Kwanini Yesu Kristo aliivunja Sabato? Sababu hizi hapa

Kwanini Yesu Kristo aliivunja Sabato? Sababu hizi hapa

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
1,679
Reaction score
2,123
Yesu Kristo alipokuja duniani alifanya mambo mengi ambayo hayaruhusiwi kufanywa siku ya Sabato. Kwa mfano, aliwaponya wagonjwa na pia aliwaruhusu wanafunzi wake wavunje masuke ya nafaka siku ya Sabato.

Hiyo ilikuwa kinyume na sheria ya Sabato. Wakati wa Musa, Mungu aliwaagiza Wana wa Israeli wapumzike siku ya saba ili kukumbuka jinsi walivyokuwa watumwa katika nchi ya Misri na jinsi BWANA Mungu alivyowatoa utumwani na kuwapa pumziko(Kutoka 20:8-11)

Yesu Kristo alipokuja alisema hakuja kuitangua torati bali kuitimiza. Kama ni hivyo, kwanini sasa kuna Maandiko mengi yanayoonyesha kuwa Yesu aliivunja Sabato? Ni kwanini Yesu aliivunja Sabato badala ya kuitimiza?

Iko hivi: Kabla ya kuja kwa Yesu, Nabii Hosea alitabiri kuwa Mungu ataikomesha Sabato (Hosea 2:11). Yesu Kristo ni Mungu, alipokuja aliikomesha Sabato. Ndio sababu Yesu alifanya mambo hayo yaliyopingana na sheria ya Sabato. Yesu alisema Yeye ndiye Bwana wa Sabato. Kwa kuwa Yesu Kristo ni Bwana na aliivunja Sabato, ndiyo sababu Wakristo nao wanaona ni halali kuivunja sabato kwa kuwa Yesu amewaachia kielelezo wafuate nyayo zake (Kol 2:13-14).

Mtume Paulo anaeleza pia kwamba kushika siku na miezi na nyakati na miaka ni kuyarejea mafundisho manyonge yenye upungufu (Gal 4:9-11).

Je, umewahi kujiuliza kwanini katika zile amri kumi, amri ya nne(ya sabato) haipo katika Agano Jipya? Sababu kuu ni hiyo kwamba Yesu aliye Bwana wa Sabato aliikomesha sabato kama ilivyokuwa imetabiriwa ili watu wapate pumziko la kweli kwa kumwendea Yesu, wanaposumbuka na kulemewa na mizigo (Mt 11:28).

Wote wanaokaa ndani ya Yesu wanapumzishwa hapa duniani, na pia watapumzika katika Sabato ya milele mbinguni (Ebr 4:8-11). Fanya bidii uwe miongoni mwa watu hao watakaoingia katika raha hiyo ya milele. Wanaotenda dhambi hawataingia (Ebr 4:1-11; Ufu 14:13).

Kwakuwa Yesu aliivunja Sabato, ndio sababu Wakristo wanasali au kuabudu siku ya Jumapili ambayo ni siku ya kwanza ya juma. Kwa Wakristo:
  • Jumapili ni siku ya ushindi, kwa sababu ndiyo siku ambayo Yesu Kristo alifufuka
  • Ni siku aliyokuja Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu alikuja siku ya Jumapili - siku ya Pentekoste (Mdo 2:1).
  • Jumapili ndiyo siku ambayo kanisa la kwanza lilianza kuhubiri na watu 3,000 wakaokoka na kuanza kukusanyika pamoja katika ibada (Mdo 2; 20:6-12; 1Kor 16:1-2).
Hata hivyo kusali Jumapili sio tiketi ya kwenda mbinguni. Ili tupate tiketi ya kwenda mbinguni ni lazima tukubali kuokoka. Tunaokolewa kwa kutubu dhambi, kukiri na kuamini kuwa Yesu ni Bwana na Mwokozi na sio kwa kushika siku (Rum 10:9-10,13). Kuna watu wanasali Jumapili lakini wakitoka Kanisani wanaenda kufanya dhambi.

Kwaya na Wasanii wa Nyimbo za Injili, siku ya Jumapili wanaimba nyimbo tamu lakini wakitoka kanisani wanasengenya watu, wanasema uongo, na wengine wanafanya uzinzi na kulewa pombe. Nyimbo zinazoimbwa Jumapili na watu wa aina hiyo ni kelele mbele za Bwana. Soma uzi huu hapa 👇 upate ufahamu wa kina kwa nini Mungu anaziita nyimbo “kelele”

 
Roman Catholic ndio wanafundisha hivo sawa ujakomaa kiiman ndgu
 
Yesu Kristo alipokuja duniani alifanya mambo mengi ambayo hayaruhusiwi kufanywa siku ya Sabato. Kwa mfano, aliwaponya wagonjwa na pia aliwaruhusu wanafunzi wake wavunje masuke ya nafaka siku ya Sabato.

