora na kuua watu kwa silaha za moto bado serikali itafanya uchunguzi kwa taratibu zake including PGO na sio kumkamata kwa sababu kakiri katika kusanyiko la waabuduo. Na huu ni utaratibu wa toka kale; toka nyakati za mitume sio wa jana wala juzi.
Lakini je confession hiyo hiyo akiifanya sehemu nyingine tofauti na kanisani bado serikali itafanya uchunguzi wake au itamhukumu moja kwa moja
 
Lakini je confession hiyo hiyo akiifanya sehemu nyingine tofauti na kanisani bado serikali itafanya uchunguzi wake au itamhukumu moja kwa moja
Uchunguzi ni sehemu muhimu ya mwenendo wa makosa ya jinai. Hata mtu akiri mwenyewe (nje ya mahakama) kutenda kosa uchunguzi ni lazima. Uchunguzi ndio huibua ushahidi na ushahidi ndio huamua hukumu. Bila ushahidi mahakama itaamua vipi?

Mahali pekee ambapo ushahidi wa mhusika mwenyewe una-sound ni mbele ya jaji na sio vinginevyo tena very cautiously. Waliotunga hizi sheria wana akili sana.
 
Mimi nashauri makanisa yote yafungwe mic kwenye vile vyumba vya kuhungama.
Majambazi wengi sana wanaua kisha weekend wanaenda kusamehewa na mchungaji ambae ukute na yeye anakula mke wa mtu.
Sijui nani atamsamehe yeye.
Hayo watajua wao lkn wakristo toka wameambiwa kuna kusameheana kwa kutoa hela kidogo basi wanafanya maasi chungu nzima kisha wanaenda kumwaga mzigo wote wa madhambi kwa elf 10.

Tena ukiwa na laki 1 wachungaji wanakusamehe hata kwa WhatsApp fasta tu.
Huna haja ya kwenda kanisani.
Na ukiwa na laki 3 mchungaji anakuja popote ulipo kukusamehe.
Yaani Imani za kisanii ni janga la dunia
 
Back
Top Bottom