Kuna mwaka tulikuwa tunafanya kazi somewhere sehemu fulani hivi imetulia sana hauingii hapo kama una cent za kuunga unga, juice hapo unanunua elf 10 Na juice tu ya kawaida sikwambii soda, bia na vitu vingine kama chakula na zaga zingine , mimi nilikuwa naenda kama muhudumiaji mshahara ulikuwa safi sana na kadri unavyohudumia zaidi mshahara unapanda... ilikuwa hatari sana
Kisa hiki hapa
Kulikuwa mdada hapo mkali hatari alikuwa mtu wa kupokea wageni, hiyo ilikuwa juu kabsa ghorofani na huku chini kulikuwa na matengenezo ya club, mafundi walikuwa wanapiga ujenzi, basi hako kadada kana meza yake ghorofa ya nne hapo ndio anapopokea wageni sijui ilikuaje? Akaacha simu akaenda chooni alaf ulikuwa mida ya mafundi kutoka ilikuwa kama saa mbili usiku, mafundi wakapita na simu.. sister kurudi kutoka chooni ajaikuta simu si ndio kuwaita maboss, maboss walikuwa wahindi kuanza kulalamika na kisister hakikuweka msindo wa siri yaani hakikuweka namba za siri kwenye simu yake.. kadada ni kazuri hatari alaf kasomi, msako ukaanza kwenye kamera cctv zao,
Kadada kilio chote kumbe ni kujirikodi akifanya mapenzi na bwana wake, yaani akaanza kuropoka kuwa yeye alilii sim analilia zile picha na video walizokuwa wanachukuana yeye na mtu wake bahati nzuri akaonekana fundi aliyeiba simu akapigiwa simu akaambiwa arudishe simu kuwa ameonekana kwenye kamera mtego, jamaa akadai elf 30 ya kutoka gongo la mboto mpaka masaki wahindi wakatuma fasta kuja jamaa akampa mlinzi sim mlinzi akaileta kwa sister, sister kupata simu tu akaingia whatsapp kuangalia kweli banah jamaa akawa ameshatuma baadhi ya video kwa washikaji zake na kwake pia dada alizidisha kilio full kuzimia palee
Kikubwa alikuwa akilalamika kuwa alikuwa na ndoto kubwa kufanya kazi serikalini yaani awe kiongozi mkubwa uenda wakili maana amesomea sheria au mbunge na uongozi wowote mkubwa sasa akawa analalamika kuwa itakuaje? Amekuwa kiongozi mkubwa na picha zake za video za ngono na picha zinavuja ataiweka wapi sura yake, watu wakawa wanamuhoji sasa dada kipi? Kinakufanya mpaka uchukue video na kupiga picha za utupu akawa anasema mapenzi tu na bwana wake alikuwa akimshawishi na yeye akawa anafanya vile kwa mapenzi tu akawa anasema ila kwa sasa amejifunza atofanya tena ujinga huo watu wakawa wanamwambia kuwa umeshachelewa tena
Akawa nampigia yule fundi kumbembeleza afute hizo picha na awaambie aliowatumia asisambaze jamaa akawa anakataa kuwa ajatuma wakati kwenye sim ya msichana ushahidi upo, yule fundi hakuja tena site alijua ile ni kesi na wasomi wanakufunga na yule dada aliomba likizo kama ya wiki mbili baada ya kuwa poa kiakili ndio akawa anakuja tena kazini
Kidada ni kizuri hatari kifupi alafu kina shepu akivaa viatu vya mchuchumio wee hautoki, kisichana kinene kiasi bwanah wew alaf kinapenda watu hapo kazini maana kinaongea vizur mpaka na watu wa usafi bwanah wewe sijui kipo wapi sasa hivi hiyo ilikuwa 2017.. hiyo hapo masaki
Hii changamoto hasa ipo kwa madada zetu na kupiga picha za utupu au kujirekodi video za utupu ukiwa na bwana wako au kumtumia picha ni mbaya sana hii, wewe fikiria mtu mwenye malengo ya kweli na wewe hawezi furahia picha zako za utupu au mme wako hawezi kukubali uwe unamtumia picha kama hizo jifunzeni baadhi ya dada zetu tunawapenda sana na mnajua.
Usitumie sim vibaya hakikisha una uelewa sahihi wa kutumia hasa hii mitandao ya kijamii ndio uanze kuitumia kama hauwezi bora tu kuachana nayo kwani hauto pungukiwa chochote kile.
Asante