Hiyo ilikuwa kinyume na sheria ya Sabato. Wakati wa Musa, Mungu aliwaagiza Wana wa Israeli wapumzike siku ya saba ili kukumbuka jinsi walivyokuwa watumwa katika nchi ya Misri na jinsi BWANA Mungu alivyowatoa utumwani na kuwapa pumziko(Kutoka 20:8-11)

Yesu Kristo alipokuja alisema hakuja kuitangua torati bali kuitimiza. Kama ni hivyo, kwanini sasa kuna Maandiko mengi yanayoonyesha kuwa Yesu aliivunja Sabato? Ni kwanini Yesu aliivunja Sabato badala ya kuitimiza?

Iko hivi: Kabla ya kuja kwa Yesu, Nabii Hosea alitabiri kuwa Mungu ataikomesha Sabato (Hosea 2:11). Yesu Kristo ni Mungu, alipokuja aliikomesha Sabato. Ndio sababu Yesu alifanya mambo hayo yaliyopingana na sheria ya Sabato. Yesu alisema Yeye ndiye Bwana wa Sabato. Kwa kuwa Yesu Kristo ni Bwana na aliivunja Sabato, ndiyo sababu Wakristo nao wanaona ni halali kuivunja sabato kwa kuwa Yesu amewaachia kielelezo wafuate nyayo zake (Kol 2:13-14).

Mtume Paulo anaeleza pia kwamba kushika siku na miezi na nyakati na miaka ni kuyarejea mafundisho manyonge yenye upungufu (Gal 4:9-11).

Je, umewahi kujiuliza kwanini katika zile amri kumi, amri ya nne(ya sabato) haipo katika Agano Jipya? Sababu kuu ni hiyo kwamba Yesu aliye Bwana wa Sabato aliikomesha sabato kama ilivyokuwa imetabiriwa ili watu wapate pumziko la kweli kwa kumwendea Yesu, wanaposumbuka na kulemewa na mizigo (Mt 11:28).

Wote wanaokaa ndani ya Yesu wanapumzishwa hapa duniani, na pia watapumzika katika Sabato ya milele mbinguni (Ebr 4:8-11). Fanya bidii uwe miongoni mwa watu hao watakaoingia katika raha hiyo ya milele. Wanaotenda dhambi hawataingia (Ebr 4:1-11; Ufu 14:13).

Kwakuwa Yesu aliivunja Sabato, ndio sababu Wakristo wanasali au kuabudu siku ya Jumapili ambayo ni siku ya kwanza ya juma. Kwa Wakristo:
  • Jumapili ni siku ya ushindi, kwa sababu ndiyo siku ambayo Yesu Kristo alifufuka
  • Ni siku aliyokuja Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu alikuja siku ya Jumapili - siku ya Pentekoste (Mdo 2:1).
  • Jumapili ndiyo siku ambayo kanisa la kwanza lilianza kuhubiri na watu 3,000 wakaokoka na kuanza kukusanyika pamoja katika ibada (Mdo 2; 20:6-12; 1Kor 16:1-2).
Hata hivyo kusali Jumapili sio tiketi ya kwenda mbinguni. Ili tupate tiketi ya kwenda mbinguni ni lazima tukubali kuokoka. Tunaokolewa kwa kutubu dhambi, kukiri na kuamini kuwa Yesu ni Bwana na Mwokozi na sio kwa kushika siku (Rum 10:9-10,13). Kuna watu wanasali Jumapili lakini wakitoka Kanisani wanaenda kufanya dhambi.

Kwaya na Wasanii wa Nyimbo za Injili, siku ya Jumapili wanaimba nyimbo tamu lakini wakitoka kanisani wanasengenya watu, wanasema uongo, na wengine wanafanya uzinzi na kulewa pombe. Nyimbo zinazoimbwa Jumapili na watu wa aina hiyo ni kelele mbele za Bwana. Soma uzi huu hapa 👇 upate ufahamu wa kina kwa nini Mungu anaziita nyimbo “kelele”

amina ubarikiwe sanaa
japo biblia inasema sabato imebaki kwa watakatifu tuuu,
ile ya kusika siku ilikuwa kivuli cha sabato halisi.

wote waliompokea roh wa mungu wamo kwenye sabato
biblia inasema sabato i aha na waliompokea roho wa mungu wamo kwenye ile raha halisi.

si kushika siku wala saaa wala majira,.
inasikitisha kuona watu wanangali wanashika siku ya sabato na wanajiita wakristo badala ya kujiita wa musa
 
BIBLIA HAISOMWI KAMA KATIBA AU GAZETI LA UDAKU

Yesu Hakuvunja Sabato

Moja ya shtaka kubwa Wayahudi walilomletea Yesu ni kwamba alivunja Sabato. Lakini, je, shtaka hilo lilikuwa sahihi? Wayahudi walimshtumu Yesu kwa mambo mengi, ikiwa ni pamoja na kudai kuwa alijifanya kuwa Mungu (Yohana 10:33), kuponya wagonjwa siku ya Sabato (Luka 13:14), na kuwa na uhusiano na wenye dhambi (Luka 15:2). Hata hivyo, madai yao mara nyingi yalikuwa ya uongo au ya upotoshaji wa ukweli.

