Kwanini Watanzania tunajenga utamaduni wa kubanana?

Kwanini Watanzania tunajenga utamaduni wa kubanana?

Bro ukitaka kujua watu wanabanana vipi kwenye public, nenda China au India...
China na India hawawezi kukwepa kubanana kutokana na idadi yao kulingana na ukubwa wa ardhi yao. Tanzania hatutakiwi tubanane.
 
Watanzania tuna utamaduni wa kubanana sana. Ukiingia kwenye daladala, hakuna mtu atakayefanya jitihida za kutobanana, utakuta abiria anamwegemea abiria mwingine kila kupata ridhaa mradi tu "sote tubababe."

Konda wa daladala anaweza kujaza abiria kuliko uwezo wa gari na kuwaacha wabanane na wala abiria hao hawawezi kulalamika.

Kwenye ujenzi wa makazi, utaona watu wanajenga mpaka kwenye mpaka wa kiwanja bila kuweka ile futi sita clearance kiasi kuwa mtu hawezi kupita katikakati ya viwanja viwili. Sababu yake ni nini?
Ni saikolojia ya umasikini. Ni kukosa maono ya kuweza kuona zaidi ya kilicho mbele ya macho yetu.

Tuna ardhi kubwa sana lakini tumejenga kwenye miji michache kwa kubanana.

Tuna uwezo wa kuzalisha cha kumtosha kila mtu, lakini wengi wanakufa kwa umasikini unaotokana na ujinga tu.

Katika kitabu cha "Why Nations Fail: The Origins of Power, Prosperity, and Poverty" waandizhi wamejadili mengi sana, lakini, kimoja cha msingi kabisa ni kwamba, nchi zilizoendelea zimejengwa katika misingi ya kumjumuisha kila mmoja, inclusivity.

Sisi tuna unhealthy competition. Tunafungiana fursa kwa njia za mkato ili wachache waweze kubaki juu.

Tunajikuta tunaua ubunifu.

Hapo hatuwezi kuendelea.
 
Kubanana Kama hivi. 😁
db23f75a9b1e280a7a8677e424076501.jpg
 
Watanzania tuna utamaduni wa kubanana sana. Ukiingia kwenye daladala, hakuna mtu atakayefanya jitihida za kutobanana, utakuta abiria anamwegemea abiria mwingine bila kupata ridhaa mradi tu "sote tubababe."

Konda wa daladala anaweza kujaza abiria kuliko uwezo wa gari na kuwaacha wabanane na wala abiria hao hawawezi kulalamika.

Kwenye ujenzi wa makazi, utaona watu wanajenga mpaka kwenye mpaka wa kiwanja bila kuweka ile futi sita clearance kiasi kuwa mtu hawezi kupita katikakati ya viwanja viwili. Sababu yake ni nini?
Hata kwako, mtu una nunua kitanda cha futi sita kwa sita ulalie hauridhiki unaenda kuoa mradi hiko kitanda mlale watu wawili mradi Mbabane tuuu, umezidi watanzania
 
Labda ni wapi ambapo public transport watu hawabanani?

Kuhusu makazi, ukishaamua kujenga kwenye unplanned places kubali usumbufu, kama hutaki nenda sehemu zilizopangilia.

Kuna sehemu inaitwa Tegeta Skansika, ile sehemu walokuwa wanachimba kokoto, kule likitokea na kutokea zimamoto lisiende maana nyumba zimeshikana na barabara hakuna. Kila mtu anajenga anavyojua na tamisemi ipo
 
Watanzania tuna utamaduni wa kubanana sana. Ukiingia kwenye daladala, hakuna mtu atakayefanya jitihida za kutobanana, utakuta abiria anamwegemea abiria mwingine bila kupata ridhaa mradi tu "sote tubababe."

Konda wa daladala anaweza kujaza abiria kuliko uwezo wa gari na kuwaacha wabanane na wala abiria hao hawawezi kulalamika.

Kwenye ujenzi wa makazi, utaona watu wanajenga mpaka kwenye mpaka wa kiwanja bila kuweka ile futi sita clearance kiasi kuwa mtu hawezi kupita katikakati ya viwanja viwili. Sababu yake ni nini?
Ujinga na kukosa ustaarabu
 
Hii imeathiri hata wafugaji, utakuta mtu ana kuku 500 ila banda aliloweka kuku Hao halina uwezo huo, zizi la mbuzi 100 mtu anaswaga humo mbuzi 500, wakati wa ukaguzi wa mifugo au chanjo anapita kwa shida yeye mwenyewe ili mradi tu afurahie kubanana banana mpaka na mbuzi.
 
Watanzania tuna utamaduni wa kubanana sana. Ukiingia kwenye daladala, hakuna mtu atakayefanya jitihida za kutobanana, utakuta abiria anamwegemea abiria mwingine bila kupata ridhaa mradi tu "sote tubababe."

Konda wa daladala anaweza kujaza abiria kuliko uwezo wa gari na kuwaacha wabanane na wala abiria hao hawawezi kulalamika.

Kwenye ujenzi wa makazi, utaona watu wanajenga mpaka kwenye mpaka wa kiwanja bila kuweka ile futi sita clearance kiasi kuwa mtu hawezi kupita katikakati ya viwanja viwili. Sababu yake ni nini?
Ujamaa umetutia ujinga flani ambao itachukua muda mrefu kuondoka.
 
Watanzania tuna utamaduni wa kubanana sana. Ukiingia kwenye daladala, hakuna mtu atakayefanya jitihada za kutobanana, utakuta abiria anamwegemea abiria mwingine bila kupata ridhaa mradi tu "sote tubababe."

Konda wa daladala anaweza kujaza abiria kuliko uwezo wa gari na kuwaacha wabanane na wala abiria hao hawawezi kulalamika.

Kwenye ujenzi wa makazi, utaona watu wanajenga mpaka kwenye mpaka wa kiwanja bila kuweka ile futi sita clearance kiasi kuwa mtu hawezi kupita katikakati ya viwanja viwili. Sababu yake ni nini?
We are black people, we are black people, we are black people!
They are not like us we are not like them.
Our physical appearance are quite different from them, why do you want to look, think and behave like them? We are different people.
Do you want a Monkey to look like Gorila, it will never happen until the end of the time.
Ipo siku utasema kwa nini tusioe kama wao.
Bob Marley aliwahi imba "we will share the shelter" kama unadhani aliimba ujinga shauri yako.
 
Labda ni wapi ambapo public transport watu hawabanani?

Kuhusu makazi, ukishaamua kujenga kwenye unplanned places kubali usumbufu, kama hutaki nenda sehemu zilizopangilia.

Kuna sehemu inaitwa Tegeta Skansika, ile sehemu walokuwa wanachimba kokoto, kule likitokea na kutokea zimamoto lisiende maana nyumba zimeshikana na barabara hakuna. Kila mtu anajenga anavyojua na tamisemi ipo
Public transportation haina maana ya abiria kubanana. In fact basi au tren linaweza kuwa limejaa lakini abiria hawagusani.

Hata maeneo yote yaliyopimwa ni yale ya low density tu ambayo hakuna mbanano. Ukienda Tabata, Segerea, Sinza, Goba kote nyumba zimebanana ingawa ni maeneo yaliyopimwa.
 
Back
Top Bottom