Kweli Ndoa yataka Moyo.....

Kweli Ndoa yataka Moyo.....

Ndugu zanguni yamenikuta na naomba ushauri wenu,Mimi ninaishi na mume wangu yapata miaka miwili sasa,nina mpenda sana Mume wangu na ninaamini kuwa naye ananipenda pia.Ila kuna tatizo linanisumbua sana juu yake ambalo linanipa wasiwasi kiasi kwamba nashindwa kuelewa hatma ya mahusiano yetu ya ndoa kwa maana ya kwamba nahofia yasije yakaingia shubiri na ile imani nlionayo juu yake ikateteleka.Ni hivi kabla ya kunioa mimi aliwahi kuwa na mahusiano na wanawake wengine ila mwanamke wa mwisho ambaye aliachana nae amekua akiendelea kuwasiliana na mume wangu na kila ninapohoji juu ya hilo Mume wangu hunijibu kuwa hauna kitu kinachoendelea baina yetu ni rafiki yangu tu wakawaida na hana shida yoyote na sisi kwanza huwa anapiga simu na kutuma meseji za kutujulia hali,anyways nimejitahidi sana kuwa na mtizamo chanya na kuuambia moyo wangu uamini hivyo.Ila siku zinavyokwenda nikaona mazoea yanakua sio mazuri kwa maana wakati mwingine humpigia simu ana hutuma meseji humueleza mume wangu kuwa amemmiss sana na anataka kuonana nae na vitu kama hivyo.Nlimwambia mume wangu mawasiliano na huyo mpenzi wako wa zamani hayanibariki hata kidogo naomba uwe na mipaka na ikibidi uache kwa maana yananiumiza mimi zaidi,aliniahidi kufanya hivyo na kweli kwa kipindi fulani kazi ilipungua ila sasa leo ametuma tweets kuhusu mume wangu kwenye mtandao wa twitter kitu ambacho kimeniuma maana anaeleza jinsi anavyofurahia tendo la ndoa na mume wangu na baada ya kuliona hilo nkampigia mume waqngu kumweleza akaniambia atampigia simu kumsema juu ya hilo na kumuonya.Badala yake kilichotokea yule mwanamke alituma tweets za kunitukana na kunidhalilisha mimi kitu ambacho kinaniuma sana kwa maana mume wangu anasema yule mwanamke ni rafiki mzuri tu na hana shida hata kidogo.Nisaidieni ushauri ndugu zangu je niendelee kuvumilia hayo yote yanayojitokeza na kuamini maneno ya mume wangu kuwa huyo mwanamke hana shida na sisi ama nifanyenye?Naomba ushauri wenu katika hili.....

Pole sana, mketishe mmeo akueleze vizuri kwa upole, upendo na unyenyekevu huenda kuna vitu havipendi kwako ndo maana anarudi kwa x wake kuvitafuta
 
Pole mydia. We ushafuga tatizo hapo.

Hakuna mahusiano ya kawaida hapo.. La muhimu ni kumpa mumeo ukweli wake ya kuwa hautaki kabisa kusikia hayo mahusiano na huyo bibie.

Kama ataendelea nayo tena kwa kukuonyeshea u need to do something else.

Usitumie ubabe (nguvu) kutatua hili as hautasaidia kitu na utaumia zaidi.

Mwombe Mungu akusaidie haya ni majaribu.. Sali kuhakikisha ndoa yako inasimama imara na haitetereshwi na huyo dada. (Aidha.. Usiangaike kujibizana nae coz mwenye shida ni mumeo)

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
ikute huwa anakuponda huko,inauma sana kwa kweli.MUITE MUNGU