Wayahudi Walimshtumu Bila Kuelewa Maandiko

Yesu mwenyewe aliwakemea Wayahudi kwa kutokujua Maandiko na kwa kuweka mapokeo yao juu ya amri za Mungu:

"Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hamkusoma ya kuwa alichokifanya Daudi, hapo alipoona njaa, yeye na wale waliokuwa pamoja naye?" (Mathayo 12:3)

"Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hamkusoma katika torati ya kuwa siku za Sabato makuhani hekaluni huinajisi Sabato, wasipate hatia?" (Mathayo 12:5)

Yesu aliwaambia wazi kuwa hawajui Maandiko wala uweza wa Mungu:

"Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hampotei kwa sababu hii, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu?" (Marko 12:24)

Kwa hiyo, shtaka lao dhidi ya Yesu la kuvunja Sabato lilitokana na kutoelewa maana halisi ya Sabato.

Unabii wa Yesu Kuhusu Sabato Mwaka 70 AD

Katika Mathayo 24, Yesu alitoa unabii wa uharibifu wa Yerusalemu ambao ulitokea mwaka 70 AD, miaka 40 baada ya kifo chake. Katika unabii huu, Yesu aliwaonya wafuasi wake waombe ili wasikimbie wakati wa baridi au siku ya Sabato:

"Ombeni, ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato." (Mathayo 24:20)

Hii inaonyesha kuwa Yesu alijua Sabato bado ingekuwepo hata miaka 40 baada ya kifo chake. Kama Sabato haikuwa na umuhimu tena baada ya msalaba, kwa nini Yesu awaonye wanafunzi wake waombe ili wasikimbie siku ya Sabato?

Je, Yesu hakujua kama Sabato baada ya miaka 40 haitakuwepo? Hapana! Maneno yake yanaonesha kuwa Sabato ilikuwa bado na nafasi yake kwa watu wa Mungu, si tu wakati wa mitume, bali hata katika siku za mwisho.

Sabato Ipo Hadi Siku za Mwisho

Biblia inaonyesha kuwa Sabato bado ni sehemu ya mpango wa Mungu kwa watu wake hadi siku za mwisho:

"Basi imesalia raha ya Sabato kwa watu wa Mungu." (Waebrania 4:9)

Na katika ufalme wa Mungu, wanadamu wote wataendelea kuiheshimu Sabato:

"Na itakuwa, kila mwezi mpya na kila Sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema Bwana." (Isaya 66:23)

Kwa hiyo, hoja kwamba Yesu alivunja Sabato au kwamba Sabato iliondolewa baada ya msalaba haina msingi wa Kibiblia. Yesu hakuvunja Sabato, bali aliifunua maana yake halisi, na unabii wake unaonyesha kuwa Sabato itaendelea kuwepo hadi milele.


EPUKA UPOTOSHAJI
 
Tumekombolewa kwa neema tu

Kwanza Yesu alikufa kwa ajili yetu

Kwa kupigwa kwake sisi tumepona
 
BIBLIA HAISOMWI KAMA KATIBA AU GAZETI LA UDAKU

Yesu Hakuvunja Sabato

Moja ya shtaka kubwa Wayahudi walilomletea Yesu ni kwamba alivunja Sabato. Lakini, je, shtaka hilo lilikuwa sahihi? Wayahudi walimshtumu Yesu kwa mambo mengi, ikiwa ni pamoja na kudai kuwa alijifanya kuwa Mungu (Yohana 10:33), kuponya wagonjwa siku ya Sabato (Luka 13:14), na kuwa na uhusiano na wenye dhambi (Luka 15:2). Hata hivyo, madai yao mara nyingi yalikuwa ya uongo au ya upotoshaji wa ukweli.

Wayahudi Walimshtumu Bila Kuelewa Maandiko

Yesu mwenyewe aliwakemea Wayahudi kwa kutokujua Maandiko na kwa kuweka mapokeo yao juu ya amri za Mungu:

"Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hamkusoma ya kuwa alichokifanya Daudi, hapo alipoona njaa, yeye na wale waliokuwa pamoja naye?" (Mathayo 12:3)

"Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hamkusoma katika torati ya kuwa siku za Sabato makuhani hekaluni huinajisi Sabato, wasipate hatia?" (Mathayo 12:5)

Yesu aliwaambia wazi kuwa hawajui Maandiko wala uweza wa Mungu:

"Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hampotei kwa sababu hii, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu?" (Marko 12:24)

Kwa hiyo, shtaka lao dhidi ya Yesu la kuvunja Sabato lilitokana na kutoelewa maana halisi ya Sabato.

