Kuna vitu vya msingi unaficha ndio maana watu wengi hawana imani manake kama wewe unavyosema ndivyo wasemavyo wachungaji lakini hawasemi siri za ndani; wanaomba kwa njia gani, nini siri ya maombi yenye kujibiwa, namna gani ya kuombo ujibiwe, nk.
Mimi siamini katika kuokoka kama mleta mada anavyosisitiza. Maana hakuna ajuaye ameokolewa hadi ile siku ya mwisho, na kama binadamu tuko prone kutenda dhambi, yaani kuanguka na kuinuka, hata Yesu alisema. Nina msusi wangu "ameokoka" lakini anaishi na mwanaume bila ndoa, sasa yeye na mimi nani mwenye unafuu kwenye eneo la uzinzi? Ni neema tu ya Mungu inatuokoa maana anazijua dhamiri zetu.
Cha msingi, kuomba kwa imani ni kuamini kuwa unachoomba Mungu anaenda kusikia na siyo uombe kwa kujaribu, au uombe huku unafanya njia zako nyingine ovu za kutafuta suluhisho mfano unafanya ushirikina, au unajaribu shortcut mfano huna hela unaiba za ofisi huku ukitarajia kweli Mungu alete majibu, hell no, hutajibiwa.
Ili kujiweka vizuri kiimani na kupokea majibu ya maombi yako, omba na kufunga. Ni muhimu sana maana utakuwa constantly focused na ombi lako siku nzima. Katika biblia kuna watu walifunga siku 3 kama Esther na Wayahudi wenzake. Pia Daniel alifunga kwa siku 21 katika interval ya siku 7 I think. Pia Yesu alifunga kwa siku 40. Angalia hao walifunga kwa sababu gani, yumkini hitaji lako linaweza kufanana na kati ya hao. Pia usiombe kwa tamaa, mfano unasema nataka niwe kama Elon Musk, labda mwambie Mungu nisaidie nipate ahueni ya kukabili mahitaji yangu ya kifedha. Au nisaidie nipate kuwa na mahali pangu pa kuishi (nyumba yangu).
Au mfano huna kazi, unasema Mungu nisaidie nipate kazi siyo nisaidie kazi nije niwe bosi wa ofisi fulani, unaona hiyo tofauti? Shida yako hapo siyo kazi, unataka uwe bosi, sasa hiyo ni tamaa. Ombea tu nafasi kubwa itimie pale inapokuja dalili ya wewe kuwa promoted kwenye hiyo nafasi, maana nyakati hizo shetani hujiinua ukajikuta anapewa mtu mwingine instead, tena unapoomba Mungu akujalie hiyo nafasi omba pia na akuondolee kiburi usije ukamkosea, yaani jinyenyekeze siyo kuweka tamaa mbele ni chukizo kwa Mungu. Maombi kama hayo hayajibiwi, la sivyo nenda tu kwa mganga, ila ujue utateseka tu shetani hasaidii mtu bure.