Na hii ndio shida kubwa.. Kimada akifikia hatua ya kutanua mbavu na kuhakikisha wewe unajua uwepo wake lazima kuna kitu kinampa confidence si bure.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Ndugu zanguni yamenikuta na naomba ushauri wenu,Mimi ninaishi na mume wangu yapata miaka miwili sasa,nina mpenda sana Mume wangu na ninaamini kuwa naye ananipenda pia.Ila kuna tatizo linanisumbua sana juu yake ambalo linanipa wasiwasi kiasi kwamba nashindwa kuelewa hatma ya mahusiano yetu ya ndoa kwa maana ya kwamba nahofia yasije yakaingia shubiri na ile imani nlionayo juu yake ikateteleka.Ni hivi kabla ya kunioa mimi aliwahi kuwa na mahusiano na wanawake wengine ila mwanamke wa mwisho ambaye aliachana nae amekua akiendelea kuwasiliana na mume wangu na kila ninapohoji juu ya hilo Mume wangu hunijibu kuwa hauna kitu kinachoendelea baina yetu ni rafiki yangu tu wakawaida na hana shida yoyote na sisi kwanza huwa anapiga simu na kutuma meseji za kutujulia hali,anyways nimejitahidi sana kuwa na mtizamo chanya na kuuambia moyo wangu uamini hivyo.Ila siku zinavyokwenda nikaona mazoea yanakua sio mazuri kwa maana wakati mwingine humpigia simu ana hutuma meseji humueleza mume wangu kuwa amemmiss sana na anataka kuonana nae na vitu kama hivyo.Nlimwambia mume wangu mawasiliano na huyo mpenzi wako wa zamani hayanibariki hata kidogo naomba uwe na mipaka na ikibidi uache kwa maana yananiumiza mimi zaidi,aliniahidi kufanya hivyo na kweli kwa kipindi fulani kazi ilipungua ila sasa leo ametuma tweets kuhusu mume wangu kwenye mtandao wa twitter kitu ambacho kimeniuma maana anaeleza jinsi anavyofurahia tendo la ndoa na mume wangu na baada ya kuliona hilo nkampigia mume waqngu kumweleza akaniambia atampigia simu kumsema juu ya hilo na kumuonya.Badala yake kilichotokea yule mwanamke alituma tweets za kunitukana na kunidhalilisha mimi kitu ambacho kinaniuma sana kwa maana mume wangu anasema yule mwanamke ni rafiki mzuri tu na hana shida hata kidogo.Nisaidieni ushauri ndugu zangu je niendelee kuvumilia hayo yote yanayojitokeza na kuamini maneno ya mume wangu kuwa huyo mwanamke hana shida na sisi ama nifanyenye?Naomba ushauri wenu katika hili.....

Tisa karibu na kumi, Zake au zako zinakaribia punguza pupa katika kuliendea hilo! Manake anafanye kusudi ili awakosanishe! na actually dhamira yake inaelekea kutimia (according to your thread)
 
khaaaaa. huyo mwnamke ni mshezi na wewe unakubali kuonewa.mkabe mumeoa a to z!
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
wat if anatuma post twitter kukuumiza!
wat if mumeo kweli ana mahusiano na ex wake
wat if mumeo anafurahia ex wake anavokurusha roho
wat if mumeo bado anampenda ex wake
wat if mumeo anamtuma ex wake kufanya yote hayo!
wat if mumeo hasemi kweli juu ya ex wake
wat if !wat if !wat if!wat if!
nawaza tu kwa sauti mdogo wangu!
katika hili
1.ukipigana vita ya nyama huwezi!pigana vita ya kiroho!
2.mkalishe chini mumeo umpe msimamo wako
3.mpe nafasi ya kuufanyia kazi
4.baada ya muda chek tatizo kama bado lipo!
thn fanya maamuzi magumu!
 
It's hard to love someone and not be loved and return but what the more pain to love someone and never feel the carage to let the parson to know how you feel maybe god just want to make you fell meet the wrong parson when finally you meet the right parson you will know how to be a greatfull for that gift love is when you take away the feeling the passion and to be remain relationship and found out you care for that parson and third things in your life when you meet sameone who means a lot to you and find out at the end it was never the end to be it just to let them go. When the door happens close another opens but haven't time to seem so longer to close the door . The best kind of friend a friend the kind you can just be with never say a word and then make a way feeling like it was the best conservation over hand.
It's true that we don't know what we got until we lose it but it also we don't know what we are missing until it arrive.
Given someone all you love and never show that then love it back don't except love and return just wait it until it grow in their heart but if it dosen't be contain it to grow in your's .
There are thing you love to hear that you wouldn't nerve hear from the parson you would like to hear from but don't be so bland if you will hear from the sameone who said it from their heart .
Never say goodbye if you still want to try never give up if you still fell can't go on never say you don't love a parson any more if you can't let go.
Love come to those who still hope who those has been disappointed to those who still believe or have still to love to those has been heat before, to those who has the carage and faith to be trust again.
It take only a minutes to get a crush to someone only houur to like sameone only a day to love sameneone but it take so life time to forget sameone.
 