Unabii wa Yesu Kuhusu Sabato Mwaka 70 AD

Katika Mathayo 24, Yesu alitoa unabii wa uharibifu wa Yerusalemu ambao ulitokea mwaka 70 AD, miaka 40 baada ya kifo chake. Katika unabii huu, Yesu aliwaonya wafuasi wake waombe ili wasikimbie wakati wa baridi au siku ya Sabato:

"Ombeni, ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato." (Mathayo 24:20)

Hii inaonyesha kuwa Yesu alijua Sabato bado ingekuwepo hata miaka 40 baada ya kifo chake. Kama Sabato haikuwa na umuhimu tena baada ya msalaba, kwa nini Yesu awaonye wanafunzi wake waombe ili wasikimbie siku ya Sabato?

Je, Yesu hakujua kama Sabato baada ya miaka 40 haitakuwepo? Hapana! Maneno yake yanaonesha kuwa Sabato ilikuwa bado na nafasi yake kwa watu wa Mungu, si tu wakati wa mitume, bali hata katika siku za mwisho.

Sabato Ipo Hadi Siku za Mwisho

Biblia inaonyesha kuwa Sabato bado ni sehemu ya mpango wa Mungu kwa watu wake hadi siku za mwisho:

"Basi imesalia raha ya Sabato kwa watu wa Mungu." (Waebrania 4:9)

Na katika ufalme wa Mungu, wanadamu wote wataendelea kuiheshimu Sabato:

"Na itakuwa, kila mwezi mpya na kila Sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema Bwana." (Isaya 66:23)

Kwa hiyo, hoja kwamba Yesu alivunja Sabato au kwamba Sabato iliondolewa baada ya msalaba haina msingi wa Kibiblia. Yesu hakuvunja Sabato, bali aliifunua maana yake halisi, na unabii wake unaonyesha kuwa Sabato itaendelea kuwepo hadi milele.


EPUKA UPOTOSHAJI
Asante sana kwa kupita hapa. Andaa Biblia yako na notes zako vizuri, ntakurudia
 
Asante sana kwa kupita hapa. Andaa Biblia yako na notes zako vizuri, ntakurudia
Ungejibu hoja zangu vzr,kabla hujaandaa notes maana Huwa mnavuruga maandiko jibu maswali haya

1. Ikiwa Yesu alivunja Sabato, kwa nini hakuweza kushitakiwa kwa kuvunja sheria ya Musa, bali kwa mujibu wa tafsiri ya Mafarisayo?


2. Kwa nini Yesu aliwaambia Wayahudi kwamba hawajui Maandiko wala uweza wa Mungu (Marko 12:24)? Je, hili linaashiria nini kuhusu madai yao dhidi yake?


3. Katika Mathayo 24:20, Yesu aliwaonya wanafunzi wake waombe ili wasikimbie siku ya Sabato miaka 40 baada ya kifo chake. Je, hii haithibitishi kuwa Sabato bado ilikuwa na maana kwa Wakristo hata baada ya msalaba?


4. Ikiwa Sabato iliondolewa, kwa nini Biblia inasema "Imesalia raha ya Sabato kwa watu wa Mungu" (Waebrania 4:9)?


5. Kwa mujibu wa Isaya 66:23, wanadamu wote wataendelea kuiheshimu Sabato hata katika ufalme wa Mungu. Je, hii haithibitishi kuwa Sabato haikuwa ya muda mfupi bali ni ya milele?
 
Yesu Kristo alipokuja duniani alifanya mambo mengi ambayo hayaruhusiwi kufanywa siku ya Sabato. Kwa mfano, aliwaponya wagonjwa na pia aliwaruhusu wanafunzi wake wavunje masuke ya nafaka siku ya Sabato.

Hiyo ilikuwa kinyume na sheria ya Sabato. Wakati wa Musa, Mungu aliwaagiza Wana wa Israeli wapumzike siku ya saba ili kukumbuka jinsi walivyokuwa watumwa katika nchi ya Misri na jinsi BWANA Mungu alivyowatoa utumwani na kuwapa pumziko(Kutoka 20:8-11)

Yesu Kristo alipokuja alisema hakuja kuitangua torati bali kuitimiza. Kama ni hivyo, kwanini sasa kuna Maandiko mengi yanayoonyesha kuwa Yesu aliivunja Sabato? Ni kwanini Yesu aliivunja Sabato badala ya kuitimiza?

Iko hivi: Kabla ya kuja kwa Yesu, Nabii Hosea alitabiri kuwa Mungu ataikomesha Sabato (Hosea 2:11). Yesu Kristo ni Mungu, alipokuja aliikomesha Sabato. Ndio sababu Yesu alifanya mambo hayo yaliyopingana na sheria ya Sabato. Yesu alisema Yeye ndiye Bwana wa Sabato. Kwa kuwa Yesu Kristo ni Bwana na aliivunja Sabato, ndiyo sababu Wakristo nao wanaona ni halali kuivunja sabato kwa kuwa Yesu amewaachia kielelezo wafuate nyayo zake (Kol 2:13-14).

Mtume Paulo anaeleza pia kwamba kushika siku na miezi na nyakati na miaka ni kuyarejea mafundisho manyonge yenye upungufu (Gal 4:9-11).

