Unazoita dispensary pengine ni za magumashi, umesema lengo ununue dawa zao... au kama ni za serikali pengine ni utaratibu rasmi.
Hiyo unayoita karatasi ni 'prescription', wala sio kwajili yako... inaandikwa dawa na maelekezo ya matumizi.
Ile unaandikiwa ili ukachukue dawa FAMASI, sasa kama dawa umepata unaihitaji ya kazi gani?
Siku hizi mifumo imeboreshwa, hakuna cha karatasi ni electronics unapewa namba tu nenda famasi chukua dawa anza kutumia kwa kuzingatia maelekezo.
Utapewa uende nayo ikiwa tu dawa hazipatikani hapo hospitali, na inategemea na aina ya dawa.