wat if anatuma post twitter kukuumiza!
wat if mumeo kweli ana mahusiano na ex wake
wat if mumeo anafurahia ex wake anavokurusha roho
wat if mumeo bado anampenda ex wake
wat if mumeo anamtuma ex wake kufanya yote hayo!
wat if mumeo hasemi kweli juu ya ex wake
wat if !wat if !wat if!wat if!
nawaza tu kwa sauti mdogo wangu!
katika hili
1.ukipigana vita ya nyama huwezi!pigana vita ya kiroho!
2.mkalishe chini mumeo umpe msimamo wako
3.mpe nafasi ya kuufanyia kazi
4.baada ya muda chek tatizo kama bado lipo!
thn fanya maamuzi magumu!
Thanks for the advice coz am going to work for them an hopefuly i will come out with a constructive decision...thanks alot...
 
I think you are 99% correct, mumewe ndio ana entertain hayo madudu; ni Zombie wa X wake and he is not over her. Bidada, awe na roho ngumu apende kwa akili na imani. Ikiwezekana amuombe mumewe wakacheck afya, akikataa watengane kiunyumba na asali sana na kufunga huenda Mungu akarestore ndoa yake.

Unaonaje, aje this weekend tumfungue kwa maombi ya Moto wa Roho Mtakatifu? Tumshirikishe na mwenyekiti wa baraza la walei gfsonwin na muhesabu sadaka Asprin.

wat if anatuma post twitter kukuumiza!
wat if mumeo kweli ana mahusiano na ex wake
wat if mumeo anafurahia ex wake anavokurusha roho
wat if mumeo bado anampenda ex wake
wat if mumeo anamtuma ex wake kufanya yote hayo!
wat if mumeo hasemi kweli juu ya ex wake
wat if !wat if !wat if!wat if!
nawaza tu kwa sauti mdogo wangu!
katika hili
1.ukipigana vita ya nyama huwezi!pigana vita ya kiroho!
2.mkalishe chini mumeo umpe msimamo wako
3.mpe nafasi ya kuufanyia kazi
4.baada ya muda chek tatizo kama bado lipo!
thn fanya maamuzi magumu!
 
Last edited by a moderator:
Na hii ndio shida kubwa.. Kimada akifikia hatua ya kutanua mbavu na kuhakikisha wewe unajua uwepo wake lazima kuna kitu kinampa confidence si bure.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Nazidi kumwomba Mungu azidi kunipa ujasiri na nguvu katika hili ili mwisho wa siku nifanye maamuzi ya busara na nisimwonee mtu
 
I think you are 99% correct, mumewe ndio ana entertain hayo madudu; ni Zombie wa X wake and he is not over her. Bidada, awe na roho ngumu apende kwa akili na imani. Ikiwezekana amuombe mumewe wakacheck afya, akikataa watengane kiunyumba na asali sana na kufunga huenda Mungu akarestore ndoa yake.

Unaonaje, aje this weekend tumfungue kwa maombi ya Moto wa Roho Mtakatifu? Tumshirikishe na mwenyekiti wa baraza la walei gfsonwin na muhesabu sadaka Asprin.
hili la boldini ni la msingi na sekondari!sawa fellow rev mother.
 
mwambie mumeo

1. achague either wewe au huyo mwanamke

2. Au achague wewe uwe urudiane na ex wako.

inshort huyo mwanaume mpumbavu ndo maana anaruhusu nyumba yake kuvurugwa na hawara.

 
Pole sana, mketishe mmeo akueleze vizuri kwa upole, upendo na unyenyekevu huenda kuna vitu havipendi kwako ndo maana anarudi kwa x wake kuvitafuta

kwanini huwa tunaamini sana kuwa kutoka nje ni mapungufu ya mwenza !
WAKATI MWINGINE HUWA TUNATOKA NJE KWA KUWA WENZI WETU NI WAKAMILIFU MPAKA TUNATAMANI KUFANYA DHAMBI TUWACHAFUE!mwanadamu huwa simwelewi kwa kweli!simwelewi kabisa!yani kabisaaaaaa!
 
kwanini huwa tunaamini sana kuwa kutoka nje ni mapungufu ya mwenza !
WAKATI MWINGINE HUWA TUNATOKA NJE KWA KUWA WENZI WETU NI WAKAMILIFU MPAKA TUNATAMANI KUFANYA DHAMBI TUWACHAFUE!mwanadamu huwa simwelewi kwa kweli!simwelewi kabisa!yani kabisaaaaaa!

