Kwanini watu wanaopendana sana ndio wanaongoza katika kufanyiana mabaya?

Kwanini watu wanaopendana sana ndio wanaongoza katika kufanyiana mabaya?

Hamza Nsiha

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2022
Posts
221
Reaction score
197
Ripoti za utafiti zinaonesha kuwa Tanzania ni nchi mojawapo ambayo inakuja kwakasi katika idadi ya watu wenye matatizo ya afya ya akili. Mpaka sasa kati ya watu wanne basi mmoja wao yupo hatarini kupata matatizo ya afya ya akili.

Pia siku chache hapo nyuma tumesikia kuhusu kulemewa kwa idadi ya wagonjwa matika hospitali ya Afya ya akili~ Milembe, kutokana na kupokea idadi kubwa ya watu wenye matatizo ya afya ya akili kuliko ilivyokawaida.

Ukweli ni kuwa hivi sasa matatizo ya afya ya akili yanahusishwa sana na mahusiano. Hususani wapenzi ambao walikuwa wakipendana sana ndio wanaongoza katika kufanyiana matukio mabaya hadi kutoana uhai.

Binafsi ninaona kwanini watu ambao wanapendana sana wasingekuwa wanaoana. La hasha ni vema ndoa zingekuwa zikifungwa na watu ambao wanapendana kiasi hii itasaidia kupunguza matarajio baina yao na wataishi kwa amani tele.

Hivi sasa mapenzi yaliyopita kiasi yamegeuka kuwa kama hali hatarishi kwa wapenzi badala ya kuwa nguzo bora ya kujenga ndoa imara.

Watu wengi wanaangukia katika misongo ya mawazo sababu ya mahusiano yanayoonekana kuwa ni mazuri kutokana na kupendana sana.

Ikumbukwe tu kuwa, wataalamu wa afya ya akili wanasisitiza kuwa ili kuondoa msongo wa mawazo(Depression) njia mojawapo kuu ni kuondoa kitu kinachokupa huo msongo wa wa mawazo (Stressor).

Je! Unaweza kumuondoa mpenzi wako ambaye unampenda sana kama njia ya kutatua msongo wako wa mawazo katika mahusiano yasiyo na furaha?
 
Mimi nadhani maisha ni zaidi ya mapenzi na ujumla wake.

Changamoto ni vile wengi tumefanya mapenzi kama sehemu muhimu kwenye maisha kuliko hata majs6 yenyewe, hii ni kwa sababu kwenye mapenzi kuna kitu kinapatikana huko nacho ni sex, hio sex ni burudani fulani hivi ambayo umuhimu wake ni mdogo sana lakini wengi wetu tumeipa umuhimu kiasi cha kuona heri kutokuishi kuliko kuikosa au kushare!

Tunaweza kupata burudani nje ya sex na love na pia tujitahidi sana furaha yetu isitoke kwa yoyote isipo mtu binafsi ajipatie furaha mwenyewe.
 
Mimi naona katika hili ipo haja ya Backup team kutoka mbinguni..maana Sisi wenyewe tutakufa mkuu
 
Nyie ambao mnazichakata hadi kimasihara
Kuna tofauti kubwa sana kati ya hilo na serious relation .
Ndio maana mtu anaona heri ang'ang'anie mahusiano fulani hata kama yanamchoma.
 
yaani ila watu eti uko kwenye mahusiano hayakupi furaha, na bado unang’ang’ana humohumo wooi kisa? Utasikia nampenda tumetoka mbali 😅😅😅
Mambo ni hatariiiiiiiiiiiii kwakwel mkuuu
 
Wakolosai 1:13
Naye alituokoa katika nguvu za Giza,akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa mwana na pendo lake ,¹⁴ ambaye katika yeye tuna ukombozi,yaani msamaha wa dhambi.
 
Watu wana shindana umuhimu kwenye mapenzi kila mtu ana jiona wa muhimu ,,kuna mmoja Ali taka kuniletea izo pozy za mala ani nyamazie bla sababu ndo ikawa ticket yake hakuamini.
 
Watu wana shindana umuhimu kwenye mapenzi kila mtu ana jiona wa muhimu ,,kuna mmoja Ali taka kuniletea izo pozy za mala ani nyamazie bla sababu ndo ikawa ticket yake hakuamini.
Hii pia imeua mahusiano mengi sana aan
 
Wakolosai 1:13
Naye alituokoa katika nguvu za Giza,akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa mwana na pendo lake ,¹⁴ ambaye katika yeye tuna ukombozi,yaani msamaha wa dhambi.
Amen ndugu, Mungu akubariki sanaaa
 
Watu wana shindana umuhimu kwenye mapenzi kila mtu ana jiona wa muhimu ,,kuna mmoja Ali taka kuniletea izo pozy za mala ani nyamazie bla sababu ndo ikawa ticket yake hakuamini.
Imagine unadate mtu usipomuanza ye hana habari, ukipiga asipopokea hata haji kukutafuta labda umtafute tena wewe bado kwenye maongezi ni ile unajikuta mambo unajibiwa poa, unaongeza mzima kinajibu mi mzima tu😅😅unaona kabisa unaforce alafu bado unaendelea et oh nampenda 😅😅😅😅
 
Back
Top Bottom