Precious Diamond
JF-Expert Member
- Jun 9, 2023
- 593
- 1,376
Salama Ijumaa hii?
Kusifiwa ni jambo zuri, hasa ukipewa sifa ikiwa umefanya kitu kizuri. Inakupa hamasa ya kufanya vizuri zaidi. Shida inakuja ukiambiwa kinyume. Yaani mtu akikuchana ukweli unakasirika, unafura na kumuona tu hafai.
Tena ukiambiwa ukweli na mtu aliyekuwa anakusifia kila siku ndio kabisa unaumia na kuona kama dunia imeisha.
Kulikuwa na member humu anamwaga like kwenye kila uzi anaokutana nao, jamaa hadi akawa maarufu, halafu akaja mwamba ambae alikuwa anaponda na kudislike kila uzi na comment anayokutana nayo, palikuwa pamoto humu kila mtu akilalamika.
Viongozi serikalini kila siku tunaona wakisifiwa wanatoa mpaka vyeo kama sadaka, ila kinyume chake wakiambiwa kweli virungu vinatembea, mara watu wanakamatwa na kupotea, yaani tafrani.
Hii inaonesha ni jinsi gani watu wanapenda kusifiwa na kupambwa.
Kama ukweli ni mzuri kwanini watu wengi wasiupende na kufurahia kusifiwa hata kama ni uongo?
Kusifiwa ni jambo zuri, hasa ukipewa sifa ikiwa umefanya kitu kizuri. Inakupa hamasa ya kufanya vizuri zaidi. Shida inakuja ukiambiwa kinyume. Yaani mtu akikuchana ukweli unakasirika, unafura na kumuona tu hafai.
Tena ukiambiwa ukweli na mtu aliyekuwa anakusifia kila siku ndio kabisa unaumia na kuona kama dunia imeisha.
Kulikuwa na member humu anamwaga like kwenye kila uzi anaokutana nao, jamaa hadi akawa maarufu, halafu akaja mwamba ambae alikuwa anaponda na kudislike kila uzi na comment anayokutana nayo, palikuwa pamoto humu kila mtu akilalamika.
Viongozi serikalini kila siku tunaona wakisifiwa wanatoa mpaka vyeo kama sadaka, ila kinyume chake wakiambiwa kweli virungu vinatembea, mara watu wanakamatwa na kupotea, yaani tafrani.
Hii inaonesha ni jinsi gani watu wanapenda kusifiwa na kupambwa.
Kama ukweli ni mzuri kwanini watu wengi wasiupende na kufurahia kusifiwa hata kama ni uongo?