Welcome on board rev.mom; ninaongeza idadi ya free and critical thinkers wa MMU!
 
Welcome on board rev.mom; ninaongeza idadi ya free and critical thinkers wa MMU!

im honored mpenzi!
mi hapa huwa pananishangaza kweli!ndo mana naumia sana mtu akibaki kujikunyata na kuamini kuwa uzinzi wa mume au wa mkewe ni kwa kuwa yeye mke au mume ana mapungufu mahali!
ushawahi kuwa na kila kitu kiasi cha kutamani the opposite? sasa ndo hii!
 
hahahaaaa.

mumeo anakula mzigo.....tena hana adabu na wala hakuheshimu.....tikisa kiberiti,utapata jibu.....
 
sitaki kukwambia pole, ila nataka kukwambia kwamba hakuna maisha ambayo hayana milima. ingawa aina ya vilima hutofautiana kati ya mtu na mtu lakini vyote ni vilima na lazima muhusika apande tena atulize akili apande kwa busara asije akajajuta baadae.

tuje upande wa huu mlima wako, kwanza umenikumbusha mbali sana enzi hizo nikiwa MISRI hapa Kaunga atakumbuka vyema namaanisha nini. wakati huo ANNA alipokuwa ananitesa kwenye ndoa. Lakini namshukuru sana Mungu leo hii niko KANAANI nakula maziwa na asali.

Sasa mwali nikupe ushuhuda wangu kidogo, binafsi niliangalia nahitaji nini katika maisha yangu, je ndoa yangu bado naipenda?? nikapata jibu ndio, je mume wangu bado ni mzuri nikapata jibu ndio nikajiuliza tatizo ni nini?? nikapata jibu ni mwanamke mwenzangu hapa nikasema sitoruhusu mwanamke mwenzangu anitese maishani mwangu. sasa nitafanyeje??

nikasema nitafanya haya yafuatayo nitamwona mume wangu mzuri kuliko kwanza, kisha nitaanza kusali kuombea ndoa yangu. neno la Mungu linasema hivi ndoa na iheshimiwe na watu wote, istoshe Mungu anasema yyte alalaye na mwanamke asiyekuwa mke wake anazini na zinaa huaribu hekalu la Mungu so mume wangu kama kichwa cha familia ni hekalu la Mungu kuliharibu inamaana naharibu kichwa cha nyumba yangu.

nilitubu kwaajili ya Mume wangu, kisha nikamtenga na yule mwnamke kwa maombi ya moto wa RMT na damu ya Yesu. mfunike mumeo kwa damu ya Yesu, mzungushie moto wa roho mtakatifu mwekee utisho wa Mungu uwe ndio utukufu wake.

ukijifunza kusali maomabi haya usiku kabla ya saa 10 usiku basi utaona majibu ya Mungu muda mfupi tu. mwenzio mie hadii nilikua nampiga upofu Anna kwa maombi na ndio maana hata alipotolewa ndani hakuona aibu iliyokuwa mbele yake manake alitoka uchi na kitenge changu.

usilale ukalemaa ukategemea hurum ya mumeo, tegemea maombi ya vita na uwe mshindi kwenye maombi haya tena usiwe mpole sema na Mungu wako unataka nini na mwambie adui yako ambaye ni shetan kwamba hana uwezo wa kulipa kisasi juu yako wala familia yako.

hebu acha kulalamika anza leo tena unapoanza kuomba panda sadaka ya mbegu kwamba unaipanda ili Mungu akufanye uvune ndoa njema, mweleze mungu aikumbuke sadaka yako ya mbegu na weleze kabisa kwamba unataka kumpiga upofu huyo rafiki yenu asiione ndoa yako na wala mwanamke yyte yule kahaba asiione na unataka uavune ndoa yeney amani na furaha.

naamini utakuwa umenielewa vyema mpendwa wangu. nakutakia kwaresma njema na Mungu akutane na haja ya moyo wako.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom