Kwanini wasanii wa Mwanza mnapenda sana kuigiza kisukuma kwenye nyimbo zenu

Kwanini wasanii wa Mwanza mnapenda sana kuigiza kisukuma kwenye nyimbo zenu

Mmmh utakuwa na visa na wasukuma ww, mbona wasanii wengine kibao tu wanachomeka na vilugha vyao mf kina linex,.
Wasanii kibao afu mfano ni linex pekee
 
Ikitokea umehamia mwanza ndio utachoka kabisa na sisi,,, kwani huku ni ndio kuna wasanii kama kina Budagala wao ni full kisukuma na nyimbo zao zinapigwa sana mitaani na kwenye mabaa na daladala pia.. Hao uliowataja ni wachache tu waliotokamo..
Aaah ngosha hilo ulilotaja hapo ni jina la msanii mbona sio la kizungu kama john makin vile
 
Hilo ni swali langu wakuu wa nyumba hii kwanini hawa wasanii wa mwanza hupenda sana kuchanganya kisukuma kwenye nyimbo zao kinawapelekea kufanya hivo au ndo kuendeleza ukabila

COYO MC huyu ni mwana hip pop kutoka mwanza anayetamba na ngoma yake ya njoo badae humu kuna kuna kisukuma kingi sana

DARASA pia huyu naye ni msanii wa hip hop kachanganya kisukuma ngoma zake nyingi mfano ile aliyoimba na mr blue pamoja na hii mpya ya inayoitwa muzik

Fid q huyu ile ngoma yake mpya inayosifiwa na makonda na kigangwala mwanzon imeanza kwa kisukuma kitupu

Young kiler huyu ndo usiseme kila nyimbo natokea mwanza sijui mwanza mwanza kuna nyimbo kaimba na juma natur yan ni kisukuma tupu

Kara jeremiah masanja huyu naye ana nyimbo ameimba kwa kisukuma tu sijui alimanisha nini kwenye ile nyimbo

Dudu baya huyu huchanganya lakin sio sana

Hao tu ni wale wa hip hop tutaendelea badae na wale wabana pua
Huwezi ukasahau unakotoka. Hata Mwl Nyerere alimtolea mfano sir. George Kahama, somewhere alijikuta akitamka Maiwee!
 
Mkulu akianza kubonga kisukuma hadi ana-relax usoni. Mwambie aongee lugha ile ya malkia-duh anakuwa mpole huyo, utakuta anaongea huku kichwa kakipindisha kushoto kijasho chamtiririka kwa mbali. Chezea simple participle tense wew!
 
Lugha ukiijua ni vigumu sana kuacha kuitumia at all, ndo maana hata wasanii kama Fid.Q, AY, Vanessa, Diamond na wengineo wanachomekea kiingereza kwenye nyimbo zao ni kwa sababu wanakijua. Sikiliza hata wasanii wa nje mfano Davido anachanganya lugha za kwao, ni kawaida mkuu vumilia.
hapa nahisi angechomeka lugha tofauti na kabila lao pia wangehoji uhalali wa makabila yao...
 
Mkataa kwao ni mtumwa na ili ufahamike utokeapo lazma utupie kitu kitakachokutambulixha na ndivyo afanyavyo mtu km linex na wengine wengi
 
Uzuri ni lugha ya Taifa siku nyingi tu sana msije sema kwa Rais ni msukuma hii inajulikana miaka mingi! Kuna mtu asiyejua Nduhu Tabu! Anyooshe mkono!
 
Ikitokea umehamia mwanza ndio utachoka kabisa na sisi,,, kwani huku ni ndio kuna wasanii kama kina Budagala wao ni full kisukuma na nyimbo zao zinapigwa sana mitaani na kwenye mabaa na daladala pia.. Hao uliowataja ni wachache tu waliotokamo..
Wasanii Wa Kanda Ya Ziwa.

1. Bhudagala

2.Mchele Mchele

3.Suzy

4.Lady Killy

5.Ya Leo Kali

5.Mwl George Sura 2 !
 
Back
Top Bottom