Je, umewahi kujiuliza kwanini katika zile amri kumi, amri ya nne(ya sabato) haipo katika Agano Jipya? Sababu kuu ni hiyo kwamba Yesu aliye Bwana wa Sabato aliikomesha sabato kama ilivyokuwa imetabiriwa ili watu wapate pumziko la kweli kwa kumwendea Yesu, wanaposumbuka na kulemewa na mizigo (Mt 11:28).

Wote wanaokaa ndani ya Yesu wanapumzishwa hapa duniani, na pia watapumzika katika Sabato ya milele mbinguni (Ebr 4:8-11). Fanya bidii uwe miongoni mwa watu hao watakaoingia katika raha hiyo ya milele. Wanaotenda dhambi hawataingia (Ebr 4:1-11; Ufu 14:13).

Kwakuwa Yesu aliivunja Sabato, ndio sababu Wakristo wanasali au kuabudu siku ya Jumapili ambayo ni siku ya kwanza ya juma. Kwa Wakristo:
  • Jumapili ni siku ya ushindi, kwa sababu ndiyo siku ambayo Yesu Kristo alifufuka
  • Ni siku aliyokuja Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu alikuja siku ya Jumapili - siku ya Pentekoste (Mdo 2:1).
  • Jumapili ndiyo siku ambayo kanisa la kwanza lilianza kuhubiri na watu 3,000 wakaokoka na kuanza kukusanyika pamoja katika ibada (Mdo 2; 20:6-12; 1Kor 16:1-2).
Hata hivyo kusali Jumapili sio tiketi ya kwenda mbinguni. Ili tupate tiketi ya kwenda mbinguni ni lazima tukubali kuokoka. Tunaokolewa kwa kutubu dhambi, kukiri na kuamini kuwa Yesu ni Bwana na Mwokozi na sio kwa kushika siku (Rum 10:9-10,13). Kuna watu wanasali Jumapili lakini wakitoka Kanisani wanaenda kufanya dhambi.

Kwaya na Wasanii wa Nyimbo za Injili, siku ya Jumapili wanaimba nyimbo tamu lakini wakitoka kanisani wanasengenya watu, wanasema uongo, na wengine wanafanya uzinzi na kulewa pombe. Nyimbo zinazoimbwa Jumapili na watu wa aina hiyo ni kelele mbele za Bwana. Soma uzi huu hapa 👇 upate ufahamu wa kina kwa nini Mungu anaziita nyimbo “kelele”

KIJANA ACHA KUCHEZEA MAANDIKO, HATA PAPA NA WAKATOLIKI WAASISI WA IBADA YA JUMAPILI WANAJUA UKWEL

WEWE UNASALI KWA TAPELI MWAMPOSA AMEANZISHA KANISA JUZI AKITOKEA IPINDA MBEYA NAOMBA UJIBU HAYA MASWALI

  1. Ikiwa Yesu Kristo aliikomesha Sabato kama inavyodaiwa, kwa nini aliwaonya wanafunzi wake waombe ili wasikimbie siku ya Sabato katika Mathayo 24:20, ambayo ilikuwa unabii wa miaka 40 baada ya kifo chake?
  2. Hosea 2:11 inazungumzia hukumu juu ya Waisraeli kwa sababu ya dhambi zao, si juu ya kukomeshwa kwa Sabato kwa watu wote wa Mungu. Je, ni sahihi kutumia andiko hili kama uthibitisho kuwa Mungu alikomesha Sabato kwa kila mtu?
  3. Yesu aliposema kuwa Yeye ni Bwana wa Sabato (Mathayo 12:8), je, alimaanisha kuwa ameikomesha Sabato, au kwamba Yeye ndiye mwenye mamlaka juu yake na anaitimiza kwa uhalisia wake?
  4. Ikiwa Yesu alivunja Sabato, je, hilo halingemfanya kuwa mwenye dhambi kwa mujibu wa sheria ya Musa (Kutoka 31:14)? Na kama Yesu alikuwa mwenye dhambi, angewezaje kuwa sadaka isiyo na waa kwa ajili ya wokovu wetu (1 Petro 1:18-19)?
  5. Ikiwa kushika siku ni "kurudi kwenye mafundisho manyonge" kama inavyodaiwa kwa kutumia Wagalatia 4:9-11, kwa nini Biblia inasema wazi katika Waebrania 4:9 kwamba "Imesalia raha ya Sabato kwa watu wa Mungu"?
  6. Ikiwa amri ya Sabato ilikoma, kwa nini katika Isaya 66:23 inasemwa kwamba katika mbingu mpya na nchi mpya, watu wote watakuja kuabudu mbele za Mungu "Sabato baada ya Sabato"?
  7. Yesu aliposema kuwa hakuja kutangua Torati bali kuitimiza (Mathayo 5:17), je, hiyo haimaanishi kwamba alikuja kuonyesha maana halisi ya Sabato badala ya kuikomesha?
  8. Ikiwa Wakristo wanaabudu Jumapili kwa sababu ya kufufuka kwa Yesu, je, kuna amri yoyote katika Biblia inayosema kuwa Sabato imebadilishwa kutoka Jumamosi kwenda Jumapili?
  9. Katika Luka 23:56, hata baada ya kifo cha Yesu, wanafunzi wake waliheshimu Sabato na kupumzika kama ilivyoagizwa. Je, hili halionyeshi kuwa Sabato bado ilikuwa ikizingatiwa hata baada ya msalaba?
  10. Kwa nini Wakristo wengi wa kwanza, akiwemo Mtume Paulo, waliendelea kuiheshimu Sabato na walikusanyika siku ya Sabato kwa maombi na mafundisho (Matendo 13:42-44, 16:13, 17:2)? Je, kama Sabato ilikuwa imekoma, kwa nini Paulo hakuwaambia watu waache kuiheshimu?
 
