Kwanini watu wanapuuzia kumuomba Mungu wakati Mungu anasikia na kujibu maombi?

Kwanini watu wanapuuzia kumuomba Mungu wakati Mungu anasikia na kujibu maombi?

Kwa aliye matured katika Imani yampasa kuamini tu
#maombi ni kwa mtu aliye katika hofu mchanga kiimani.....✍️
 
Mungu huyu huyu ambaye anaruhusu vita kila kona ya Dunia?
Kama nilivyokujibu awali, uovu uliopo duniani ni matokeo ya dhambi iliyotendwa katika bustani ya Eden. Kuanzia wakati ule dhambi ya uuaji iliingia. Hata hivyo siku inakuja ambapo watenda dhambi wote watatupwa katika moto wa milele. Na walioishi sawasawa na mapenzi ya Mungu wataingia mbinguni, kusikokuwa na vita wala uovu wowote.
 
weka vigezo na mashart
Ili upate unayoyaomba zingatia mambo haya yafutayo:
1. Omba kwa Imani
Marko 11:24 – "Kwa sababu hiyo nawaambia: Mambo yote myaombayo mkisali, amini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu."

2. Omba kwa Jina la Yesu
Yohana 14:13-14 – "Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, ili Baba atukuzwe katika Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya."

3. Omba sawasawa na mapenzi ya Mungu
1 Yohana 5:14 – "Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kwamba tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia."

4. Uwe na moyo safi (Usitende dhambi)
Isaya 59:1-2 – "Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa; wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia."

5. Omba kwa unyenyekevu
2 Mambo ya Nyakati 7:14 – "Ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watanyenyekea, na kuomba, na kunitafuta uso wangu, na kuacha njia zao mbaya; basi nitasikia kutoka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao."

6. Omba kwa uvumilivu bila kukata tamaa
Luka 18:1 – "Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu siku zote, wala wasikate tamaa."

7. Epuka kuomba kwa ajili ya tamaa zako
Yakobo 4:3 – "Mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu."

8. Omba na kufunga
Mathayo 17:21 – "Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga."

Hivyo ni baadhi ya vigezo na masharti ya kuzingatia ili tupate tunayoyaomba
 
Mungu anawapenda watoto na anasikia vibaya wanapofanyiwa uovu(Mathayo 18:6). Lakini kwa sasa, dunia hii imeathiriwa na dhambi ile ya wanadamu wa kwanza, Adam na Hawa. Uovu uliopo ni matokeo ya dhambi zetu wenyewe, sio kosa la Mungu.

Hata hivyo siku ya mwisho, Mungu atamhukumu kila atendaye uovu (Ufunuo 20:12). Hivyo hao wanaobaka watoto usifikiri wako salama wasipotubu.

Mungu hapendi uovu ndiyo maana alimtuma Yesu ili kuleta wokovu. Watu wote duniani wakiokoka, hakutakuwa na mtu wa kubaka watoto.
Kuna vitu vya msingi unaficha ndio maana watu wengi hawana imani manake kama wewe unavyosema ndivyo wasemavyo wachungaji lakini hawasemi siri za ndani; wanaomba kwa njia gani, nini siri ya maombi yenye kujibiwa, namna gani ya kuombo ujibiwe, nk.
 
Asante kwa kuwa wazi. Sasa hatua ya kwanza kabisa ya kujibiwa maombi ni kuwa na uhusiano mzuri na Mungu. Ukiokoka, Mungu anakuwa Baba yako na wewe unakuwa mtoto wake. Ndio maana ya andiko lile la Mt 7:7-12, kwamba Baba yetu wa mbinguni atatupa vitu vilivyo vizuri...

Ukiomba Mungu akupe mahitaji yako wakati bado unaendelea kutenda dhambi, ni vigumu kupata majibu. Mungu hamsikii mwenye dhambi. Soma Yn 9:31 (SUV). Imeandikwa hivi: "Twajua ya kuwa Mungu hawasikii wenye dhambi; bali mtu akiwa ni mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake, humsikia huyo."

