Sang'udi
JF-Expert Member
- May 16, 2016
- 9,138
- 22,236
Tufwate njia ya msalaba
Tuifwate mpaka Kalvario
Tusimamepo bila haya
Msalaba, Msalaba, huponya roho
Sala mbele ya altare
Ee Mkombozi wangu, nimekuja leo kufuata njia ile uliyoshika siku ya kufa sadaka yetu. Nimetubu dhambi zangu zote; ninataka kugeuza mwendo wangu; ninaomba kwako niwapatie roho za waamini marehemu waliomo toharani, rehema zote zilizotolewa na Kanisa kwa njia ya msalaba.Nawe Maria Bikira Mtakatifu, uliyefuata njia ile ya nyuma ya mwanao Yesu, uniangalie kwa wema, unitie moyo mkuu, nisipende dhambi tena, nikivumilia kazi na usumbufu na mateso na matukano yatakayonipata.