Mitaani Hali NI Tete nyinyi wenzetu bado mpo na sabato .Na jirani yangu NI muislam pure lakini futari anakula chumban kwake sad simuelewi namuuliza vipi ananijibu ANASAVE NA DAKU PIA HALI TETE.
 
BIBLIA HAISOMWI KAMA KATIBA AU GAZETI LA UDAKU

Yesu Hakuvunja Sabato

Moja ya shtaka kubwa Wayahudi walilomletea Yesu ni kwamba alivunja Sabato. Lakini, je, shtaka hilo lilikuwa sahihi? Wayahudi walimshtumu Yesu kwa mambo mengi, ikiwa ni pamoja na kudai kuwa alijifanya kuwa Mungu (Yohana 10:33), kuponya wagonjwa siku ya Sabato (Luka 13:14), na kuwa na uhusiano na wenye dhambi (Luka 15:2). Hata hivyo, madai yao mara nyingi yalikuwa ya uongo au ya upotoshaji wa ukweli.

Wayahudi Walimshtumu Bila Kuelewa Maandiko

Yesu mwenyewe aliwakemea Wayahudi kwa kutokujua Maandiko na kwa kuweka mapokeo yao juu ya amri za Mungu:

"Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hamkusoma ya kuwa alichokifanya Daudi, hapo alipoona njaa, yeye na wale waliokuwa pamoja naye?" (Mathayo 12:3)

"Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hamkusoma katika torati ya kuwa siku za Sabato makuhani hekaluni huinajisi Sabato, wasipate hatia?" (Mathayo 12:5)

Yesu aliwaambia wazi kuwa hawajui Maandiko wala uweza wa Mungu:

"Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hampotei kwa sababu hii, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu?" (Marko 12:24)

Kwa hiyo, shtaka lao dhidi ya Yesu la kuvunja Sabato lilitokana na kutoelewa maana halisi ya Sabato.

Unabii wa Yesu Kuhusu Sabato Mwaka 70 AD

Katika Mathayo 24, Yesu alitoa unabii wa uharibifu wa Yerusalemu ambao ulitokea mwaka 70 AD, miaka 40 baada ya kifo chake. Katika unabii huu, Yesu aliwaonya wafuasi wake waombe ili wasikimbie wakati wa baridi au siku ya Sabato:

"Ombeni, ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato." (Mathayo 24:20)

Hii inaonyesha kuwa Yesu alijua Sabato bado ingekuwepo hata miaka 40 baada ya kifo chake. Kama Sabato haikuwa na umuhimu tena baada ya msalaba, kwa nini Yesu awaonye wanafunzi wake waombe ili wasikimbie siku ya Sabato?

Je, Yesu hakujua kama Sabato baada ya miaka 40 haitakuwepo? Hapana! Maneno yake yanaonesha kuwa Sabato ilikuwa bado na nafasi yake kwa watu wa Mungu, si tu wakati wa mitume, bali hata katika siku za mwisho.

Sabato Ipo Hadi Siku za Mwisho

Biblia inaonyesha kuwa Sabato bado ni sehemu ya mpango wa Mungu kwa watu wake hadi siku za mwisho:

"Basi imesalia raha ya Sabato kwa watu wa Mungu." (Waebrania 4:9)

Na katika ufalme wa Mungu, wanadamu wote wataendelea kuiheshimu Sabato:

"Na itakuwa, kila mwezi mpya na kila Sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema Bwana." (Isaya 66:23)

Kwa hiyo, hoja kwamba Yesu alivunja Sabato au kwamba Sabato iliondolewa baada ya msalaba haina msingi wa Kibiblia. Yesu hakuvunja Sabato, bali aliifunua maana yake halisi, na unabii wake unaonyesha kuwa Sabato itaendelea kuwepo hadi milele.