Sala ya mwenye dhambi anayoisikia Mungu, ni sala au maombi ya toba. Kama nilivyosema, mwenye dhambi akiishatubu anakuwa mtoto wa Mungu, hapo ndipo lolote aombalo atapewa na Baba(Yn16:23).

Je, uko tayari kuokoka sasa nikuongoze sala ya toba?
Kuokoka ni kufanyaje kwanza ili nisije kukubali mkataba ambao sijausoma
 
Huu uzi hadi nimalize kusoma maoni ya wadau nitakuwa nimepata kitu.
 
Kuna vitu vya msingi unaficha
Hakuna kilichofichwa. Vigezo na masharti ya kujibiwa maombi, vyote vimeandikwa kwenye Biblia. Nimeandika hapo juu masharti ya kuzingatia
 
Kuna vitu vya msingi unaficha ndio maana watu wengi hawana imani manake kama wewe unavyosema ndivyo wasemavyo wachungaji lakini hawasemi siri za ndani; wanaomba kwa njia gani, nini siri ya maombi yenye kujibiwa, namna gani ya kuombo ujibiwe, nk.
Mimi siamini katika kuokoka kama mleta mada anavyosisitiza. Maana hakuna ajuaye ameokolewa hadi ile siku ya mwisho, na kama binadamu tuko prone kutenda dhambi, yaani kuanguka na kuinuka, hata Yesu alisema. Nina msusi wangu "ameokoka" lakini anaishi na mwanaume bila ndoa, sasa yeye na mimi nani mwenye unafuu kwenye eneo la uzinzi? Ni neema tu ya Mungu inatuokoa maana anazijua dhamiri zetu.

Cha msingi, kuomba kwa imani ni kuamini kuwa unachoomba Mungu anaenda kusikia na siyo uombe kwa kujaribu, au uombe huku unafanya njia zako nyingine ovu za kutafuta suluhisho mfano unafanya ushirikina, au unajaribu shortcut mfano huna hela unaiba za ofisi huku ukitarajia kweli Mungu alete majibu, hell no, hutajibiwa.

Ili kujiweka vizuri kiimani na kupokea majibu ya maombi yako, omba na kufunga. Ni muhimu sana maana utakuwa constantly focused na ombi lako siku nzima. Katika biblia kuna watu walifunga siku 3 kama Esther na Wayahudi wenzake. Pia Daniel alifunga kwa siku 21 katika interval ya siku 7 I think. Pia Yesu alifunga kwa siku 40. Angalia hao walifunga kwa sababu gani, yumkini hitaji lako linaweza kufanana na kati ya hao. Pia usiombe kwa tamaa, mfano unasema nataka niwe kama Elon Musk, labda mwambie Mungu nisaidie nipate ahueni ya kukabili mahitaji yangu ya kifedha. Au nisaidie nipate kuwa na mahali pangu pa kuishi (nyumba yangu).

Au mfano huna kazi, unasema Mungu nisaidie nipate kazi siyo nisaidie kazi nije niwe bosi wa ofisi fulani, unaona hiyo tofauti? Shida yako hapo siyo kazi, unataka uwe bosi, sasa hiyo ni tamaa. Ombea tu nafasi kubwa itimie pale inapokuja dalili ya wewe kuwa promoted kwenye hiyo nafasi, maana nyakati hizo shetani hujiinua ukajikuta anapewa mtu mwingine instead, tena unapoomba Mungu akujalie hiyo nafasi omba pia na akuondolee kiburi usije ukamkosea, yaani jinyenyekeze siyo kuweka tamaa mbele ni chukizo kwa Mungu. Maombi kama hayo hayajibiwi, la sivyo nenda tu kwa mganga, ila ujue utateseka tu shetani hasaidii mtu bure.
 
Back
Top Bottom