Kwanini wasanii wa maigizo na uchekeshaji wa Kiume wengi huigiza kama Wanawake?

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Katika maisha kuna hatua nyingi sana sisi binadamu tunapitia na kila mmoja ana namna au mbinu yake katika kuyafikia mafanikio. Kwa mukhutadha huo nakwenda moja kwa moja kwenye mada hasa hii fani uchekeshaji ambayo kwa sasa inachezwa zaidi na vijana.

Inakuwaje wasanii wa maigizo na uchekeshaji wa Kiume, huigiza kama Wanawake na sijawahi kuona wachekeshaji wa kike wakiigiza kama wanaume? Au inaonekana wanawake ndo wameboboa zaidi katika visa na mikasa pamoja na vitimbi kuliko wanaume? Karibuni pamoja wakuu.
 
Kuwa mchekeshaji ni kazi ngumu sana maana watu wa kucheka wenyewe siku hizi wako wapi kila mtu kakasirikia maisha yake.

Sasa hawa wachekeshaji wanapokutana na watu wakiokasirika na mbinu zao kudunda lazima akili ziwatume ujinga.
 
Wafuatiliaji wanapangwa kuukubali ushoga. Zamani za kale wachekeshaji walikuwa wanachekesha wakiwa uchi
 
Kuwa mchekeshaji ni kazi ngumu sana maana watu wa kucheka wenyewe siku hizi wako wapi kila mtu kakasirikia maisha yake.

Sasa hawa wachekeshaji wanapokutana na watu wakiokasirika na mbinu zao kudunda lazima akili ziwatume ujinga.
Ha ha ha. Na huenda kukoseka wanaocheka ni kulingana na ugumu wa maisha hasa wakati huu
 
Kipaji kidogo tu. Kuna wachekeshaji maarufu duniani hawaigizi wanawake na bado wanapata washabiki lukuki mfano Trevor Noah wa South Africa au Professor Hamo wa Kenya.
Ni kweli kabisa!
 
Ili uwe mchekeshaji katika dunia ya sasa, unapaswa uwe na akili sana na uwe na upeo mpana wa kutambua mambo mengi na kuweza kuyageuza kuwa comedy itakayowachekesha watu. Wachekeshaji wetu hawana uelewa wala ujuzi wa mambo mengi, kwahiyo wanajikuta vitu pekee walivyo navyo ni vituko vituko vya kitoto na vitu vyepesi vyepesi kama hivyo kujifanya wanawake na lafudhi za ajabu..
 
Hakika huyanenayo. Akili kubwa inahitajika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…