EPUKA UPOTOSHAJI
OK, kwa fikra zako umeona kwamba mimi Biblia ninaisoma kama gazeti la Udaku. Sawa. Sasa naomba wewe unayeisoma kwa 'macho manne' unielimishe niijue vizuri Sabato kama wewe unavyoijua. Ntakuuliza maswali. Ninayo maswali mengi. Lakini ntakuuliza swali moja moja ili nihakikishe maswali yangu yote unayajibu kwa kina.
1. Je, sheria au masharti yote ya Sabato unayatekeleza/unayatimiza? Kama sio yote, nitajie yale ambayo huyatekelezi na uniambie ni kwa sababu gani
 
Subiri kwanza usijibu swali hilo, kwa sababu umeniwahi na maswali yako. Acha niyapitie nikujibu. Ila nikuonye uongo ni dhambi. Unasema nasali kwa Mwamposa na huna ushahidi wowote.
 
OK, kwa fikra zako umeona kwamba mimi Biblia ninaisoma kama gazeti la Udaku. Sawa. Sasa naomba wewe unayeisoma kwa 'macho manne' unielimishe niijue vizuri Sabato kama wewe unavyoijua. Ntakuuliza maswali. Ninayo maswali mengi. Lakini ntakuuliza swali moja moja ili nihakikishe maswali yangu yote unayajibu kwa kina.
1. Je, sheria au masharti yote ya Sabato unayatekeleza/unayatimiza? Kama sio yote, nitajie yale ambayo huyatekelezi na uniambie ni kwa sababu gani
Nilijua tu maswali niliyokuuliza hutaweza kuyajibu, kama kweli unajiamini na usomaji wako wa maandiko ilikuwa simple tu kujibu maswali niliyokuhoji hapo juu

Kitendo cha kutafuta uchochoro ni wazi umeongopa

Na wasomaji wanaofata watakuwa wamejionea
 
Subiri kwanza usijibu swali hilo, kwa sababu umeniwahi na maswali yako. Acha niyapitie nikujibu. Ila nikuonye uongo ni dhambi. Unasema nasali kwa Mwamposa na huna ushahidi wowote.
Kusali kwa mwamposa ,ni ishara ya wapotoshaji

Wewe kama husali kwa mwamposa basi unasali kwa Hawa MATAPELI wanaofungua makanisa kama uyoga kwa kutoelewa nyaraka za Paulo au Hawa wanaotanguliza matumbo mbele

Nilipo mtandao unasumbua sana, naomba ujibu hayo maswali kwa utaratibu na usahihi wa MAANDIKO,hata mjinga na maamuma akisoma aone kweli Sabato ilifutwa ,sio ujibu bla blaa tu,

Maana na asilimia 100 hata Mchungaji au muanzilishi wa dhehebu au kanisa unalosali hapa ,ukimtaja na uhakika 100% anajua kwanini mwasali jumapili na anajua Sabato ni jumamos ,na haikufutwa Bali mmebeba Upagani wa Roma ,kama mlivyobeba X mass, Easter , Halloween,Na upagani mwingine


Hizi nyingine za kusema Yesu alifuta sijui kilikwenda kimerudi ni sarakasi tu,

Mimi nitarud kesho kuona kama umejibu hayo maswali

Ni mpumbavu pekee ambaye anasema Yesu alifuta Sabato ,halafu mwaka huo huo 33AD ANASEMA ombeni kukimbia kwenu isiwe wakati wa Sabato ,hapo anaongelea tukio la 70AD na mwisho wa Dunia

Sasa kwa akili ya kula maharagwe tu utaona ni upotoshaji wa maandiko kumsingizia Yesu


Huyo huyo Yesu alishutumiwa na mafarisayo kuwa anatoa pepo kwa belzbubu ,anavunja Sabato, n.k

MLIVYO wakurupukaji mnasema alivunja Sabato kwa kigezo cha shutuma za wayahudi ,

Ila shutuma nyingine mnazikataa


Mitume na manabii wote hakuna hata mmoja aliyefanya ibada jumapili kwa kigezo Yesu amefufuka

Ufufuko wa Yesu alisema tusherehekee kwa kumega mkate na kutawazana miguu ,maandiko yapo wazi

Kasome historia ya kanisa ,toka awali wamefanya ibada lini ,kasome hata mababa wa awali ,


Then utakuja kukuta ibada ya jumapili imeanza mwaka 321 AD ,mitume na manabii wote wameshakufa ndio unaletewa hiyo ibada .
 
SASA WEWE ENDELEA KUWASIKILIZA KINA MWAMPOSA,KIBOKO YA WACHAWI, GWAJIMA,SUGUYE,MZEE WA UPAKO, BUSHIRI, KUHANI MUSA MWASHA,NA MATAPELI WENGINE


Sikia hapa Mungu mwenye mbingu anachosema

Isaya 66:22-23 BHN


[22] “Kama vile mbingu mpya na dunia mpya nitakazoumba zitakavyodumu milele kwa uwezo wangu, ndivyo wazawa wako na jina lako litakavyodumu. [23] Katika kila sikukuu ya mwezi mpya, na katika kila siku ya Sabato, binadamu wote watakuja kuniabudu. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.


SASA KAMA GWAJIBOY, MWAMPOSA ,NA MATAPELI WENGINE WANA MBINGU YAO ISIYO NA SIKU YA SABATO ENDELEA KUWASIKILIZA
 
Yesu Kristo alipokuja duniani alifanya mambo mengi ambayo hayaruhusiwi kufanywa siku ya Sabato. Kwa mfano, aliwaponya wagonjwa na pia aliwaruhusu wanafunzi wake wavunje masuke ya nafaka siku ya Sabato.

Hiyo ilikuwa kinyume na sheria ya Sabato. Wakati wa Musa, Mungu aliwaagiza Wana wa Israeli wapumzike siku ya saba ili kukumbuka jinsi walivyokuwa watumwa katika nchi ya Misri na jinsi BWANA Mungu alivyowatoa utumwani na kuwapa pumziko(Kutoka 20:8-11)

Yesu Kristo alipokuja alisema hakuja kuitangua torati bali kuitimiza. Kama ni hivyo, kwanini sasa kuna Maandiko mengi yanayoonyesha kuwa Yesu aliivunja Sabato? Ni kwanini Yesu aliivunja Sabato badala ya kuitimiza?

Iko hivi: Kabla ya kuja kwa Yesu, Nabii Hosea alitabiri kuwa Mungu ataikomesha Sabato (Hosea 2:11). Yesu Kristo ni Mungu, alipokuja aliikomesha Sabato. Ndio sababu Yesu alifanya mambo hayo yaliyopingana na sheria ya Sabato. Yesu alisema Yeye ndiye Bwana wa Sabato. Kwa kuwa Yesu Kristo ni Bwana na aliivunja Sabato, ndiyo sababu Wakristo nao wanaona ni halali kuivunja sabato kwa kuwa Yesu amewaachia kielelezo wafuate nyayo zake (Kol 2:13-14).

Mtume Paulo anaeleza pia kwamba kushika siku na miezi na nyakati na miaka ni kuyarejea mafundisho manyonge yenye upungufu (Gal 4:9-11).

Je, umewahi kujiuliza kwanini katika zile amri kumi, amri ya nne(ya sabato) haipo katika Agano Jipya? Sababu kuu ni hiyo kwamba Yesu aliye Bwana wa Sabato aliikomesha sabato kama ilivyokuwa imetabiriwa ili watu wapate pumziko la kweli kwa kumwendea Yesu, wanaposumbuka na kulemewa na mizigo (Mt 11:28).

Wote wanaokaa ndani ya Yesu wanapumzishwa hapa duniani, na pia watapumzika katika Sabato ya milele mbinguni (Ebr 4:8-11). Fanya bidii uwe miongoni mwa watu hao watakaoingia katika raha hiyo ya milele. Wanaotenda dhambi hawataingia (Ebr 4:1-11; Ufu 14:13).

Kwakuwa Yesu aliivunja Sabato, ndio sababu Wakristo wanasali au kuabudu siku ya Jumapili ambayo ni siku ya kwanza ya juma. Kwa Wakristo:
  • Jumapili ni siku ya ushindi, kwa sababu ndiyo siku ambayo Yesu Kristo alifufuka
  • Ni siku aliyokuja Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu alikuja siku ya Jumapili - siku ya Pentekoste (Mdo 2:1).
  • Jumapili ndiyo siku ambayo kanisa la kwanza lilianza kuhubiri na watu 3,000 wakaokoka na kuanza kukusanyika pamoja katika ibada (Mdo 2; 20:6-12; 1Kor 16:1-2).
Hata hivyo kusali Jumapili sio tiketi ya kwenda mbinguni. Ili tupate tiketi ya kwenda mbinguni ni lazima tukubali kuokoka. Tunaokolewa kwa kutubu dhambi, kukiri na kuamini kuwa Yesu ni Bwana na Mwokozi na sio kwa kushika siku (Rum 10:9-10,13). Kuna watu wanasali Jumapili lakini wakitoka Kanisani wanaenda kufanya dhambi.

Kwaya na Wasanii wa Nyimbo za Injili, siku ya Jumapili wanaimba nyimbo tamu lakini wakitoka kanisani wanasengenya watu, wanasema uongo, na wengine wanafanya uzinzi na kulewa pombe. Nyimbo zinazoimbwa Jumapili na watu wa aina hiyo ni kelele mbele za Bwana. Soma uzi huu hapa 👇 upate ufahamu wa kina kwa nini Mungu anaziita nyimbo “kelele”

kwa hiyo wanaoabudu jumamosi wanatenda dhambi ?
 
Hakuvunja sabato, aliitimiza kwa kutofuata sheria walizojiwekea mafarisayo, waliweka sheria za kipuuzi kwamba huwezi kula bila kunawa mikono, Yesu na wanafunzi wake walikuwa na njaa walipita shambani kuchuma chakula wakaanza kula bila kunawa, Yesu akawaambia kimuingiacho binadamu hakimnajisi asipoosha mikono kabla ya kula, kwa bahati mbaya biblia nyingine watafsiri wameweka mabano kwa maoni yao kwamba alimaanisha tunaweza kula chpchote na kufuta sheria za wanyama walioruhusiwa na kukatazwa kuliwa
 
Back
Top Bottom